Huwezi kuwa tajiri kwenye nchi masikini

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,891
HUWEZI KUWA TAJIRI KWENYE NCHI MASIKINI

Na, Robert Heriel

Nianze kwa kuwaomba radhi wale wote mnaofuatilia makala zangu kutokana na kukaa kimya kwa muda kidogo, mpaka kufikia watu wengi kunipigia simu na kuniuliza kulikoni mbona sitoi makala. Wengine wamekuja ofisini kwangu kunisabahi, wote nawashukuru sana. Nilikuwa kimya kidogo, kuna mambo ya kitaifa nilikuwa nafuatilia. Sasa nimerudi, nimeona nianze na hili la Mhe, Kigwangala ambaye ni Waziri wa Utalii hapa nchini.

Mhe. Kigwangala amejaribu kushauri vijana wa taifa hili wafute fikara na mtazamo wa kuajiriwa badala yake wajiajiri wao wenyewe. Ni wazo zuri mno lakini sio halisi kwa jamii yetu katika zama hizi. Hakuna asiyependa kujiajiri. Watu wengi hupenda kujisimamia kwa kila kitu ikiwemo masuala ya kazi. Lakini jambo hilo haliwezekani.

Moja ya falsafa zangu katika masuala ya kiuchumi ni kuwa; Mtu hawezi kuwa tajiri katika nchi masikini hata siku moja. Iwe ni umasikini wa kiuchumi, kifikra au umasikini wa aina yoyote ule. Hata katika muktadha wa kifikra, mtu hawezi kuwa na akili katika jamii za watu wajinga. Siku zote jamii jinga huzalisha watu wajinga, na kama atatokea mwenye kuonekana anaakili basi hizo ni akili kwa waliowajinga ambazo sio akili zenyewe bali ujinga uliorembwa.

Kuwaambia watu watafute utajiri kwenye jamii zao, ikiwa jamii hizo ni masikini, huko ni kuruhusu dhuluma na unyonyaji. Huko ni kuruhusu watu hao wanyonyana na kudhulumiana. Na yule mwenye nguvu na ujanja kidogo basi huyo ndio ataibuka tajiri kwa masikini wenzake.

Hakuna tajiri katika nchi au jamii masikini, bali kuna wanyonyaji na wanaodhulumu wengine na kujilimbikizia mali nyingi mno. Matajiri wote waliopo katika jamii zetu ambazo ni masikini, wote ni wanyonyaji, wezi na watu wenye dhuluma kwa masikini wenzao.

Wengine ni wasaliti, na matapeli wanaonyang'anya mali za wenzao kwa nguvu zote.

Mara kadhaa nimekuwa nikiongea na baadhi ya viongozi wa nchi hii, nikiwasisitiza kuhusu namna ya kuinua nchi hii lakini bado wamekuwa wagumu kunielewa. Sijajua ugumu wao upo kwa manufaa yao au ni kweli hawanielewi. Lakini bado ninatumaini ipo siku watanielewa.

Nchi yetu ni masikini kwa sababu inaundwa na jamii masikini. Serikali inapokuwa masikini ni wazi haiwezi kuunda taifa tajiri kwa kutegemea wananchi masikini, hilo katu haliwezekani, lazima likandamize na kunyonya wananchi wake Ili walau liweze kujiendesha.

Sishangai kwa nini watu wanalalamika mishahara ni midogo isiyotosha kitu. Huko serikalini watumishi wengi wa umma wanalia kwa ufinyu wa malipo. Waalimu wanalia na kufia katika umasikini usioelezeka, Mapolisi nao halikadhalika, hata hao wauguzi na matabibu kutwa kucha kulalamika. Mishahara ni midogo haiendani na kazi zao na hali ngumu ya maisha.

Wakandarasi na wahandisi kutwa kusubiri pesa zao. Serikali haina uwezo wa kuwalipa mishahara mikubwa kutokana na umasikini wake.

Nchi ni masikini kamwe haiwezi toa serikali yenye kufanya watu wawe matajiri bila kuruhusu watu kunyonyana na kudhulumiana.

