Anakupenda mno mkuu, anakuhusudu haswaa! Nawe mpende zaidi ya hapo. Mpe support yako sana katika kazi yake ngumu na yenye changamoto nyingi.
Hebu pia jaribu kuongelea namna mnavyoweza kubadili kazi, mpate hata mtaji na kufanya ujasiriamali. Hii yote itakuwezesha kulala kwa wakati na kuamka ukiwa hujachoka sana. Mjali sana Mtoto wake na mtunze vema. Kumbuka mkifanikiwa kuzaa atamtunza pia mwanao. Kuna mdau hapo kagusia suala la kupima afya zenu. Hili la muhimu sana. Ili sasa kama mmepata maambukizi (sio lazima awe yeye kakuambukiza) mjue namna ya kuishi kwa matumaini.
Hongera sana mkuu kwa namna ulivyojitoa, wapo jamaa wengi tu ambao walienda bar kama kuopoa watu wa kupooza tu lakini hadi sasa wanaishi vizuri kabisa kwa utulivu.