TWIZAMALLYA
JF-Expert Member
- Oct 1, 2011
- 397
- 81
Nimesikiliza Bunge jana na kumsikiliza mwigulu akijaribu kuchallenge hotuba ya kambi ya upinzani hasa pale aliposema inawadhalilisha waalimu na wahadhiri kwa kusema waalimu wanafanya biashara wakati wa kazi na wahadhiri wanafundisha vyuo zaidi ya vile walivyoajiriwa.Mwigulu anauita huu ni udhalilishaji kwa watu hawa,hapa anatafuta kupata umaarufu kwa watu hawa.Hapa mimi naona anajisumbua tu kwani ni kweli kabisa waalimu wanafanya biashara na ni kweli kabisa wahadhiri wanafundisha vyuo zaidi ya walivyoajiriwa navyo.Hata kama chadema hawakutumia neno baadhi ya waalimu na wahadhiri ndio wanafanya hivyo vitu hii haiwezi ikachukuliwa kama matusi kwa waalimu. Kwani Chadema kwa hoja zao hizo walikuwa na maana ya kutetea maslahi ya waalimu na si kingine,sasa Mwigulu anajaribua kupindisha maana ili waalimu waje juu?,huyu jamaa anatakiwa arudi darasa la kwanza na sitoi kauli yangu.Haya ni matatizo ya kulelewa na watu baki kwani jina lake MWIGULU NCHEMBA ni jina la kisukuma kabisa ambalo mtu wa kabila jingine hawezi akalitumia hivi hivi tu bila sababu ya msingi.Huwezi kuta jaluo kwa mfano anaitwa MASAWE.kwa wasukuma hasa wale wa igunga na Nzega watakubaliana na mimi kuwa WANYIRAMBA wengi kwa sababu ya hali ngumu huwa wanahama kwao n a kwenda usukumani kutafuta maisha.Wakifika huko wanaomba hifadhi kwa ma-TAICOON wa kisukuma ambapo hupewa kazi za kuchunga ng'ombe na kulima.Wasukuma kwa sababu ya utani wao huwa wanawabadilisha majina yao kwa kuwachukulia kama watoto wao hivyo Sir name inaanza kubadilishwa haraka na kutambuliwa ya yule bosi wake.Huyo kijana akifikia muda wa kuoa atalipiwa mahari na bosi wake.Akija kupata mtoto ni huyo baba wa kufikia ndio ana mamlaka ya kutoa jina kwa mtoto aliyezaliwa.Kwa hiyo inawezekana tu baba wa jamaa alienda usukaumani kutafuta maisha akapewa jina la NCHEMBA na wasukuma baadaye alizaa mtoto akamuita MWIGULU.