Sishangai kuona wanasiasa wakilipana mapesa mengi, posho zisizoisha, wabunge na mawaziri hutembelea matako na magari ya bei ghali ambayo mafuta yake kwa mwezi ni mishahara ya wafanyakazi wengine.

Kwa bahati nzuri nimezunguka kidogo katika nchi hii. Viwandani nimejionea vijana wakisulubika kwa kazi zaidi ya masaa 12, tena kazi ya shifti za mchana na usiku. Imenilazimu nitaje mshahara japo sikutaka kufanya hivyo kutokana na uchungu wa dhuluma na unyonyaji wa wazi kabisa. Mtu analipwa laki na ishirini kwa mwezi ati huyo siku moja anampango wa kuwa tajiri thubutu yake.

Matajiri wote kwenye nchi masikini huko viwandani huwalipa wafanyakazi wake mishahara ya aibu, mishahara ya kitumwa, hao ndio huitwa matajiri ambao kimsingi sio matajiri isipokuwa jina sahihi ni wanyonyaji au wenye dhuluma.

Sekta ya sanaa katika fani ya uigizaji na muziki napo unyonyaji ndani nje. Wasanii wengi wamebaki kuwa wacheza sinema za kitoto kama wehu. Wamevurugwa na kuchanganyikiwa kutokana na malipo kidunchu wayapatayo. Kazi wanayoifanya ni kubwa, pesa wanayozalisha ni ndefu lakini wao hulipwa pesa ya kitumwa. Wengine imefikia hatua wanajiingiza katika dili chafu na hatari kwa usalama wao na usalama wa jamii, wapo waliojiingiza kwenye madawa ya kulevya kama vichaa. Ati wanaondoa stress za maisha, sonono na ufukara uliosababishwa na dhuluma walizofanyiwa.

Wengine ni makahaba wanaodanga kutwa kucha. Mpaka imefikia kuonyesha nyuchi zao ambazo ni aibu kwao na kwa kizazi chao. Huo wote ni umasikini. Mtu tajiri hawezi kukaa uchi au kujiuza na kujidhalilisha isipokuwa mwehu na aliyechanganyikiwa au mwenye laana.

Wafanyakazi wa ndani nao kilio, mishahara kama pesa ya matumizi ya mwanafunzi wa shule ya msingi, ati huo mabosi ndio wanauita mshahara, imefikia kipindi baadhi yao huwanyanyasa kabisa. Huwezi mlipa mtoto wa watu 50,000 hata kama anakula na kunya kwako. Huo ni unyonyaji.

Kutafuta utajiri kwenye jamii masikini ni kutafuta ugomvi na sheria za Mungu. Ni kujiingiza katika kudhulumu masikini na jamii yako mwenyewe.

Sijawahi kuona wala kusikia mtu aliyekuwa tajiri akitokea jamii masikini bila kunyonya wenzake au kuwadhuru kwa namna yoyote ile. Kama sio kuwauzia madawa ya kulevya, basi ni kuwaibia pesa zao za kodi, kama sio uganga wa kienyeji, badi ni pesa za utapeli za hawa wachungaji wahuni wa zama hizi.

Mhe. Kigwangala, kama ulikuwa hujui ni kuwa matajiri wote unaowaona, au wote wenye pesa waliopo nchi masikini basi jua hao ni wanyonyaji na wanaodhulumu wengine, ukiwemo na wewe. Huwezi kuwa na kipato cha zaidi milioni 10 kwa mwezi katika nchi kama hii bado usiitwe mnyonyaji. Watanzania wengi kipato chao kwa mwezi hakifiki laki moja wewe unapataje milioni na ushee katika nchi ya namna hiyo. Wewe lazima uwe nyonyaji.

Kuwa na ndoto ya utajiri kwenye nchi masikini ni sawa na kuwa na ndoto ya kuwa mdhulumati na nyonyaji lisilojali utu wala haki za binadamu.

