Huyu nabii ametokea wapi mbona ametrend sana?

Huyu nabii ametokea wapi mbona ametrend sana?

Iko HV nimepita pita mtandao fln na kuona picha ya kijana anasemekana Ni nabii na akiwa amejichora tattoo mikono yote na kutoboa sikio na haitoshi akasuka na Rasta kbsa

Taarifa isiyo rasmi inasemekana atakuwepo hapo leader club kufanya maombi na nabii sijui clear malisaa sijajuwa Bado

Swali

Je, muonekana wa mtu Haina shida kwenye imani au dini ,kweli kuchora tatooo inakubalika wapi ktk kanisa gani

Picha ya manabii hi hapa chini.

View attachment 2836696View attachment 2836695
Ivi wanaoenda kwenye iyo mikutano kichwani zinachaji kweli au wanakuwa washalogwa
 
Wapo manabii kwenye biblia kabla hawampokea kristo huko nyuma maisha yao hayakumpendeza Mungu
Mfano musa aliua kule misri lakini baada ya kuteuliwa yeye ndio alipewa agano la amri kumi za Mungu na aliendelea kuishi maisha yakumpendeza Mungu baada ya kuitwa kwenye wokovu


Mtume paulo aliuwa watu wengi alimpompokea kristo aliishi maisha ya kumpendeza Mungu mpaka kifo chake

Je huyu nabii kwa huo muonekano wake vipi
musa aliua yule mmisri aliyekuwa anamnyanyasa ndugu yake muebrania mwenzake huko utumwani misri. Paulo alipookoka alibadilika tabia. Why huyu anaingia wokovuni na tabia za kale? Alitakiwa abadilike. Akina makassy, chidimule, yohana wanted na remmy ongala walipookoka walibadilika tabia, remmy alinyoa rasta zake. Inakuaje huyu nabii aendelee na mitindo yake inayoendana kinyume na maisha, tamaduni na desturi za kikristo?
 
Samahan kdg mkuu ila bado sijaridhika naomba unipe zile taratibu au labda niseme requirements za mtu kuteuliwa kuwa Nabii katik Ukristo ni zipi ? Au wanajiamulia wenyew ?
Au wanasomea chuoni na kupewa Unabii, mwenye anaelew na ameelewa swali langu naomba anijibu.

Coz saiz manabii wamekua wengi mnooo, wengi sana.

Tukishajua requirement za mtu kua nabii kwa mujib wa biblia nd tutajua fulani ni nabii au sio nabii wa kweli.

Nawasilisha.
kasome biblia, siku za mwisho kutatokea manabii wa uongo, ndio hawa wenye utata wanaotokea wakidanganya watu
 
Upumbavu wa baadhi ya wabongo kupenda umbea umbea na kuandika andika kila kitu ndio chanzo cha habari kutrend...

Mtu kama huyo unampa airtime kwa lipi labda la maana ambalo wqtu watafaidika?
 
Huyu ni Mkongo kabisa, Awilo Longomba ni mjomba wao. Babu yake aliwahi kupiga na bendi ya TP OK Jaz, na baba yake pia alikuwa mwanamuziki huko Kongo, bendi nimeisahau jina.
sasa ndio aje kwenye nchi ya werevu wanaojua kupambanua mambo ya kiroho na kujua nani ni nabii wa kweli na nani ni nabii wa uongo? Angebaki tu huko kwao kongo huku hatutamuelewa kama ni nabii wa Mungu, sanasana tutamuona ni wakala wa shetani
 
Hivi huyu nabii hasomi mitandaoni ajibu hoja, mbona kuna wenyeji wake wanashindwa nini kupata kipindi kwenye tv na redio aseme uhalali wa kuonekana vile? Sie wengine tuna mashaka nae tunamuona ni muhuni tu, media zipo azitumie kututoa mashakani ndio tuamini huduma yake ya unabii hata kama anaonekana vile
 
sasa ndio aje kwenye nchi ya werevu wanaojua kupambanua mambo ya kiroho na kujua nani ni nabii wa kweli na nani ni nabii wa uongo? Angebaki tu huko kwao kongo huku hatutamuelewa kama ni nabii wa Mungu, sanasana tutamuona ni wakala wa shetani
Unaiongelea nchi gani mkuu? hii Tanzania au?. Hii ni mojawapo ya nchi iliyojaa mazuzu, wepesi kudanganywa na ni rahisi kuvuna utajiri bila jasho lolote. Nchi watu wake wanasubiri miujiza kupata kitu ambacho walipaswa kufanya kazi kwa bidii kukipata.

Yaani mtu anatoa 200K kwa nabii ili mtoto wake aombewe kufaulu mtihani wa kidato cha 2 au 4. Watu wananunua maji na mafuta ya mizeituni kwa zaidi ya mara 5 ya bei, eti kwa kuwa tu yameombewa na anayejiita mtume/nabii.

Tena mtu tumemuona hapa Mbeya kitambo na hakuna mahali ametuthibishia ni lini aliingia mkataba na Mungu ili awe nabii. Mtu janja janja tangu kitambo, sasa anaogelea kwenye utajiri kwa upumbavu wa watu.
 
