Huyu mwanamke nilimpenda sana

Hziyech22

JF-Expert Member
Jun 8, 2019
13,576
18,894
Kuna demu mmoja hivi anaitwa Glory huyu demu nilimkubali ila tatizo ni moja tu nilikuwa namuogopa kumtongoza kutokana na the way alivyo na anavyojiweka anajiweka classic Sana ukimuangalia tu unaona huyu demu ni very expensive na me uwezo Sina kiivyo nilikuwa bado nasoma.

Nakumbuka siku moja nilikuwa nimechukua daladala inaelekea Bunju na me nilikuwa naenda Bagamoyo na nilipata seat naangalia vizuri nimeona yule demu amekaa kwenye seat na bahati nzuri seat aliyokaa kuna jamaa ambaye amekaa nae kama abiria mwenzake alishuka so nikaona chance kwangu kwenda kukaa nae. Basi nikaenda tukasalimiana na maongezi yakaanza nilimuuliza anaenda wapi akasema anaenda Mbezi Beach kwa baba yake mdogo akaniuliza je wewe na me nikasema naenda Mbezi pia kiukwel nilikuwa siendi Mbezi naenda Bagamoyo yaani kupenda acha tu.

So tulivyofika Mbezi tukashuka nikanunua ice cream nikamwambia hivi nikununulie akasema hapana nikamwambia si vizuri niwe nakula peke yangu ni vizuri na wewe pia kweli akakubali nikamnunulia hapo nikiwa bado sijaomba number.Nikasema hapa ndo muda sahihi wakuomba namba yake.Nikamuomba pale kwa maneno ya technique so akanipa.

Natukawa tunawasiliana sana the end of the day tukawa kwenye uhusiano huyu demu alikuwa wa tofauti sana nilitegea hela zitanitoka sana akijaga getto ambalo nilikuwa nakaa na mshikaji wangu na mara nyingi hakaagi sana anakuja na vitu na ananipikia getto tunapiga story na kila Ijumaa na Jumapili lazima anipigie simu kuniombea before sijalala.

Demu alikuwa ananipenda sana kuna wakati nilikuwa sina hela na ilikuwa muhimu sana kila niliyemuomba anikopeshe alikuwa hana so mshikaji wangu akamwambia demu wangu bila mimi kujua wakati nimekaa nikakuta kwenye simu yangu imetumwa laki moja na nusu wakati mimi nilikuwa nahitaji elfu 60 nakaa kidogo napigiwa simu na demu wangu akaniambia nimekutumia mimi nikamwambia kwanini umenitumia ndio akaniambia mshikaji wangu ndio amemwambia basi nikamwambia hela yako nitakurudishia akaniambia wala usinirudishie me nimekupa tu kwa moyo mmoja.

Yule demu alinionesha mahaba matamu Sana siwezi kusahau.Baada yakupita muda mrefu yule demu akanipa taarifa ya yeye kuondoka kwenda uingereza ambapo anakaa baba yake ambapo mama yake anakaa Tanzania. So alitakiwa aende uingereza kwa ajili ya kuendelezwa kimasomo.

So akaniaga na kunipa saa pamoja na raba kama kumbukumbu kwangu kwake kiukwel nilihuzunika lakini nilikuwa Sina jinsi.

Hiyo saa mpaka sasa ninayo Ila yule demu bado hajarudi ila kama akirudi huyu demu niliyenae sasa namtema.
 
Back
Top Bottom