Kitu pekee ambacho niliwahi kukisema siku za nyuma ni kuwa; lazima tutafute mahali pa kuufukuzia umasikini uliopo katika nchi yetu. Kama hatutaufukuza basi tutafanyana kuwa masikini sisi kwa sisi. Kama taifa, hatuna budi sisi viongozi kutafuta namna bora za kuzitawala nchi nyingine, nchi hizo ndizo tuzifanye shimo letu la taka, nchi hizo ndizo tuzigeuze makaburi ya kuzikia adui masikini, ujinga na maradhi. Nchi hizo ndizo tutafutie utajiri huko.

Serikali iunde mkakati kabambe uliosukwa kikamilifu bila ya kushukiwa na adui zetu.

Hakuna mtu makini anayeweza kujisifu kwenye nchi yetu kuwa yeye ni tajiri na anamaisha mazuri ikiwa asilimia 89 ya watanzania ni masikini. Mtu huyo labda awe mwehu, Nilimsikia Mo Dewji akikebehi mtu kukosa elfu kumi mfukoni, nikagundua anamatatizo makubwa ya kufikiri. Na ni kwa vile nchi yetu wajinga wengi, ila ingekuwa na watu wenye akili Mo asingethubutu kunyanyua mdomo wake kuongea pumba kama ile.

Wazungu wao wameamua kutuletea matatizo yao, ujinga wao wametuletea, dini zao za kipuuzi wametuletea, teknolojia yao ni nzuri lakini hawatufundishi namna ya kuitengeneza zaidi ya kuitumia nayo wametuletea, umasikini na maradhi wametuletea, sanaa na mitindo karibu yote ya nguo wametuletea, kwa nini wasiwe matajiri.

Utajiri ni kumfanya mwingine awe masikini, hiyo ni kanuni. Uhai ni kufanya mwingine afe, akili ni kumfanya mwingine awe mjinga, Uungu ni kumfanya mwingine awe kiumbe.

Sasa sisi tunatafuta utajiri humu humu, sisi kwa sisi ilhali sisi ni masikini. Lazima wengine wakione chamoto ili wengine wale bata.

Mwisho: Niombe Serikali ijadli namna bora ya kuliinua taifa hili kwa kuzitawala nchi zingine kusudi kupunguza umasikini kwa taifa letu.

Nafurahi kuona wenzetu wa Rwanda na Uganda wakihangaika huko Kongo. Kwa kweli mimi nawapongeza hata kama wenye ufinyu wa fikara wataona ninatabia ya uvamizi. Lakini ni heri tuvamie nchi zingine kuliko kuvamiana sisi kwa sisi.

Nipumzike sasa, Taikon wa Fasihi kwa sasa Nipo Morogoro.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
 
Sijawahi kuona wala kusikia mtu aliyekuwa tajiri akitokea jamii masikini bila kunyonya wenzake au kuwadhuru kwa namna yoyote ile. Kama sio kuwauzia madawa ya kulevya, basi ni kuwaibia pesa zao za kodi, kama sio uganga wa kienyeji, badi ni pesa za utapeli za hawa wachungaji wahuni wa zama hizi.
Endela kuamini hivyo kutokana kukariri vitabu vya watu. Nimeshuhudia watu wakifanikiwa kutokana na kilimo na ufugaji. Mwalimu wa shule ya msingi anaagia Toyota Dyna kutoka nje.

Watu anapiga hela za miti, hata juzi tu watu wamepiga pesa za nyanya. Jitume tu Pesa ipo wala hunyonyi watu. Nakushauri amini katika Ardhi utafanikiwa. Labda unipe kipimo cha mtu kuwa Tajiri.
 
Nchi inapokuwa masikini maana yake resources hazijatumiwa to the optimum......
Hiyo ndio nafasi pekee ya kuibua matajiri wengi, itakuwa kinyume Kama hamna sera madhubuti na endelevu
 
Kwa kweli nashindwa kuandika mengi baada ya kusoma huu uzi
Yote Tisa
Laiti ungeangalia na thamani ya hela yetu ungeelewa kwanini mfanyakazi wa ndani au wa kiwandani analipwa hela ndogo



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Nadharia yako kuna sehemu inafanya kazi na kuna sehemu hakuna lolote!
Si sahihi kusema wote wanaokuwa matajiri wanakandamiza wengine!! Mbona yapo mambo mtu anaweza kufanya na akawa tajiri bila kukandamiza wengine.. haswa ukiielewa hili "kufanya matatizo kuwa fursa" mfano watu hawana maji ukapeleka maji na ukawa unauza kwa bei stahiki unafikiri huchomoki..

