Huwajui waluguru ndio maana

Huwajui waluguru ndio maana

Mtu kakurupuka kaleta uzi humu, japo ni wa muda kidogo, anaponda kabila hili adhimu kabisa hapa Tz, et ooh wabish, mara wafupi.

Unawajua kwanza waluguru kama hili ndo kabila pekee Tz lililotoa wagombea wawili wa vyama viwili tofauti wakashindana na Nyerere kugombea urais, kipindi wakoloni wanataka kutoa uhuru

Na inadaiwa hao waluguru wawili yaani Mtemvu na Kunambi walimchemsha saana mwalimu, alikuwa anakosa hadi usingizi akiwafikiria waluguru wale

Hadi ndo chanzo mwalimu kuwa mbunge morogoro ili kuwa-counter check wapinzani wake wale.

Kwa hyo dharau muache, waluguru kitambo waliamka, kipindi ambacho hata akina nshomile, bado wanatafta ma-phd,

Na mpaka leo waluguru wako vizur, hata ukiangalia kwenye kada ya mpira wa miguu, wao ndo kama kiwanda cha wachezaji nchini

#Hebu_acha_dharau_wewee

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa kubushana na mwalimu JK ndo sio ubishi huo? Au kisa alikuwa baba wa Taifa?? Na ni obvious walikuwa wanabusha tu kama utamaduni wao ulivyo na sio upinzani wa kisomi. Waluguru wafupi wabishi sana. Yaani wao kila kiti lazma wapinge. Yaani mtu anataka kuwandoa wakoloni ili mbali huru bado pia mnambishia. Kwa kwa kwaaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom