Freightliner
JF-Expert Member
- Aug 22, 2013
- 720
- 528
Siku moja wikiendi nilitembelewa na rafiki yangu hapa mjini Mbeya akitokea wilaya ya Mwakyembe huko tukakubaliana tukutane Kiwanja kimoja hapa mjini kinaitwa Mwailubi.
Lakini huyu rafiki alikuja na rafiki pia, tukakaa pale tukitupia moja baridi moja moto kifupi tulikuwa tunalipa kodi ya nchi. Huyu rafiki wa rafiki wangu ni mzuri sana basi nikaomba namba pale nikasepa kiutuuzima tukaanzisha mapenzi.
Kama unavyojua mapenzi lazima utagharamia na nilimgharamia hadi anavyoondoka kurudi kwa Mwakyembe. Alipokuwa kule pia ile mipigo kama kawaida hadi birthday ya mwanae ananambia kidume najitoa.
Juzi kati sasa kanambia nitumie nauli nije mjini, kidume nikatuma. Aisee alichofanya akaja mjini bila taarifa akanambia siko mjini kesho yake anasema niko mjini. Kumuuliza umekuja lini anasema ana siku kadhaa.
Nikamwambia haya basi tuonane akajibu ngoja nijiandae. Kidume najipa moyo hadi usiku unaingia kimya. Kumuuliza eti naumwa nitumie hela ya hospitali nikamwambia kesho.
Hiyo kesho ananambia karudi kwa Mwakyembe alizidiwa sana, hapa aliona atamtesa rafiki yake wa kufikia ila bado anataka nimpe hela.
Huu si utapeli huu?
Lakini huyu rafiki alikuja na rafiki pia, tukakaa pale tukitupia moja baridi moja moto kifupi tulikuwa tunalipa kodi ya nchi. Huyu rafiki wa rafiki wangu ni mzuri sana basi nikaomba namba pale nikasepa kiutuuzima tukaanzisha mapenzi.
Kama unavyojua mapenzi lazima utagharamia na nilimgharamia hadi anavyoondoka kurudi kwa Mwakyembe. Alipokuwa kule pia ile mipigo kama kawaida hadi birthday ya mwanae ananambia kidume najitoa.
Juzi kati sasa kanambia nitumie nauli nije mjini, kidume nikatuma. Aisee alichofanya akaja mjini bila taarifa akanambia siko mjini kesho yake anasema niko mjini. Kumuuliza umekuja lini anasema ana siku kadhaa.
Nikamwambia haya basi tuonane akajibu ngoja nijiandae. Kidume najipa moyo hadi usiku unaingia kimya. Kumuuliza eti naumwa nitumie hela ya hospitali nikamwambia kesho.
Hiyo kesho ananambia karudi kwa Mwakyembe alizidiwa sana, hapa aliona atamtesa rafiki yake wa kufikia ila bado anataka nimpe hela.
Huu si utapeli huu?
