Leejay49
JF-Expert Member
- Feb 10, 2023
- 12,835
- 39,700
Habari wanajamvi...
Nina imani humu kuna wazazi ambao walishawahi kua na watoto wenye tabia kama hizi naombeni msaada wenu wa mawazo na ushauri unisaidie na mimi.
Binafsi nina mdogo wangu aliyenifuata wa kiume, ana miaka 17...huyu mdogo wangu alikua ni mpole Sanaa, akiwa nyumbani ni mtu wa kushinda ndani mda wote ni kusoma kula na kulala, mara chache sana unaweza kumkuta anaangalia movie hata marafiki zake ni mpaka waje nyumbani kutembelea ndo apige nao story bila hivyo hatoi mguu nyumbani labda aagizwe mahali..
Shida kwamba sikuizi( yani miezi hii hapa miwili) amebadilika sana hadi tunaogopa,, amekua ni mtu wa kuondoka nyumbani bila kuaga na akiondoka asubuhi harudi nyumbani msipompigia simu anaweza asionekane kabisa hadi usiku,, sometimes tukimpigia simu anaweza akapokea halafu akajibu kwa ukali kua tusimfatilie na maisha yake, hataki kula chakula nyumbani, amekua ni mtu wa kufokafoka tu mda wote hadi mama akimuuliza kitu anajibu kwa kufoka tu sio kama alivyokua zamani.
Saizi amefikia hatua kwenda kanisani pamoja na sisi hataki anasema tumuache., alikua anaumwa hakutoa taarifa mpaka anapona na hatuelewi alikua anaumwa nini yani tumefanya tu kustukia kumwona anakunywa dawa, kuna mda alivyoondoka mama akaingia chumbani kwake kukagua akakuta dawa nyingi sana, hata hatuelewi zinatibu ugonjwa gani., baada ya mama kumuuliza alikua mkali sana na ametupigia marufuku kuingia chumbani kwake hata kama ni kufanya usafi.
Ajabu ni kwamba tukimuelezea baba tabia za huyu dogo sikuizi wala hata hatilii maanani anasema tu muacheni kama alivyowaambia mumuache...hasa tatizo ni lipo kwa mama amekua na wasiwasi sana na mabadiliko ya huyu mdogo wangu yani pressure inampanda mda wote, akijaribu hata kukaa nae chini kuongea nae dogo hataki kumskiliza yeyote zaidi ni anakua mkali ukimsogelea jirani anaweza akupige makofi...
Naombeni msaada wenu wa mawazo ili niweze kumsaidia huyu mdogo wangu maana napata shida sana kumuona mama akiwa na wasiwasi mda wote 🙏🏼
Nina imani humu kuna wazazi ambao walishawahi kua na watoto wenye tabia kama hizi naombeni msaada wenu wa mawazo na ushauri unisaidie na mimi.
Binafsi nina mdogo wangu aliyenifuata wa kiume, ana miaka 17...huyu mdogo wangu alikua ni mpole Sanaa, akiwa nyumbani ni mtu wa kushinda ndani mda wote ni kusoma kula na kulala, mara chache sana unaweza kumkuta anaangalia movie hata marafiki zake ni mpaka waje nyumbani kutembelea ndo apige nao story bila hivyo hatoi mguu nyumbani labda aagizwe mahali..
Shida kwamba sikuizi( yani miezi hii hapa miwili) amebadilika sana hadi tunaogopa,, amekua ni mtu wa kuondoka nyumbani bila kuaga na akiondoka asubuhi harudi nyumbani msipompigia simu anaweza asionekane kabisa hadi usiku,, sometimes tukimpigia simu anaweza akapokea halafu akajibu kwa ukali kua tusimfatilie na maisha yake, hataki kula chakula nyumbani, amekua ni mtu wa kufokafoka tu mda wote hadi mama akimuuliza kitu anajibu kwa kufoka tu sio kama alivyokua zamani.
Saizi amefikia hatua kwenda kanisani pamoja na sisi hataki anasema tumuache., alikua anaumwa hakutoa taarifa mpaka anapona na hatuelewi alikua anaumwa nini yani tumefanya tu kustukia kumwona anakunywa dawa, kuna mda alivyoondoka mama akaingia chumbani kwake kukagua akakuta dawa nyingi sana, hata hatuelewi zinatibu ugonjwa gani., baada ya mama kumuuliza alikua mkali sana na ametupigia marufuku kuingia chumbani kwake hata kama ni kufanya usafi.
Ajabu ni kwamba tukimuelezea baba tabia za huyu dogo sikuizi wala hata hatilii maanani anasema tu muacheni kama alivyowaambia mumuache...hasa tatizo ni lipo kwa mama amekua na wasiwasi sana na mabadiliko ya huyu mdogo wangu yani pressure inampanda mda wote, akijaribu hata kukaa nae chini kuongea nae dogo hataki kumskiliza yeyote zaidi ni anakua mkali ukimsogelea jirani anaweza akupige makofi...
Naombeni msaada wenu wa mawazo ili niweze kumsaidia huyu mdogo wangu maana napata shida sana kumuona mama akiwa na wasiwasi mda wote 🙏🏼