Upande wa wanaozulumu hiyo sikatai Tena watu wanadidimizana utafikiri unaishi kwa bahati mbaya! Watu wanakwepa kodi ili kuongeza faida za biashara zao.. makato muda mwengine huwa mengi ni tabu! Mtu alipe kodi ya pango la biashara kwa gharama ya juu Kodi ya biashara,Kodi ya makazi yake bado kuna familia!!! Nadharia yako ipo sawa mkuu Kuna baadhi ya mazingira ktk nchi maskini ni ngumu kuibuka tajiri
 
Asilimia 100% au tuseme hata asilimia zote mtu ambaye anaweza badilisha maisha yako ni wewe mwenyewe, ni kuchagua tu kukaa na kulalamika au kuamka na kupambana,hakuna mtu atakuja kukusaidia kupambana labda uwe wa kishua lakini mwenzangu na mimi pambana ya hela yote arifu
 
Hoja fikirishi! Japo ni nadharia tu umeandika kiuhalisia unachokishauri hakitekelezeki.
 
Mkuu umeandika kwa uchungu sana, lakini elewa kwamba ni principle ya maisha kwamba fanya ufanyavo ili watu wawe na maisha mazuri lazima kuwe kuna low, middle na high class, hii ni all over the world toka miaka ya kina yesu.
Na itd very interesting kwa sababu inampa mwanadamu motivation ya ushindani.ukizembea unabaki bottom line na ukikomaa unakaa on top, uzuri pia dunia inakupa chances za kutoka kwenye matatizo.
Its always scramble game. Its a game of lucky and efforts. So nikawaida tu mkuu
Watanzania kama group la watu ni masikini lakini ukifanya analysis ya mtu mmoja mmoja utaona kuna watu wako vizuri.
Alafu pia we mwenyewe unaji contradict unavyosema kwamba huwezi kua masikini kwenye nchi tajiri alafu at the same time unasema unaweza kua tajiri kwa utapeli na unyonyaji, but it doesnt matter, pesa inatafutwa kwa njia nyingi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HUWEZI KUWA TAJIRI KWENYE NCHI MASIKINI

Na, Robert Heriel

Nianze kwa kuwaomba radhi wale wote mnaofuatilia makala zangu kutokana na kukaa kimya kwa muda kidogo, mpaka kufikia watu wengi kunipigia simu na kuniuliza kulikoni mbona sitoi makala. Wengine wamekuja ofisini kwangu kunisabahi, wote nawashukuru sana. Nilikuwa kimya kidogo, kuna mambo ya kitaifa nilikuwa nafuatilia. Sasa nimerudi, nimeona nianze na hili la Mhe, Kigwangala ambaye ni Waziri wa Utalii hapa nchini.

Mhe. Kigwangala amejaribu kushauri vijana wa taifa hili wafute fikara na mtazamo wa kuajiriwa badala yake wajiajiri wao wenyewe. Ni wazo zuri mno lakini sio halisi kwa jamii yetu katika zama hizi. Hakuna asiyependa kujiajiri. Watu wengi hupenda kujisimamia kwa kila kitu ikiwemo masuala ya kazi. Lakini jambo hilo haliwezekani.

Moja ya falsafa zangu katika masuala ya kiuchumi ni kuwa; Mtu hawezi kuwa tajiri katika nchi masikini hata siku moja. Iwe ni umasikini wa kiuchumi, kifikra au umasikini wa aina yoyote ule. Hata katika muktadha wa kifikra, mtu hawezi kuwa na akili katika jamii za watu wajinga. Siku zote jamii jinga huzalisha watu wajinga, na kama atatokea mwenye kuonekana anaakili basi hizo ni akili kwa waliowajinga ambazo sio akili zenyewe bali ujinga uliorembwa.

