Aiseee hii I'dNdugu, unafanya jazi, ni vyema ukatafuta nyumba yenye mazingira rafiki kulingana na hitaji lako.
Sijawahi kufurahia mawasiliano na mama mtoto wangu
Discussion in 'Mahusiano, mapenzi, urafiki' started by Sigara Kali, Jul 2, 2017.
Watch Thread
Sigara Kali JF-Expert Member
#1
Jul 2, 2017
Joined:May 28, 2017
Messages:1,414
Likes Received:2,816
Trophy Points:280
Habari wakuu
Husika na mada tajwa hapo juu
ni mwaka wa 4 Sasa nipo nae ,tulikutana wakati nasoma chuo kikuu flani hapa TZ
Nakumbuka mara ya Kwanza nlikutana nae barabarani nkamwomba namba akanipa
Kama kawaida yetu wanaume atulembi nkamtia vocal binti kajaa
Tukaingia katika mahusiano maisha yakaendelea.
Siku za mwanzo za mahusiano yetu binti alikua na juhudi Sana ya kupiga cm na kuchat na mm mawasiliano yakawa mazuri ya kupendeza
Baada ya muda binti akaenda mbali na mm mawasiliano yakaendelea ,wakati flani akapata kazi mjini kwa Bashite tukawa karibu tena
Ikafika kupindi binti nikampa ujauzito kazi ikamshinda nkamwambia usijali njoo nikusaidie kulea mimba nkaishi nae kwa amani upendo na furaha
Mtoto akazaliwa baada ya miezi kadhaa mama mtoto akapata kazi yenye salary nzuri
Nkauza baadhi ya vitu nkampa hela akaenda mkoani kuanza kazi
Nligraduate degree yangu salama salmin nkasema niende kwa mama mtoto tukaishi vzr but baada ya muda mawasiliano yakawa nji shida
Mimi ndo nkageuka mpigaji cm mtumaji msg
Sometimes simu inapigwa haipokelewe
Naishi mbali nae nimejaribu kumwelekeza juu ya umuhimu wa mawasiliano mazuri baina yetu lakini Bado tatizo linaendelea
Nsipopiga cm wala kutuma text nae anakaa kimya
Na akipiga anaanza kulaumu sijapiga cm kumjulia Hali mtoto kwa maana uwepo wa Mtoto ndo niwe mtumwa
Sifurahi kabisa mtindo wa mawasiliano yetu
Imefikia hatua michepuko ndo inanipa furaha kuliko mwandani wangu
NB: Mimi sina hela wala kazi ya maana ya kuingiza kipato napiga mishe mishe tu za mjini nna kiwango kikubwa cha elimu Ila Bado Mambo hayajanikalia poa naendelea kupambana nijenge heshima
Mama mtoto wangu ni mwajiriwa kanizidi kipato
Nimeamini wanawake ndo chanzo cha kuvurugika kwa mahusiano na ndoa mwanamke akijua unampenda anataka akutawale,mwanamke akiona huna pesa heshima inashuka Hana muda na wewe,wanawake chonde chonde mtuheshimu na kutujali waume zenu hata kama hatuna pesa wala kazi za maana .
Report
Like - 3 people likes + Quote Reply