Huyu shemeji yangu simuelewi

Huyu shemeji yangu simuelewi

Narasa

Member
Joined
Aug 2, 2017
Posts
7
Reaction score
7
Habari zenu wakuu,

Naombeni mawazo yenu,

Dada yangu kanifuata leo ofisini akinieleza matatizo yake kama kaka yake ukweli nimemwambia asubiri mpaka kesho nitampa jibu.

Dada yangu ameolewa na mtu mwenye cheo kikubwa tu serikalini cha ajabu wana miaka zaidi ya kumi hawana hata kibanda wamepanga jumba tu la maana.

Anavyonieleza amemshauri sana mumewake wajenge, hataki mwishoni mwanaume akamwambia chukua mkopo anza utakapoishia nitamalizia.

Akaomba mkopo kapewa mwanaume kujua mke kapata mkopo tena hataki kutoa ushirikiano, akimuuliza kama mume basi tafuta fundi anamwambia unaharaka gani? Toa basi ramani anamwambia subiri huu mwezi wa 2 mkopo uko tu benki hata hazungumzii kabisa habari za kujenga nanachokazania kila saa nikumweleza jinsi alivyo na madeni mara hela imepungua anataka kuagiza gari.

Wakuu dada yuko njia panda na mimi kuingilia maisha yao sitaki, je nimshauri afanye nini?
 
Kwenye maisha ya familia nyumba ni muhimu sana. Naona shemeji yako anaishi maisha ya ndoa, hafikirii maisha ya familia.
Nyumba inaweza ikawa si kipaumbele kwa baadhi ya watu, hasa nchi za ng'ambo kama ulaya na marekani, wao akipata apartment kazi kamaliza. lakini kwa nchi zetu za kiafrika ni tofauti, hata kama umepanga nyumba nzuri kiasi gani, bado utaonekana huna maisha. Hata kama unapenda maisha ya kupanga jenga nyumba yako tu uendelee na kupanga, heshima itakuja.

Mwambie dada yako ajenge nyumba ya gharama yeyote aiwezayo (nikiamini kiwanja wanacho). Ikiwezekana ajenge hata bila kumshirikisha mumewe maana hakuna ushirikiano. Kama itamuwia vigumu mwambie awashirikishe nduguze (akina wewe), akajenge hata kwao maana huko mbele hajui nini kitatokea, pengine mumewe hana mpango wa kuishi nae hadi dahari.
 
Hiyo ndoa itakuwa na mashaka hapo.


Maana ya ndoa ni ushirikiano kuelewana kuvumiliana.

Sasa hapo mwingine yupo huku mwngine kule.
 
huyo shemeji ni tatizo.kwa kumshauri dada yako ajenge kimpango wake.asisubiri mchango wa jamaa yake na tena kama hiko kiwanja walinunua kwa pamoja aachane nacho,atafute kiwanja kingine asimamishe nyumba itamsaidia sana baadae.AFUATE FORMULAR HII YA WANAWAKE WOTE DUNIANI:-
"CHANGU NI CHANGU NACHAKE NI CHANGU PIA" BILA HIVYO ITAKULA KWAKE
 
Dada yako afanye mambo kwa siri
asimwambie Huyu mwanaume mipango yake. Shost alimfanyia mume surprise mume anatoka safari anamwambia tumeshahama tunaishi huku sikuhizi. Ingawa pesa nyingi ilitoka kwenye joint account lakini kujenga ni mawazo ya mke
 