Hivi huyu nabii hasomi mitandaoni ajibu hoja, mbona kuna wenyeji wake wanashindwa nini kupata kipindi kwenye tv na redio aseme uhalali wa kuonekana vile? Sie wengine tuna mashaka nae tunamuona ni muhuni tu, media zipo azitumie kututoa mashakani ndio tuamini huduma yake ya unabii hata kama anaonekana vile
Atatumia kitabu gani kuhalalisha ule ushetani wa kuhalalisha mwanaume kuvaa kipini puani?
Ukisoma stori yake hata Biblia hajamaliza kusoma hata kitabu kimoja.
Anakuambia tu kuwa ameitwa na Yesu aje ahubiri
 
Tuliambiwa tutawatambua kwa matendo, ukiona matendo yenye kutia shaka kaambali sana na uyo mgaigai
 
Unaiongelea nchi gani mkuu? hii Tanzania au?. Hii ni mojawapo ya nchi iliyojaa mazuzu, wepesi kudanganywa na ni rahisi kuvuna utajiri bila jasho lolote. Nchi watu wake wanasubiri miujiza kupata kitu ambacho walipaswa kufanya kazi kwa bidii kukipata.

Yaani mtu anatoa 200K kwa nabii ili mtoto wake aombewe kufaulu mtihani wa kidato cha 2 au 4. Watu wananunua maji na mafuta ya mizeituni kwa zaidi ya mara 5 ya bei, eti kwa kuwa tu yameombewa na anayejiita mtume/nabii.

Tena mtu tumemuona hapa Mbeya kitambo na hakuna mahali ametuthibishia ni lini aliingia mkataba na Mungu ili awe nabii. Mtu janja janja tangu kitambo, sasa anaogelea kwenye utajiri kwa upumbavu wa watu.
Kumuona nabii bongo ni zaidi ya laki 2.
Huruma sana
 
Kuna kizazi Cha walokole wa kuanzia miaka ya 2000 kupanda wabishi na wajuaji wao hata ushoga wanakubali na kulazimisha wengine. Na vimaswali vyao imeandikwa wapi kwenye Biblia. Na hili kizazi Cha wachora tattoo miaka ishirini ijayo kitakiwa ndio kimeliua kanisa. Nawapenda Waislamu waliyoweka discipline kwenye misikiti yao, sio sisi shoga anaitwa Nabii.
Unaposema MLOKOLE maana yake mshika dini kupitiliza yaani fanatic.

Hawa wasasa ni kizazi cha nyoka kwa jina la mitume na manabii.

Ukweli mchungu...hatuna mitume Mijini...wote ni fake including Mwamposa (ni wapigaji)

Pili hakunaga nabii yeye ni kutabiri magari na mafanikio.

Nabii ndio huduma chungu kuliko zote katika imani ya kikristo.

Haikuwa jambo rahisi kwa Eliya kwenda kumchana ukweli Mfalme mwovu Ahabu.

Hawa wa sasa ni wezi, majambazi wakubwa.

1. Nabii unauza chumvi?
2. Nabii unauza sabuni?
3. Nabii unauza mafuta?
Umeona wapi nguvu ya Mungu inauzwa?

Muujiza wa Mungu huuzwa?
Iliandikwa wapi?
 
Ilimuona akifanya ushoga,hizo tattoo alizichora akiwa tayari ameokoka au kabla hajaokoka? na je tattoo ikishachorwa huwa inafurika? Na kama wewe humkubali unaonaje ukikaa kimya uwaache wanapokubali waendelee kusikiliza mahubiri yake?

Kaa kimya mwenyewe na Punguza ujuaji. Mahubiri hata nabii Tito anahubiri ijekuwanhiyo. Hizo tattoo kachora akiwa tayari ni nabii. Tena alimuiga huyo Prophet Java. Acheni kudanganya watu kuwa alichora kabla hajaokoka. Halafu huna uwezo wa kuniambia nikae kimya.
 
Unaposema MLOKOLE maana yake mshika dini kupitiliza yaani fanatic.

Hawa wasasa ni kizazi cha nyoka kwa jina la mitume na manabii.

Ukweli mchungu...hatuna mitume Mijini...wote ni fake including Mwamposa (ni wapigaji)

Pili hakunaga nabii yeye ni kutabiri magari na mafanikio.

Nabii ndio huduma chungu kuliko zote katika imani ya kikristo.

Haikuwa jambo rahisi kwa Eliya kwenda kumchana ukweli Mfalme mwovu Ahabu.

Hawa wa sasa ni wezi, majambazi wakubwa.

1. Nabii unauza chumvi?
2. Nabii unauza sabuni?
3. Nabii unauza mafuta?
Umeona wapi nguvu ya Mungu inauzwa?

Muujiza wa Mungu huuzwa?
Iliandikwa wapi?

Umeongea ukweli mtupu.
 
Cha kushangaza hawa manabii wanaishi maisha ya kifahari, wana ukwasi wa kushangaza, wana ulinzi kama wa rais, wana mirengo ya kisiasa. Hawajawahi kuitabiria nchi nini kitatokea wananchi wachukue hatua. Hawawezi kuikemea serikali ikiboronga ndio kwanza wanaenda kula nao kuku na bata za kutosha. Manabii wengine wana magari ya gharama kubwa na wanamiliki usafiri wa anga. Cha ajabu zaidi wanaitaka mpaka senti ya mwisho ya masikini
 
Back
Top Bottom