Kuwaambia watu watafute utajiri kwenye jamii zao, ikiwa jamii hizo ni masikini, huko ni kuruhusu dhuluma na unyonyaji. Huko ni kuruhusu watu hao wanyonyana na kudhulumiana. Na yule mwenye nguvu na ujanja kidogo basi huyo ndio ataibuka tajiri kwa masikini wenzake.

Hakuna tajiri katika nchi au jamii masikini, bali kuna wanyonyaji na wanaodhulumu wengine na kujilimbikizia mali nyingi mno. Matajiri wote waliopo katika jamii zetu ambazo ni masikini, wote ni wanyonyaji, wezi na watu wenye dhuluma kwa masikini wenzao.

Wengine ni wasaliti, na matapeli wanaonyang'anya mali za wenzao kwa nguvu zote.

Mara kadhaa nimekuwa nikiongea na baadhi ya viongozi wa nchi hii, nikiwasisitiza kuhusu namna ya kuinua nchi hii lakini bado wamekuwa wagumu kunielewa. Sijajua ugumu wao upo kwa manufaa yao au ni kweli hawanielewi. Lakini bado ninatumaini ipo siku watanielewa.

Nchi yetu ni masikini kwa sababu inaundwa na jamii masikini. Serikali inapokuwa masikini ni wazi haiwezi kuunda taifa tajiri kwa kutegemea wananchi masikini, hilo katu haliwezekani, lazima likandamize na kunyonya wananchi wake Ili walau liweze kujiendesha.

Sishangai kwa nini watu wanalalamika mishahara ni midogo isiyotosha kitu. Huko serikalini watumishi wengi wa umma wanalia kwa ufinyu wa malipo. Waalimu wanalia na kufia katika umasikini usioelezeka, Mapolisi nao halikadhalika, hata hao wauguzi na matabibu kutwa kucha kulalamika. Mishahara ni midogo haiendani na kazi zao na hali ngumu ya maisha.

Wakandarasi na wahandisi kutwa kusubiri pesa zao. Serikali haina uwezo wa kuwalipa mishahara mikubwa kutokana na umasikini wake.

Nchi ni masikini kamwe haiwezi toa serikali yenye kufanya watu wawe matajiri bila kuruhusu watu kunyonyana na kudhulumiana.

Sishangai kuona wanasiasa wakilipana mapesa mengi, posho zisizoisha, wabunge na mawaziri hutembelea matako na magari ya bei ghali ambayo mafuta yake kwa mwezi ni mishahara ya wafanyakazi wengine.

Kwa bahati nzuri nimezunguka kidogo katika nchi hii. Viwandani nimejionea vijana wakisulubika kwa kazi zaidi ya masaa 12, tena kazi ya shifti za mchana na usiku. Imenilazimu nitaje mshahara japo sikutaka kufanya hivyo kutokana na uchungu wa dhuluma na unyonyaji wa wazi kabisa. Mtu analipwa laki na ishirini kwa mwezi ati huyo siku moja anampango wa kuwa tajiri thubutu yake.

Matajiri wote kwenye nchi masikini huko viwandani huwalipa wafanyakazi wake mishahara ya aibu, mishahara ya kitumwa, hao ndio huitwa matajiri ambao kimsingi sio matajiri isipokuwa jina sahihi ni wanyonyaji au wenye dhuluma.

Sekta ya sanaa katika fani ya uigizaji na muziki napo unyonyaji ndani nje. Wasanii wengi wamebaki kuwa wacheza sinema za kitoto kama wehu. Wamevurugwa na kuchanganyikiwa kutokana na malipo kidunchu wayapatayo. Kazi wanayoifanya ni kubwa, pesa wanayozalisha ni ndefu lakini wao hulipwa pesa ya kitumwa. Wengine imefikia hatua wanajiingiza katika dili chafu na hatari kwa usalama wao na usalama wa jamii, wapo waliojiingiza kwenye madawa ya kulevya kama vichaa. Ati wanaondoa stress za maisha, sonono na ufukara uliosababishwa na dhuluma walizofanyiwa.

