Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,511
- 40,592
Nimetembelewa na mdada mrembo (pisi kali kweli), kwa sasa anakaribia wiki kukaa hapa kwangu. Anategemea by jumapili ijayo aweze kuondoka.
Tangu amefika kwangu, hela imekuwa haitulii. Kila siku hela inatoka tu, na mbaya zaidi anaujauzito wangu unaokaribia mwezi.
Leo atakuambia, naomba hela ya kusafisha kucha, mara hela ya kunyoosha wigi, mara nipe hela kidogo nitume nyumbani, mara hela ya mafuta ya kung'arisha ngozi yanagharimu elfu 60, mara nipe hela nikanunue chakula, na akishanunua hicho chakula hali; mpaka nyumba imekuwa na mabaki ya vyakula ambavyo havijatumika.
Mbaya zaidi, majuzi aliniomba twende 'club' kwa sababu ni mtu anayependa sana mziki; kwa upande wangu nikawa sijisikii vizuri, nikamwambia siwezi kwenda. Akanilazimisha, ikabidi nimruhusu yeye mwenyewe aende.
Alipoenda huko kwenye starehe akajisahau kurudi nyumbani; nikawa nampigia simu mpaka saa saba usiku hajarudi; kwa hasira, nikachukua nguo zake nikaanza kuzichana chana, kwa kuhisi labda yuko na mtu mwingine.
Asubuhi, akarudi huku anamajeraha mkononi; kwa sababu alipata ajali ya boda boda usiku wakati akirudi nyumbani. Wasamaria wema, wakambeba na kumpeleka hospitali kwa sababu alikuwa amezimia.
Baada ya kunipa hayo maelezo; ilibidi niende hospitali pamoja na kulipa bill. Lakini roho ikawa inaniuma, kwa kusababisha uharibifu kwenye nguo zake.
Ikabidi niingie gharama ya kumnunulia mavazi upya; hapa natamani hata leo aondoke, kutokana na hasara anazonipa.
Tangu amefika kwangu, hela imekuwa haitulii. Kila siku hela inatoka tu, na mbaya zaidi anaujauzito wangu unaokaribia mwezi.
Leo atakuambia, naomba hela ya kusafisha kucha, mara hela ya kunyoosha wigi, mara nipe hela kidogo nitume nyumbani, mara hela ya mafuta ya kung'arisha ngozi yanagharimu elfu 60, mara nipe hela nikanunue chakula, na akishanunua hicho chakula hali; mpaka nyumba imekuwa na mabaki ya vyakula ambavyo havijatumika.
Mbaya zaidi, majuzi aliniomba twende 'club' kwa sababu ni mtu anayependa sana mziki; kwa upande wangu nikawa sijisikii vizuri, nikamwambia siwezi kwenda. Akanilazimisha, ikabidi nimruhusu yeye mwenyewe aende.
Alipoenda huko kwenye starehe akajisahau kurudi nyumbani; nikawa nampigia simu mpaka saa saba usiku hajarudi; kwa hasira, nikachukua nguo zake nikaanza kuzichana chana, kwa kuhisi labda yuko na mtu mwingine.
Asubuhi, akarudi huku anamajeraha mkononi; kwa sababu alipata ajali ya boda boda usiku wakati akirudi nyumbani. Wasamaria wema, wakambeba na kumpeleka hospitali kwa sababu alikuwa amezimia.
Baada ya kunipa hayo maelezo; ilibidi niende hospitali pamoja na kulipa bill. Lakini roho ikawa inaniuma, kwa kusababisha uharibifu kwenye nguo zake.
Ikabidi niingie gharama ya kumnunulia mavazi upya; hapa natamani hata leo aondoke, kutokana na hasara anazonipa.