Huyu ndiye mwanzilishi wa chama kipya cha Umoja Party (UP)

FDR franklin delano roosevelt wetu Ndio Huyu!BADO mdogo kwa umri!kwa Sasa ana miaka 49 Hadi 2025 atakuwa na miaka 52 ukijumlisha na 12 atakuwa na miaka 64!!ngoja Tuone!!
 
Mkuu ninakusoma kwani wewe ni moto mara moja. Hurembi wala hukopeshi. Kuleta mabadiliko si lelemama.

Kada uliyoiangazia ndiyo iliyofaulu kuleta mabadiliko kulikoshindikana. Kule ambako shoka lilivunjika lakini mpini ukabakia pale pale 😁😁.

Hao ndiyo walioleta Mapinduzi duniani. Ongelea Russia, Ufaransa, China, Zanzibar na sehemu lukuki. The Lumpen Proletariats.

Lumpen Proletariat, (German: “rabble proletariat”), according to Karl Marx in The Communist Manifesto, the lowest stratum of the industrial working class, including also such undesirables as tramps and criminals.

View attachment 1997849

Hao ndiyo hiyo mitu. CCM wanawaogopa kuliko ukoma. Juhudi zote zinafanyika kuhakikisha hawafikii kwenye mawazo kama yako.

Ulipo ni mwanzo mzuri.

Hapa ndipo wengine wanapopotea maboya.

Ninaunga mkono hoja:

"Kama kuna mmachinga humu na anakubaliana na hoja zako tujuane na tujikusanye kwa ajili kufanya maamuzi haya magumu."
Iwapo Chadema wangekuwa makini wajaze haraka pengo la kuwabeba wanyonge kifalsafa halafu waachane na sera nyepesi za kumchafua Magufuli all the time na kuwananga wasukuma na kanda ya ziwa hailipi kisiasa. Wajikite kuibua falsafa mpya ya kuwatetea wananchi wa chini kama enzi za dr Slaa,kupitia katiba mpya, kuibua ufisadi, maonevu na dhana ya haki mtambuka. Agenda hizi wasipoziwahi si muda mrefu CCM ilivyo makini itavifanyia kazi mapema km enzi za awamu ya tano na wataendelea kusindikiza siasa ni Agenda na falsafa sahihi.Asubuhi njema
 
Mtu anakwambia hivyo vyama vyengine vyote ni matawi ya ccm au wanatumika na ccm ila ajabu unakuta wanashirikiana na vyama hivyo hivyo kupambana na huyo huyo ccm, tumeona Ukawa ila pia tukaona ushirikiano wa Chadema na ACT.

Siasa za bongo sio za kuzichukulia serious kabisa.
 
Mmmmmmh either kimekuja kupunguza kura za Chadema au kuna kundi kubwa toka mboga mboga ambalo halikubaliani na mkulima mkuu
 
Iwapo Chadema wangekuwa makini wajaze haraka pengo la kuwabeba wanyonge kifalsafa halafu waachane na sera nyepesi za kumchafua Magufuli all the time na kuwananga wasukuma na kanda ya ziwa hailipi kisiasa. Wajikite kuibua falsafa mpya ya kuwatetea wananchi wa chini kama enzi za dr Slaa,kupitia katiba mpya, kuibua ufisadi, maonevu na dhana ya haki mtambuka. Agenda hizi wasipoziwahi si muda mrefu CCM ilivyo makini itavifanyia kazi mapema km enzi za awamu ya tano na wataendelea kusindikiza siasa ni Agenda na falsafa sahihi.Asubuhi njema
Chadema imekufa ila magufuli legacy inaishi milele
 
Back
Top Bottom