Huyu mtu anajitambulisha kama pastor mstaafu na amekuwa maarufu sana kwenye media.
Jana kuna jamaa mmoja aliyesikia moja ya mafunzo yake kuhusiana na mahusiano ya mapenzi na ndoa.
Alimsikia akisema kina mama wenye umri wa miaka zaidi ya 40 wanapenda sana vijana wadogo kama ambavyo wanaume wenye umri mkubwa wanavyopenda vibinti.
Sasa jamaa analalamika sana mkewe sasa hivi kawa mkali na hamjali na wala hana hamu ya kufanya naye tendo la ndoa.Alivyosikia kauli hizi tena zinatoka kwa mtumishi anayejiita wa Mungu, aliamini hadi kufikia kumtilia mashaka mke wake kuwa huenda ana tembea na wavulana wadogo.Jamaa alisema hali hii ikiendelea,atamgawanya mkewe vipande viwili.Hahitaji kuwa na ushahidi zaidi ya hicho anachofanyiwa na mkewe.
Sasa nimeandika hivi,na kuomba huyu Mzee (Pastor) adhibitiwe,kwa kuwa analeta hofu katika ndoa za watu.Ujumbe wake hauna matumaini zaidi ya kuleta taharuki.Huyu jamaa akimchinja mkewe kwa hisia tu kwa vile amesikia kutoka kwa Mchungaji ,hamuoni hiyo ni hatari sana?
Nimesikia matukio ya mauaji yameongezeka sana hasa yanayohusiana na wivu wa mapenzi.Na Waziri akatoa rai kwa viongozi wa dini wawasaidie wananchi.Itakuwaje kwa wachungaji kama hawa wanaochochea taharuki kama hizi?
Kwa uelewa wangu mdogo, akina mama wanapofikia umri wa utu uzima,huwa wana kipindi cha mpito kutoka katika siku zao za kila mwezi kuingia kipindi ambacho hawaoni tena siku zao(menopause),huwa wanapata dalili za kuwa wenye wasi wasi,hasira,kutojisikia kushiriki tendo la ndoa,kutokana na mabadiliko ya homoni( post menopausal syndrome)Hali hii isipotibiwa huweza hata kusababisha ndoa kuvunjika.
Sasa watu hawa wasio na elimu ya kutosha wakiachwa tu waendelee na mafunzo yao yasiyo na tafiti,yanayotolewa tu kama hadithi za kizee,wanaweza kuleta balaa sana katika jamii kwa vile jamii yetu bado inawaamoni sana viongozi wanaojiita watumishi wa Mungu
Jana kuna jamaa mmoja aliyesikia moja ya mafunzo yake kuhusiana na mahusiano ya mapenzi na ndoa.
Alimsikia akisema kina mama wenye umri wa miaka zaidi ya 40 wanapenda sana vijana wadogo kama ambavyo wanaume wenye umri mkubwa wanavyopenda vibinti.
Sasa jamaa analalamika sana mkewe sasa hivi kawa mkali na hamjali na wala hana hamu ya kufanya naye tendo la ndoa.Alivyosikia kauli hizi tena zinatoka kwa mtumishi anayejiita wa Mungu, aliamini hadi kufikia kumtilia mashaka mke wake kuwa huenda ana tembea na wavulana wadogo.Jamaa alisema hali hii ikiendelea,atamgawanya mkewe vipande viwili.Hahitaji kuwa na ushahidi zaidi ya hicho anachofanyiwa na mkewe.
Sasa nimeandika hivi,na kuomba huyu Mzee (Pastor) adhibitiwe,kwa kuwa analeta hofu katika ndoa za watu.Ujumbe wake hauna matumaini zaidi ya kuleta taharuki.Huyu jamaa akimchinja mkewe kwa hisia tu kwa vile amesikia kutoka kwa Mchungaji ,hamuoni hiyo ni hatari sana?
Nimesikia matukio ya mauaji yameongezeka sana hasa yanayohusiana na wivu wa mapenzi.Na Waziri akatoa rai kwa viongozi wa dini wawasaidie wananchi.Itakuwaje kwa wachungaji kama hawa wanaochochea taharuki kama hizi?
Kwa uelewa wangu mdogo, akina mama wanapofikia umri wa utu uzima,huwa wana kipindi cha mpito kutoka katika siku zao za kila mwezi kuingia kipindi ambacho hawaoni tena siku zao(menopause),huwa wanapata dalili za kuwa wenye wasi wasi,hasira,kutojisikia kushiriki tendo la ndoa,kutokana na mabadiliko ya homoni( post menopausal syndrome)Hali hii isipotibiwa huweza hata kusababisha ndoa kuvunjika.
Sasa watu hawa wasio na elimu ya kutosha wakiachwa tu waendelee na mafunzo yao yasiyo na tafiti,yanayotolewa tu kama hadithi za kizee,wanaweza kuleta balaa sana katika jamii kwa vile jamii yetu bado inawaamoni sana viongozi wanaojiita watumishi wa Mungu