Huyu houseboy simuelewi jamani

Huyu houseboy simuelewi jamani

Manselly

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2010
Posts
456
Reaction score
130
Wadau ndani ya jamii zetu kuna mambo na vijambo yani hata sielewi watu wengine wana akili kweli au matope lakini sio ishu tumeambiwa tukubali diversities coz hatulingani.

Turudi kwenye mada sasa.

Hapa kwetu kuna ka n'gombe kamoja ka maziwa na kwasababu ya ubize wa sisi watoto wa kiume imelazimu kutafta houseboy ambaye atakua anahusika na kazi ndogo ndogo pamoja na kumhudumia huyu mfugo mmoja.

Tumempata jamaa kutoka Iringa kama kawa ana kama 27 years na ana piga kazi balaa.

Kama unavyojua tena ma gateman kwenye Bongo muvi karibu wote wanakuaga kama minara flani ivi yani netwok inasearch mda wote wanakuaga kama na mawenge ivi(wengi wa hawa wafanyakaz wanaotoka vijijini wanakuaga hivo)
Jamaa tumekaa nae kama mwaka mmoja sasa anapiga kazi haswa na hajawahi kutetereka kiafya japo kazi anazofanya ni ngumu sana.

Sasa kuna rafiki ake tunaishi nae mtaa mmoja hapa akamshauri waende kupima ukimwi kweli housboy wetu akaenda kuchek wakamwambia anao tena afanye fasta kuanza dawa. Hakuamini akarudi home akamwambia maza, so maza akamshauri aende kwenye zahanati nyngne alivyoenda majibu yakawa hayo hayo tena wakamwambia aanze dawa fasta.

Jamaa karudi hom akampa ripot maza so maza akamwambia aanze dozi jamaa kakataa kasema liwalo na liwe hawez meza dawa na kijijini harudi ataendelea na kazi zake kama kawaida.

Tatizo ni kuwa kabla hajapima alikua anamtongoza housgel wa hapa hom dem akasema kwa maza maza akamshauri awe na msimamo asikubali tukajua baada ya kupima ataacha hii tabia. Juzi mdada wa kazi analalamika tena kwa maza kuwa jamaa anamtongoza, then kahamia kukatongoza ka beki tatu ka jirani na bahat mbaya wengi wanamtosa coz hana hadhi kisa mkata majani ya mifugo.

Hebu nishaurini wadau tumfanyeje huyu jamaa manake anasema kwao harudi na dawa hamezi sasa tunapata mashaka akianza kuumwa itakuaje.Ni stori ya kweli wadau.

Napata mashaka na washauri nasaha alikoenda kupima manake wameshindwa kumshawishi kutumia dawa na kumpa maadili ya kuishi na ngoma. Kwa sasa home tunaishi nae vizuri tu na anaendelea na kazi zake lakini bado tuko dilema
 
ushauri nasaha alitakiwa apewe kule hosp alikoenda kupima.hapa tunamwambiaga aende kuanza dawa anasema liwalo na liwe hamez dawa. Hebu nambieni tukimrudisha kwao kinguvu kwa kutumia police tutakua fair kweli au
 
Mrejesheni kijijini kama hataki.
Kwanza ifahamike kwamba kama Ngombe akishikwa chuhu na huyu jamaa basi na nyie mmekwenda na maji.
 
Threads nyingine zimekaa kinyanyapaa ila kwa mfumo wa kistaarabu....
 
grace aliyajaaliwa mleta uzi anaishi kwa wazazi, hboy atakulaje mkewe na watoto? turudi kwenye mada, kawapiga changa la macho ila sijui lengo lake ni nini. Hata mi nilipataga wa hukohuko akanipiga chsnga la macho hivyihivyo ila sikumuelewa alikuwa na maana gani
 
Mwambie unataka upaone kwao km tatizo litatokea ujue pakuanzia alafu akikubali kwenda nawewe ukifika huko umwambie hali halisi
 
Zanzibar Spices:
Naomba ufafanue hiyo kauli yako. Ina maana HIV watamwingia ngombe? Ama HIV wataingia kwenye maziwa? Then what? From cow/milk to human being? Hii sayansi mpya...
 
Natamani jf wote tupime tujue hali za afya zetu.
 
Tafuteni mshauri nasaha aje hapo home kwenu aonane nae, kukubaliana na tatizo ni hatua kubwa sana ya kukabiliana na tatizo afu jaribun kumwelewesha kuwa huo sio mwisho wa maisha, na kitu kikubwa ambacho wengi huwa hawakijui ni kwamba ukianza kutumia dawa za ARV kwa usahihi unakuwa huna uwezo wa kumwambukiza mtu mwingine ndo mana HIV activists wanashaur watu wapime kujua afya zao na kama wameathirika basi CD4 count zikifika level flan wanatakiwa waanze dozi manake in the longrun tunaweza tukatokomeza hili gonjwa kwa style hiyo, mkuu yafanyie kazi haya nloshauri, ukishindwa rudi tena nikupe njia mbadala.
 
Mrejesheni kijijini kama hataki.
Kwanza ifahamike kwamba kama Ngombe akishikwa chuhu na huyu jamaa basi na nyie mmekwenda na maji.

sayans ya wapi hii?kwamba akishika chuchu na sie kwisha sio kweli. Hana madonda wala hajaanza kukohoa ukimuona huwez amini
 
Threads nyingine zimekaa kinyanyapaa ila kwa mfumo wa kistaarabu....

kiukweli hatujui cha kufanya kaka manake sisi tumemleta kwaajili ya kazi za nguvu mf kukata majani sa inafikia kipnd tunahofu kama zitamfanya achoke mapema na pia kama ataanza dawa lazma itamlazm kupata tym ya kupumzka so lengo letu la kuwa nae ni kama linakufa vile
 
duh ishu ni kuwa hata akija mshauri akafanya kazi yake je haya makazi anayofanya ya kwenda kukata majani porini ni sahihi kwake?hapo ndo tunapopata mawazo ya kumrudisha kwao unles tutafte hboy mwngne af ye abaki tu kujisikilizia afya kitu ambacho ni kama hakiwezekani flani ivi
 
Back
Top Bottom