Wengine ni makahaba wanaodanga kutwa kucha. Mpaka imefikia kuonyesha nyuchi zao ambazo ni aibu kwao na kwa kizazi chao. Huo wote ni umasikini. Mtu tajiri hawezi kukaa uchi au kujiuza na kujidhalilisha isipokuwa mwehu na aliyechanganyikiwa au mwenye laana.

Wafanyakazi wa ndani nao kilio, mishahara kama pesa ya matumizi ya mwanafunzi wa shule ya msingi, ati huo mabosi ndio wanauita mshahara, imefikia kipindi baadhi yao huwanyanyasa kabisa. Huwezi mlipa mtoto wa watu 50,000 hata kama anakula na kunya kwako. Huo ni unyonyaji.

Kutafuta utajiri kwenye jamii masikini ni kutafuta ugomvi na sheria za Mungu. Ni kujiingiza katika kudhulumu masikini na jamii yako mwenyewe.

Sijawahi kuona wala kusikia mtu aliyekuwa tajiri akitokea jamii masikini bila kunyonya wenzake au kuwadhuru kwa namna yoyote ile. Kama sio kuwauzia madawa ya kulevya, basi ni kuwaibia pesa zao za kodi, kama sio uganga wa kienyeji, badi ni pesa za utapeli za hawa wachungaji wahuni wa zama hizi.

Mhe. Kigwangala, kama ulikuwa hujui ni kuwa matajiri wote unaowaona, au wote wenye pesa waliopo nchi masikini basi jua hao ni wanyonyaji na wanaodhulumu wengine, ukiwemo na wewe. Huwezi kuwa na kipato cha zaidi milioni 10 kwa mwezi katika nchi kama hii bado usiitwe mnyonyaji. Watanzania wengi kipato chao kwa mwezi hakifiki laki moja wewe unapataje milioni na ushee katika nchi ya namna hiyo. Wewe lazima uwe nyonyaji.

Kuwa na ndoto ya utajiri kwenye nchi masikini ni sawa na kuwa na ndoto ya kuwa mdhulumati na nyonyaji lisilojali utu wala haki za binadamu.

Kitu pekee ambacho niliwahi kukisema siku za nyuma ni kuwa; lazima tutafute mahali pa kuufukuzia umasikini uliopo katika nchi yetu. Kama hatutaufukuza basi tutafanyana kuwa masikini sisi kwa sisi. Kama taifa, hatuna budi sisi viongozi kutafuta namna bora za kuzitawala nchi nyingine, nchi hizo ndizo tuzifanye shimo letu la taka, nchi hizo ndizo tuzigeuze makaburi ya kuzikia adui masikini, ujinga na maradhi. Nchi hizo ndizo tutafutie utajiri huko.

Serikali iunde mkakati kabambe uliosukwa kikamilifu bila ya kushukiwa na adui zetu.

Hakuna mtu makini anayeweza kujisifu kwenye nchi yetu kuwa yeye ni tajiri na anamaisha mazuri ikiwa asilimia 89 ya watanzania ni masikini. Mtu huyo labda awe mwehu, Nilimsikia Mo Dewji akikebehi mtu kukosa elfu kumi mfukoni, nikagundua anamatatizo makubwa ya kufikiri. Na ni kwa vile nchi yetu wajinga wengi, ila ingekuwa na watu wenye akili Mo asingethubutu kunyanyua mdomo wake kuongea pumba kama ile.

Wazungu wao wameamua kutuletea matatizo yao, ujinga wao wametuletea, dini zao za kipuuzi wametuletea, teknolojia yao ni nzuri lakini hawatufundishi namna ya kuitengeneza zaidi ya kuitumia nayo wametuletea, umasikini na maradhi wametuletea, sanaa na mitindo karibu yote ya nguo wametuletea, kwa nini wasiwe matajiri.

Utajiri ni kumfanya mwingine awe masikini, hiyo ni kanuni. Uhai ni kufanya mwingine afe, akili ni kumfanya mwingine awe mjinga, Uungu ni kumfanya mwingine awe kiumbe.

