kasase kafuku
Member
- Apr 7, 2012
- 27
- 0
Nawatakia kila la heri hayo ndo maendeleo kisiasa.Mageuzi hayaepukiki zama hizi.Ni vigumu kuzuia ndevu kuota.
Nami namfahamu Mtatiro tukiwa chuo, kiukweli bila unafiki wala kuvambavamba maneno, jamaa alikuwa imara sana, kweli alikuwa kwa masilahi ya wanafunzi, sijajua kama ule moyo na kujitolea na kusimama imara hata katikati ya vitisho bado anao. Lakini jamaa alikuwa vizuri sana kwa kweli.Huyu jamaa siwezi kumsahau kama ni majembe huyu jamaa ni jembe. Nikikumbuka mgomo mmoja hivi wa kupinga kuchangia 40percent, serikali nzima ya daruso ilirud nyuma jamaa akaongoza mapambano mwanzo mpaka mwisho. Pamoja na vitisho na kuitwa ikulu mara kadhaa jamaa alisimama imara! Naamini majukumu na matatizo ya watanzania anayajua vema
Mtemvu ana nguvu sana. Mtatiro asilete siasa zake uchwara
Sasa anatokaje sombetini mpaka Kinondoni? Mbona amepita majimbo mengi sana hapo njiani?
Iko wazi kuwa ukimsimamisha kugombea kisiwa cha Pemba, John, James, Peter hata kama anafaa vipi hawezi kupita. Ila ukimsimamisha Hemed, Abdul, Hamis hata kama hawafai watapita.
The same applied to Temeke, Julius Mtatiro ni kiongozi mzuri sana lakini Temeke atatwanga maji kwenye kinu???
Juma nature??? Bunge linakwenda kuwa genge sio mda!
Hapiti, mtapoteza muda.
Mbona kuna wakati Temeke kulikuwa na Mbunge anaitwa Augustino?
Tatizo Mtatiro alikosea kujiunga na chama alichomo sasa hivi.Ndugu Julius mtatiro anatarajiwa kugombea ubunge jimbo la Temeke Kwa tiketi ya ukawa kupitia chama cha CUF.
Wakati huo huo Mh. Ally Bananga atasimamishwa Kwa tiketi ya CHADEMA katika jimbo la Kinondoni.
Nawasilisha.
Uzawa ni uzushi tu , huyu Mtemvu baada ya kupata ubunge mbona amehama Temeke ?Kweli siasa kiboko watu wanazungumzia mpaka mambo ya uzawa?
Nguvu ya kuwatafutia dada zetu kazi za kufua nepi ?Mtemvu ana nguvu sana. Mtatiro asilete siasa zake uchwara
kwa nini mtatiro asiende kugombea kwao kijijini mtemvu pamoja na u ccm wake ni mtoto wa mjini anajua shida zetu baba yake mtemvu ni muhanga wa taifa hili km ni mageuzi awekwe mzawa kwa tiketi ya ukawa tutampigia kura
Ndugu Julius mtatiro anatarajiwa kugombea ubunge jimbo la Temeke Kwa tiketi ya ukawa kupitia chama cha CUF.
Wakati huo huo Mh. Ally Bananga atasimamishwa Kwa tiketi ya CHADEMA katika jimbo la Kinondoni.
Nawasilisha.