Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
Habari zenu?
Kila napoangalia wanawake wengine wanapendwa na waume zao roho huwa inaniuma sana ,sio kwasababu naona wivu ila kwasababu nawaza kwanini isiwe mimi.
Nimeolewa mwaka wa kumi na moja huu sasa tuna watoto watatu .mume wangu ana kimada nje ambae amezaa nae na ndio anaemthamini zaidi yangu na wanawe.kuna wakati hawalipii watoto ada ya shule hadi wanarudishwa nyumbani, mwaka jana mtoto wetu wa mwisho ndio alizaliwa pale katika hospitali ya tmj,mikocheni.nilijifungua kwa operesheni na nilikaa hospitali siki 3 bila mume wangu kufika hospitali na nikawa nashindwa kurudi nyumbani kwasababu sikuwa na pesa ya kulipia kila akipigiwa simu hapokei,mpaka siku ya tano ndio alinifata na kunipeleka nyumbani.
Ni visa vingi na mateso mengi nimeyapata kwa huyu baba.huwa anatuacha nyumbani hata wiki nne bila pesa ya chakula inabidi niende kuomba chakula kwa majirani,akirudi nikimuuliza ananipiga sana mpaka kuna siku alinivunja taya.sijui nifanye nini,sina pa kwenda,sina pa kuwapeleka wanangu.nifanye nini?je kuna sehemu yoyote nayoweza kwenda nikapata msaada
Kila napoangalia wanawake wengine wanapendwa na waume zao roho huwa inaniuma sana ,sio kwasababu naona wivu ila kwasababu nawaza kwanini isiwe mimi.
Nimeolewa mwaka wa kumi na moja huu sasa tuna watoto watatu .mume wangu ana kimada nje ambae amezaa nae na ndio anaemthamini zaidi yangu na wanawe.kuna wakati hawalipii watoto ada ya shule hadi wanarudishwa nyumbani, mwaka jana mtoto wetu wa mwisho ndio alizaliwa pale katika hospitali ya tmj,mikocheni.nilijifungua kwa operesheni na nilikaa hospitali siki 3 bila mume wangu kufika hospitali na nikawa nashindwa kurudi nyumbani kwasababu sikuwa na pesa ya kulipia kila akipigiwa simu hapokei,mpaka siku ya tano ndio alinifata na kunipeleka nyumbani.
Ni visa vingi na mateso mengi nimeyapata kwa huyu baba.huwa anatuacha nyumbani hata wiki nne bila pesa ya chakula inabidi niende kuomba chakula kwa majirani,akirudi nikimuuliza ananipiga sana mpaka kuna siku alinivunja taya.sijui nifanye nini,sina pa kwenda,sina pa kuwapeleka wanangu.nifanye nini?je kuna sehemu yoyote nayoweza kwenda nikapata msaada