Huwa mnawashughulikiaje watoto wanaokuwa na tabia kama hii?

Leejay49

JF-Expert Member
Feb 10, 2023
12,835
39,700
Habari wanajamvi...

Nina imani humu kuna wazazi ambao walishawahi kua na watoto wenye tabia kama hizi naombeni msaada wenu wa mawazo na ushauri unisaidie na mimi.

Binafsi nina mdogo wangu aliyenifuata wa kiume, ana miaka 17...huyu mdogo wangu alikua ni mpole Sanaa, akiwa nyumbani ni mtu wa kushinda ndani mda wote ni kusoma kula na kulala, mara chache sana unaweza kumkuta anaangalia movie hata marafiki zake ni mpaka waje nyumbani kutembelea ndo apige nao story bila hivyo hatoi mguu nyumbani labda aagizwe mahali..

Shida kwamba sikuizi( yani miezi hii hapa miwili) amebadilika sana hadi tunaogopa,, amekua ni mtu wa kuondoka nyumbani bila kuaga na akiondoka asubuhi harudi nyumbani msipompigia simu anaweza asionekane kabisa hadi usiku,, sometimes tukimpigia simu anaweza akapokea halafu akajibu kwa ukali kua tusimfatilie na maisha yake, hataki kula chakula nyumbani, amekua ni mtu wa kufokafoka tu mda wote hadi mama akimuuliza kitu anajibu kwa kufoka tu sio kama alivyokua zamani.

Saizi amefikia hatua kwenda kanisani pamoja na sisi hataki anasema tumuache., alikua anaumwa hakutoa taarifa mpaka anapona na hatuelewi alikua anaumwa nini yani tumefanya tu kustukia kumwona anakunywa dawa, kuna mda alivyoondoka mama akaingia chumbani kwake kukagua akakuta dawa nyingi sana, hata hatuelewi zinatibu ugonjwa gani., baada ya mama kumuuliza alikua mkali sana na ametupigia marufuku kuingia chumbani kwake hata kama ni kufanya usafi.

Ajabu ni kwamba tukimuelezea baba tabia za huyu dogo sikuizi wala hata hatilii maanani anasema tu muacheni kama alivyowaambia mumuache...hasa tatizo ni lipo kwa mama amekua na wasiwasi sana na mabadiliko ya huyu mdogo wangu yani pressure inampanda mda wote, akijaribu hata kukaa nae chini kuongea nae dogo hataki kumskiliza yeyote zaidi ni anakua mkali ukimsogelea jirani anaweza akupige makofi...

Naombeni msaada wenu wa mawazo ili niweze kumsaidia huyu mdogo wangu maana napata shida sana kumuona mama akiwa na wasiwasi mda wote 🙏🏼
 
Sorry to say this, lakini kama wewe ni binti, mtu wa kumsaidia mdogo wako ni mwanaume kama yeye.
Sasa kama kuna male figure around, tueleze ili tuanze kutoa ushauri on what to do.

Mjumbe hauwawi.
tatizo ni kwamba baba tumemshirikisha na hafanyi lolote anasema tumuache tu kama alivyosema mwenyewe..na bad luck nyumbani hatuna mwanaume mwingne zaidi ya yeye na baba tu
 
1. Chunguzeni anapotelea wapi.
2. Rafiki zake ni kina Nani? Wanajishughulisha na nini?

Asijeanza Michezo hatari, kama
1. Wizi, udokozi na ukibaka
2. Ushoga. Hii ndio hatari zaidi.
3. Madawa ya kulevya.

Mtoto wa miaka 17 ni mtoto. Anaweza kupigwa bakora akakaa Sawa. Kama wazazi hawawezi Kwa uzee au wanaroho nyepesi apeleke polisi wapo kwaajili ya Kazi ndogondogo kama hizo.

Ila mnaweza anzia Kwa wanasaikolojia ingawaje Huko polisi pia wapo Watu wa Aina hiyo
 
1. Chunguzeni anapotelea wapi.
2. Rafiki zake ni kina Nani? Wanajishughulisha na nini?

Asijeanza Michezo hatari, kama
1. Wizi, udokozi na ukibaka
2. Ushoga. Hii ndio hatari zaidi.
3. Madawa ya kulevya.

Mtoto wa miaka 17 ni mtoto. Anaweza kupigwa bakora akakaa Sawa. Kama wazazi hawawezi Kwa uzee au wanaroho nyepesi apeleke polisi wapo kwaajili ya Kazi ndogondogo kama hizo.

Ila mnaweza anzia Kwa wanasaikolojia ingawaje Huko polisi pia wapo Watu wa Aina hiyo
Asante,, tutajaribu kuufanyia kazi ushauri wako...ila kwenye suala la marafiki tumejaribu kuongea na marafiki zake wote nao wanasema wanashangaa mabadiliko yake yanatokana na nini
 
Asante,, tutajaribu kuufanyia kazi ushauri wako...ila kwenye suala la marafiki tumejaribu kuongea na marafiki zake wote nao wanasema wanashangaa mabadiliko yake yanatokana na nini

Hao marafiki wanaishi kwao au kuna mmoja ana-ghetto?

Vijana wadogo siku hizi wamejiingiza katika michezo ya ushoga hasa mmoja akiwa na ghetto. Chunguzeni vizuri.

Mpeni shughuli ya kufanya,
 
Habari wanajamvi...
Nina imani humu kuna wazazi ambao walishawahi kua na watoto wenye tabia kama hizi naombeni msaada wenu wa mawazo na ushauri unisaidie na mimi.
msaidia huyu mdogo wangu maana napata shida sana kumuona mama akiwa na wasiwasi mda wote
Hiyo ni foolish age ,umri huo ni waujinga mwingi unakujaga na mambo mengi ya kijinga jinga ,ndio maana wazungu waliupa hilo jina. Jinsi yakuishi na huyo ndugu watakuja wataalamu wakupe somo.
 
Hiyo ni foolish age ,umri huo ni waujinga mwingi unakujaga na mambo mengi ya kijinga jinga ,ndio maana wazungu waliupa hilo jina. Jinsi yakuishi na huyo ndugu watakuja wataalamu wakupe somo.
Sawa,, Asante kwa maoni
 
Back
Top Bottom