Sasa sisi tunatafuta utajiri humu humu, sisi kwa sisi ilhali sisi ni masikini. Lazima wengine wakione chamoto ili wengine wale bata.

Mwisho: Niombe Serikali ijadli namna bora ya kuliinua taifa hili kwa kuzitawala nchi zingine kusudi kupunguza umasikini kwa taifa letu.

Nafurahi kuona wenzetu wa Rwanda na Uganda wakihangaika huko Kongo. Kwa kweli mimi nawapongeza hata kama wenye ufinyu wa fikara wataona ninatabia ya uvamizi. Lakini ni heri tuvamie nchi zingine kuliko kuvamiana sisi kwa sisi.

Nipumzike sasa, Taikon wa Fasihi kwa sasa Nipo Morogoro.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300

Mada yako imekuja kwa wakati.

Nianze pale ulipoishia kwa kukunukuu

"Niombe Serikali ijadli namna bora ya kuliinua taifa hili kwa kuzitawala nchi zingine kusudi kupunguza umasikini kwa taifa letu."

Hongera kwa uchambuzi wako murua.

Tujiulize wapi tumekosea?!?,
Je tunahitaji mabadiliko au mageuzi

Kwa muono wangu tunahitaji mageuzi ya mfumo wa demokrasia.

Mfumo wa demokrasia una njia kuu mbili za kuuendea

1. Secularism
2. Diversity

Tunahitaji mageuzi ya kimfumo kutoka usekula na Kuwa Jumuishi/Uchotara (Diverse)

Nianze kuichambua misingi ya Secularism au Usekula

Ni Taifa ambalo hufata katiba ambayo kimsingi haiamini uwepo wa Mungu
Ni Taifa ambalo hufata katiba ambayo Serikali yake haiamini Imani na wala Dini.
Ni Taifa ambalo hufata katiba ambayo haipendelei imani na dini yyt.

Hasara ya Mfumo huu

Tafiti za taasisi zinazoheshimika duniani zinaeleza kuwa asilimia 40% ya nchi zinazofata mfumo wa Sekula hupendelea imani au dini mojawapo. Many Countries Favor Specific Religions
Case study Tanzania
Hivyo tatizo tulilonalo ni uSekula nani hadhir ndio ulioshindwa kuendeleza nchi na Ulimwengu kwa ujumla.

Leo si tu mfumo wa uchumi umevurugwa na si tu ni vigumu kupata utajirikutokana na umasikini uliotamalaki lkn pia ni si rahisi kupata pesa na mahitaji yako mwengine kwa njia halali.

Sekula inalazimisha watu waache kufata mila na desturi za imani na dini hata zile zenye kheri na Bali tunalazimika kwenda kinyume na matakwa ya Mungu.

Kwa imani ya dini yangu mfumo wa Usekula ni adui wa Mungu, na kuupigia kura mfumo wa Usekula ni sawa na kushiriki kumkanusha Mungu. Kila mwenye imani anaamini Mungu kwa kanuni za maisha sawa na mahitaji ya dini yake. Iwe Ukristo, Uislam Na hata dini ya upagani.



Umezungumzia neno ujinga............
Kwa imani yangu mifumo yote ilivyo kinyume na mfumo anaotaka mungu ni ujinga (ujahiliya) na ni UKAFIRI

Quran surat Al maida 50.
Je, wao wanataka hukumu za Kijahiliya?
Na nani aliye mwema zaidi katika kuhukumu kuliko Mwenyezi Mungu kwa watu wenye yakini?

Diversy - Taifa linalofata Mfumo Jumuishi

Ni Taifa ambalo Serikali inatafa katiba ambayo imeweka sheria zinayotambua uwepo wa makundi ya watu ktk taifa wenye imani tofauti na imani hizo zinaheshimiwa na kutambuliwa bila kuweka MATABAKA

Ni Taifa ambalo Serikali yake inafata katiba ambayo ina sheria inayoamini Dini zote. Na ni Taifa ambalo Serikali inatafa katiba ambayo imeweka sheria zinazolazimisha makundi ya watu ktk taifa hilo ni lazima wajumuishwe ktk nafasi mbali mbali kama ajita, teuzi nk
Leo watz wenye asili ya Asia - hatuoni wakijumuishwa ktk teuzi zinazofanywa na wenye maamuzi, ingawa ndio wanaoshikilia biashara na uchumi wa nchi.

