Kabakabana
JF-Expert Member
- Aug 5, 2011
- 5,550
- 1,166
Jaribu kumuuliza huyo unayemfahamu kuhusu huo mzigo ili u comfirm..
Mbona kama hauleweki. Jukwaa uliloweka uzi wako unanipa tabu kutoa ushauri.
Alie tuma anasema aliulipia wapi hadi wapi? maana kama alilipia hadi Dar kweli itakua ni vigumu wenyewe kumpa mtu mngine kama sio wewe mwenyewe. Ila wanatakiwa angalau kuusafirisha hadi arusha alafu wauweke ofisini kwao hadi utakapo pata hela za kukomboa.
Huyo jamaa aliekupigia simu anafanya kazi kampuni ya usafirishaji mizigo (ambapo mzigo ulilipiwa) au ni rafiki ya mtu alie kutumia mzigo?hilo sijamuuliza but itakuwa alilipia mpaka dar lasivyo ungesafirishwa mimi nikauchukua tu huku!
Huyo jamaa aliekupigia simu anafanya kazi kampuni ya usafirishaji mizigo (ambapo mzigo ulilipiwa) au ni rafiki ya mtu alie kutumia mzigo?
Basi ni utapeli. Mwambie unampigia sim alie tuma, na akiendelea kubana mzigo uttamripoti management ya airport!
Pole dear hio ni dhuluma ilo dhahiri kabisa..... Nimependa ushauri wa Mwali.
ni kama kuna utapeli ndani yake, kama sivyo basi ni bahati mbaya. Kwani alietuma mzigo hajui kama unakaa Arusha?
kuna dalili za utapeli au kulipia mzigo mara 2, kwa uelewa wangu unapotuma mzima sharti kulipia gharama zote mpaka mzigo unapotakiwa kupokelewa. bottom line mpigie alietuma mzigo muulize kama mzigo umelipia au bado. na pia inawezekana hakuna mzigo uliotumwa, njia pekee ni kuhakiki na alietajwa kuwa amekutumia. vinginevyo hii ni Naija style...na western money....
Unajua siku hizi watu wamekua haawaminiki. Lakini huyo mtu anachotakiwa kufanya ni kukutumia hivyo anavyotaka yeye kwa condition kwamba mzigo usipokelewe kama hujalipa. Hii ndivyo inavyokua. Na agent wa kuclear mzigo huwa ni wewe ndio unamchagua sio aliyetuma mzigo. Unless hizo document zimefikia kwake ndio kuna fees ambazo unatakiwa kulipia na wanakupa invoice na malipo yanakua na receipt. Na kuanzia hapo una hiari yeye akutolee au agent unayemtaka wewe. Lakini awali ya yote lazima akupatie invoice iliyokuja na huo mzigo na umekuja kwa Airwaybill number ngapi. Kama huyo jamaa yako alikuja nao kwa mkono basi hapo ni maelewano tu. Muulize ghara ni kiasi gani kama zinazidi nauli ya kuja Arusha basi ni vizuri uje ili uhakikishe kama kweli huo mzigo ni wako na uuchukue hapo hapo dirishani. Waweza tuma pesa halafu mzigo hakuna inakuaje? Wakati mtu mwenyewe humfahamu. Kama vipi aurudishe kwa mtu aliyeutuma kuliko ku risk wakati huna uhakika nao. Au gharama ikawa kubwa kuliko kununua mzigo huo huo hapa nyumbani.