Huwa tunakuwa wanafki kuonekana wema lakini suluhisho la kunyimwa unyumba muda mrefu na kukosa watoto ni kuongeza mke au kuvunja ndoa

Huwa tunakuwa wanafki kuonekana wema lakini suluhisho la kunyimwa unyumba muda mrefu na kukosa watoto ni kuongeza mke au kuvunja ndoa

nguvu ya buku

Senior Member
Joined
Jul 15, 2025
Posts
168
Reaction score
549
Imekuwa too much sasa, mara kwa mara naona wanaume wakilalamika kunyimwa unyumba muda mrefu, pia kumekuwa na ongezeko la ndoa nyingi zenye miaka 5+ kukosa watoto.

Kama ni mwanaume
-Ongeza mke
-Vunja ndoa oa mwengine

Kama ni mwanamke
-Omba talaka uolewe upya

Tuache kujifanya wema kwa unafki, Umevumilia miezi kukosa unyumba, kama huna matatizo ya afya mwili utakuwa na kiu kali sana ya tendo kwasababu ndivyo ulivyoumbwa na hapo ndio mwanzo wa kuchepuka, wanaume kununua dada poa na wanawake kuwa na ving'asti. mwishowe utakuja kufumaniwa na utafanywa kitu mbaya huji kusahahau maisha yako.

Kupata watoto ni majaliwa lakini kuna mpaka wake, Mmehangaika kupata mtoto mwaka wa 5 mkiwa kwenye ndoa na mnajua tatizo lipo kwa nani, asie na tatizo apewe uhuru apate watoto, awe na kizazi chake, wazazi wake waone wajukuu kabla ya kuaga dunia (kama wapo.)
 
Umenyimwa tendo muda mrefu, hamna mtoto miaka zaidi ya 10, Acheni kujifanya wema kinafki huku kwa nyuma mnachepuka au kupata watoto wa nje.

Kama ni mwanaume
-Ongeza mke
-Vunja ndoa oa mwengine
Mwanaume kuwa na mwanamke mmoja ndio inafanya ulie lie kisa unyumba.

Vilevile ukiona Mwanamke anakunyima unyumba ujue thamani yako imeshuka, au Mapenzi yameisha, au tayari Hypergamy imeingia.

Be a Man, wakati wote jitahidi uwe na options. Ili uweze ku-focus na issue zako za msingi.
 
Mwanaume kuwa na mwanamke mmoja ndio inafanya ulie lie kisa unyumba.

Vilevile ukiona Mwanamke anakunyima unyumba ujue thamani yako imeshuka, au Mapenzi yameisha, au tayari Hypergamy imeingia.

Be a Man, wakati wote jitahidi uwe na options. Ili uweze ku-focus na issue zako za msingi.
Mbona wengine tuna mke moja na mambo yanaenda vizuri tu.

Haya nayaandika kwa malalamiko mengi ambayo yamekuwa kero kila kukicha, leo hii tu kuna uzi humu mdau analalamika kunyimwa unyumba miezi minne
 
mbona wanaume mnafululiza mada za ndoa wiki hii wajameni kulikoni huko majumbani
 
Wengi aibu inawakalisha katika hayo..

Aibu yenyewe inatoka a na watu hata hawachangii maisha ya muhusika.

Muhimu wazazi wasapoti watoto wao ktk
 
mada muhimu ,ngoja nione michango ya wadau wengine
 
Back
Top Bottom