Faida ya Mfumo huu

Ni mfumo ambao kwa sasa ndio kimbilio kwa mataifa yanayohitaji amani, usalama na maendeleo ambapo jamii zote zinaishi bila kubaguliwa.
Case study Ethiopia https://www.tandfonline.com/doi/abs/10.1080/13597566.2012.709502




kwa imani ya dini yangu mfumo wa Diversity ni rafiki wa Mungu, na kuupigia kura mfumo wa Diversity ni sawa na kukubali kuishi kuendana na sheria na matakwa ya Mungu wako.

Muhimu kufata dini Si UDINI Bali UDINI ni kupendelea imani ya dini yako wakati wa kufanya maamuzi, iwe ktk ajira, teuzi nk.

Diversity ni kwa kushirikisha makundi yote ktk jamii pasipo kujali za imani na dini zao.

Muhimu: Tunajua ajira na teuzi zinategema Weledi - hata hivyo suala la weledi lipo kwa kila makundi husika. Leo hii ukitaka watu wenye level ya Masters ktk fani yyt nitakupatia zaidi ya 20 kutoka kijijini kwangu, sembuse tulioungana kwasababu za kiimani.

Diversity inawapa Uhuru kamili kwa jamii za kufata mila, desturi na imani ya dini zao, na kubwa zaidi ni kila jamii kuwa na utamaduni wa kuvumiliana.


Ni matarajio yangu kuwa Serikali ijayo itazingatia majihaji haya na mengine yanayohusiana na diversity state kwa maendeleo endelevu.

Tunaweza kupitia link hii inavyoelezea viongozi wa dini wanavyoelezea mahitaji yao ya kuwa na mfumo wa uchumi jumuishi

Watumishi wa Mungu waja na uchumi ''CHOTARA '' | Gazeti la Rai

Nimalizie kwa kuonyesha ni namna gani Usekula ndio tatizo linalotusumbua.

Hata hivyo kabla ya hilo ningependa niweke ufafanuzi kuwa ktk tahariri yangu hii sehemu yyt niliyotumia neno dini au Imani haina maana ya kuwa nataka kuhusisha mambo ya kiroho ktk kuongoza nchi, Bali neno dini au Imani lina maana ya;
The word religion comes from the Latin word religare, which means “to bind.” It is related to the Latin word regula, which referred to a measuring stick, and is the root of our English word rule. A religion, therefore, is not merely a set of beliefs, but a set of beliefs that bind the believer. Religion imposes a kind of rule or regulation upon the believer’s life. Kwa kfupi neno Dini Lima maana ya mfumo wa maisha ambapo MTU anaamua kuufata. Na katiba inampa Uhuru wa kufata

Madhara ya Useklula

1. Uchumi kwa imani ya kiislam kama mfumo wa maisha umeshikiliwa na nguzo NNE
1. Islamic bank - mfumo wa fedha usio na riba.
Islamic Insurance - Takaful
Islamic Social Investment - Awqaf
Compulsory Charity - Zakka

Mifumo hii inapatia changamoto lukuki ktk uanzishwaji wake.
Kama Islamic bank inavyoonekana kuwa ni kitisho kwa bank zinazofata mfumobwa riba, Bali pia mfumo wa bima (Takaful) umeonekana kuwa kitisho zaidi dhidi ya mfumo wa riba tuliouzoea. Kwa kusemekana kuwa wenye mamlaka na waumini wa Usekula hawataki kuupitisha ili uweze kutungiwa kanuni ili uweze rasmi kuanza kutumika.

Vikwazo vyote hivi ni kwa kuwa Taifa letu ni tunafata mfumo wa kibaguzi wa Usekula......
 
Back
Top Bottom