Huu unaweza kuwa ni ushahidi rahisi kabisa kuwa mtu anapokufa huendelea kuishi na kuona yanayoendelea duniani

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,371
Kwa muda mrefu nimekaa na kutafakari sana hiki kinachoitwa laana juu ya uzao wa mtu fulani kina maana gani hasa na ni kwanini iwe ni adhabu kwa afanyae dhambi ili hali ameshondoka duniani ila kizazi chake ndio kitateseka.

Kwa mtazamo wangu, jibu rahisi hapa ni kuwa, unapotenda uovu kwa wanadamu wenzako na Mungu akakushushia laana kwako na kwa kizazi chako, maana yake ni kuwa, hata wewe utapokufa, utaendelea kuishi na kuona mateso uliowasababishia wanao, wajukuu zako, vitukuu wako, n.k. Na hiyo kwako hiyo inakuwa ni adhabu nyingine baada ya kuondoka hapa duniani kwa maana ya kuishi ukishuhudia mateso ya kizazi chako.

Ujumbe: Wale wenye mamlaka na mnaotumia madaraka yenu kutesa, kuumiza, kuua na kunyanyasa wengine, mjue mko katika hatari ya kuja kushuhudia mateso kwa uzao wenu baada ya nyinyi kuwa mmeondoka duniani ila mkiwa hai katika ulimwengu mwingine.

Last but not least, tusiogope kufa kwani inawezekana kabisa kuna maisha mengine nje ya huu ulimwengu ila cha msingi iishi vizuri hapa duniani.
 
Hapo ulipoandika UJUMBE ndo umeeleweka zaidi kuhusu makusudio yako,fasihi ya maana kabisa.

Nami naseme kweli umeshusha nondo
 
Cha ajabu mioyo yetu inajua tukifanyacho hakimpendezi Mungu lakini bado tunaongeza juhudi huko, yaani na kanisani tunaenda, tunaonekana tuna unyenyekevu mkubwa.
 
Mimi nilifanyiwaga operation nikachomwa sindano ya nusu kaput,yaani unazimika tu huelewi chochote,kinachoendelea huku,pia ukisha chomwa na kuingizwa kufanyiwa operation hata iwe ya Massa 20 kaputi ikisha isha utahisi kama ulipelekwa SAA hiyohiyo na kurudishwa,hapa nahisi hata walikufa miaka mingi iliyopita wakifufuliwa watahisi kama walilala dakika chache zilizopita,usiogope kifo,hutohisi chochote
 
Back
Top Bottom