Dada yako naona in mtu mwelewa, akijenga bila kumshirikisha mumewe, mwanamume akija kugundua hayo ndoa itakuwa hatarini kuvunjika kabisa. Kwa kuwa dada yako ni mwelewa, nashauri achukue sehemu ya mkopo agharimie mchoro wa ramani ya nyumba, na atafute fundi aanze ujenzi kwenye kiwanja chao, na amweke wazi mumewe kwenye kila hatua anayoiendea.
Kuficha mambo kwenye ndoa sio busara hata kidogo.
Kumbuka ''Usifanye jambo lolote kwa kulipiza kama unapenda kuishi ktk ndoa''.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwambie dada yako aanze tu ujenzi wake tena kwa siri bila kumshirikisha huyo mumewe ambe ni mbumbumbu wa maisha. Mtie moyo vile vile kwani faida yake atakuja kuiona baadae maana huyo shemeji yako bado ana akili za kitoto.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu una Dada mzuri na busara, nisingekuwa nimeoa, ningekuja kleta posa kama kuna wadogo zako! Ushauri was Apejiwe ni mzuri mno,mno ajabu! Naongeza kama ndoa ya hao wawili ni ya kanisani wapate ushauri was viongozi wa kiroho au la wewe pamoja na mtu was karibu upande was shemeji yako, mtafuteni shemeji yako mweleze. Ipo ndoa ninayoijua ilivunjika kwa hatua iliyofanywa kwa hatua na ushauri was Dada yangu SKY Clet, matokeo una kuwa na Mali lakini utulivu wa akili hakuna na watoto pia kama mnao! Mtoa mada msifu sana Dada yako ni mcha Mungu wa kweli!
 
Dada yako afanye mambo kwa siri
asimwambie Huyu mwanaume mipingo yake. Shost I alimfanyia mume surprise mume Anatolia safari anakwambia tumehama tunaishi Huku sikuhizi. Ingawa pesa nyingi I kutoka kwenye joint account lakini kujenga ni mawazo ya mke
Sounds Good..but
In short wako wanaume, ambao hawatajisikia Vizuri, akiona mke amemzidi Maarifa kwa kafanya kitu kinachoonekana kama hicho.
Hapa yahitajika maarifa na hekima sana.

Na kwa kumutathmini huyu Mbaba kwenye huu Uzi, anaweza kua type hiyo..
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dada yako afanye mambo kwa siri
asimwambie Huyu mwanaume mipango yake. Shost alimfanyia mume surprise mume anatoka safari anamwambia tumeshahama tunaishi huku sikuhizi. Ingawa pesa nyingi ilitoka kwenye joint account lakini kujenga ni mawazo ya mke
Yaani wewe ndo unaegemea nyumba ya mabua.... Hata pale padogo palipobaki unapabomoa. Inaonekana hao watu wana kiwanja ila huyo mama anatumia lugha ambayo inamfanya bwashe ajione bwege. Inaonekana kila mwanaume akifikiria kitu mwanamke anakuwa ahead, na huyo mwanaume anajiona inferior.....

Halafu mbona huyo dada yetu Kama anataka sana huo mjengo?? Au anataka kumuua shemeji nini?? Usijekuta shemeji kashtukia kuwa atatolewa roho mjengo ukikamilika..... Kwa sababu Kama angekuwa na lengo la kujenga kwa maendeleo ya familia, angeshirikisha marafiki na mshenga wa ndoa na sio kukushirikisha wewe mdogo wake..... Au ndo unataka bwashe aporomoshe mjengo uje uumilik baadae......


Nakushauri, usitie neno moja kwa moja..... Mwambie dada aongee na marafiki wanakaa na bwashe bar.
 
Huyo shemeji yako ni mshirikina na aliambiwa na mganga asije akafanya kosa akajenga nyumba
 
Ana mke mwingine ambae kamjangea. Dada yako yupo nae tu kwakuwa ndo alimuoa wa kwanza.

Ushauri. Dada yako atafute kiwanja ajenge nyumba yake kwa sasa aipangishe.

Who knows?? Mme akifa dada hatotoseka na watoto.

Mwanaume ana roho mbaya hawazi hata maisha ya watoto?? Au hawana watoto??
 
Mwambie dada yako ajenge kimya kimya kwa uwezo wake maadam ameshamshirikisha bwashee kwenye hilo na bwashee haelewiki aendelee tu na ujenzi wake .
 
Duuh!!! This world bana.... sasa huyo kidume anataka life gani??? Lazima sister ajiongeze kumsaidia huyo mpenda anasa la sivyo nguvu zikiisha tutakumbukia wale wakurugenzi wa zamani zile....

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom