Huyu mwanamke simuelewi! Anajifanya anajua kila kitu

BigBaba

JF-Expert Member
Feb 7, 2017
1,909
9,038
Nina mpenzi wangu tumeahidiana tutaoana tumeshafanya taratibu mbalimbali ili kufikia malengo.

Mwaka 2015 alichaguliwa kujiunga na chuo kikuu kimoja hapa nchini process zetu za ndoa nikasitisha kwanza mana kule chuo nikawa nategemewa pia kwa kila kitu japo anakimkopo kidogo, kiukweli kimuonekano wa macho yangu anaonekana ananipenda sana ila tatizo moja tu ambalo huwa simuelewi, yani tukiwa tunapanga mambo yetu ya maisha anachokijua yeye au anachokiamini yeye anapenda kiwe kama kilivyo hataki ushauri wangu kabisa hata kama nipo sahihi.

Mnaweza mkawa mnapanga jambo tunaishia tu kugombana mana yeye hujiona anajua kila kitu. Nashindwa nifanyeje wakuu ili twende sawa sometimes nimekuwa nikifanya mambo kimya kimya bila kumshirikisha kwasababu ya kuogopa makelele.

Na mara nyinyi nimekuwa nikifuata ushauri wake unakuta ninaishia kufail tu katika mipango yangu. Kiufupi hashauriki.
 
tatizo hilo
mwanamke hata kama anajua vitu vingi hatakiwi awe mtoa maamuzi ya mwisho wewe kuwa na msimamo shikilia ulichoamini yeye akikushauri msikilize hata kama ameongea point mpinge mbele yake ila fanya alichosema ni mambo ya kisaikolojia tu
 
mi ntakwambia, hakufai but moyo wako utasisitiza uendelee Naye,utambadilisha mbeleni!lazma moyo wako utashinda tu!

MWANAMKE BORA NI YULE ANAYEMSIKILIZA MUMEWE NA KUFUATA MAWAZO YA MUMEWE HATA KAMA YANAFAIL!

UKIMUOA HUYO MWANAMKE UTAJUTA SIKU MOJA!
 
Wewe ukiingia kwenye ndoa ni kipi hasa unachokihitaji??
Kwa ninavoelewa ndoa ni paradiso ya hapa duniani, nikiwa na maana kuwa furaha, upendo, kuheshimiana, penzi la dhati, Maelewano n.k ni vitu vya kuzingatiwa kwa kila mmoja ili kweli iwe paradiso.
(Japo mikwaluzano haikosekani kwasababu wote ni binadamu)

Kama ni hivyo inamaana unatakiwa kupata mtu ambaye utaridhika naye si kimapenzi tu bali hata kwa hayo mengine yaani unae endana nae kitabia.

Sasa kabla hamjafunga ndoa tayari mnaanza kupishana kimaamuzi, ujue kabisa hapo unakwenda kujifunga pingu wewe mwenyewe na itakubidi ukakubali kuwa mume bwege yeye awe muamuzi wa kila kitu.

Tafuta mwingine huyo hatakufaa ila kama utakuwa tayari yeye ndo awe kichwa kwako na familia sawa oa tu.
 
Nina mpenzi wangu tumeahidiana tutaoana tumeshafanya taratibu mbalimbali ili kufikia malengo.

mwaka 2015 alichaguliwa kujiinga na chuo kikuu kimoja hapa nchini process zetu za ndoa nikasitisha kwanza mana kule chuo nikawa nategemewa pia kwa kila kitu japo anakimkopo kidogo, kiukweli kimuonekano wa macho yangu anaonekana ananipenda sana ila tatizo moja tu ambalo huwa simuelewi, Yani tukiwa tunapanga mambo yetu ya maisha anachokijua yeye au anachokiamini yeye anapenda kiwe kama kilivyo hataki ushauri wangu kabisa hata kama nipo sahihi.

mnaweza mkawa mnapanga jambo tunaishia tu kugombana mana yeye hujiona anajua kila kitu. Nashindwa nifanyeje wakuu ili twende sawa sometimes nmekuwa nikifanya mambo kimya kimya bila kumshirikisha kwasababu ya kuogopa makelele.

Na mara nyinyi nmekuwa nikifuata ushauri wake unakuta ninaishia kufail tu ktk mipango yangu. Kiufupi hashauliki.

0d6c6507f6f0e859d19304bca6824155.jpg

picha sio halisi
nimeweka kutoa lile swali letu la picha

ANajua we kilaza unatema shudu kila ukipanua mdomo.Sasa hapa picha yA mwingine anayelalamikiwa mwingine weka picha yako na yake tuone kwanza kama mnaendana
 
obama aliulizwa kwenye interview moja jambo linalowagombanisha na mkewe mara kwa mara.....akajibu alikuja kugundua kila wanapoingia kwenye malumbano baadaye anakuja kugundua mkewe alikuwa sahihi...
so kuanzia hapo malumbano hamna tena!
so mkuu tafuta namna ya kuongea naye taratibu ( hasa mnapokua kwenye mudi nzuri)
umueleweshe usahihi wa mawazo yako kuhusu jambo mnalolumbana...
 
Back
Top Bottom