Huyo ni Chaguo Lako

Huyo ni Chaguo Lako

Freeland

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2012
Posts
14,481
Reaction score
10,233
Kwa wanandoa mkipata huu wimbo sikilizeni...Mimi hua unanigusa sana nikihudhuriaga harusi pale watu wanapojifunga na ma sweet heart wao.

Download hapo chini;


View attachment 166829


Huyooo ni chaguo lako
Umeomba miaka mingi
Umetafuta kila mahali
Leo umepata wako
Ambae ni chaguo lako

Alizaliwa kwa ajili yako
Ameumbwa kwa ajili yako
Huyo ni chaguo lako*3

Huyo ni chaguo lako
Hata kama mbeba zege
Hata kama aendesha guta
Hata kama ni kilema
Hata kama ni kipofu
Huyo ni chaguo lako

Hata kama atembeza mboga
Huyo ni chaguo lako
Nyumbani mwenu iwe amani
Isiwe uwanja wa mapambano
Kila mara mbembelezane
Kila mara muombeane
Huyo ni Chaguo lako

Neno la Mungu linasema
Mwanamke atamlinda mume wake kwa maombi
Na wewe tembea na mumeo
Ukimlinda kwa maombi
Kila siku muombee
Kila siku um bariki
Nyumba yenu iwe baraka
Huyoooo chaguo lako*4

Huyo ni chaguo lako
Msisikie ya walimwengu
Wekeni pamba masikioni
Ya walimwengu yatawachanganya
Ya walimwengu yatawachafua
Mwiteni Mungu awatawale
 
Mkuu sio kila mwenye mke au mume ni chaguo lake,wengine ni mambo tu yalitokea ndio wakaishia kuwa mke na mume
 
  • Thanks
Reactions: ram
Hata mm naupenda sana nmewahi kucheza show yake juz kati kwenye weding mm pananinoga hapo pa "umeomba miaka mingi,umetafuta kila mahali..leo umepata wako.ambae ni chaguo lako..huyo ni chaguo lake"
 

kuna vitu haviexist anymore hapa duniani ndio maana hata Oxford kila baada ya muda fulani wanatoa new version.

na hata klolokwini haitibu tena marelia, hata wadosi na mambo ya kuimbiana masong haina hiyo.
 
Last edited by a moderator:
..hamna kitu kama hicho!!..
chaguo kwa maana kwamba, baada ya kuchakachua vya kutosha sasa ameona atulie na wewe..!!

..atakuwaje chaguo laki wakati jana alikuwa "anapewa barka" na "kuagwa"..

..i don't believe in this "chaguo" shit!!
 
Hata mm naupenda sana nmewahi kucheza show yake juz kati kwenye weding mm pananinoga hapo pa "umeomba miaka mingi,umetafuta kila mahali..leo umepata wako.ambae ni chaguo lako..huyo ni chaguo lake"

Maneno ya wimbo huu ni mazito mkuu...naamini wahusika hua yanawaingia hadi moyoni ndani kabisaaaaaaaaa
 

Haipaswi kuwa hivyo MankaM ukimwomba Mungu akupatie chaguo lako...hakika hatakuangusha....Unachotakiwa tu ni kuwa mwaminifu katika kuomba kwako...Utampata tu ambae ni chaguo lako na ni saizi yako...aliyezaliwa kwa ajili yako...aliyeumbwa kwa ajili yako.....Usipomwomba Mungu ni kweli huu utabaki kuwa wimbo tu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom