CharmingLady
JF-Expert Member
- Apr 16, 2012
- 18,257
- 12,876
habari zenyu bhana!
Hii ni story ya kweli na wala si ya kutunga.... Kwanza naomba niwape majina hawa wahusika ili twende pamoja. Kuna mkaka anaitwa Juma na mdada anaitwa Fatu na pia kuna mdada mwingine anaitwa Jamila.
Juma na Fatuma walikuwa wapenzi then wachumba kisha wakafunga ndoa wiki mbili zilizopita. Pamoja na Juma kuwa mchumba wa Fatu lakini alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Jamila.
Ilipokaribia siku ya kufunga ndoa kati ya Juma na Fatu, Juma alimgharamia Jamila kwa kila kitu kilichokuwa kinahusiana na harusi... kama mjuavyo sie akina dada kwenye sherehe tunavotupia iwe viatu, nguo na kila kitu, basi pamoja na hayo Juma alimkatia tiketi ya ndege Jamila ili Jamila ahudhurie katika harusi yake (Juma).
Bila hiyana wala mshipa wa aibu kwa Jamila, Jamila alifunga safari kwenda kwenye harusi ya Juma. Basi kufika huko Jamila ndo kwanza akawa Cameraman wa maharusi tena kimbelembele kweli. Sasa hapo najiuliza huo ni ulimbukeni, unyama au tuuiteje...
Ninamsikitikia sana Fatu make najua mahusiano kati ya jamila na Juma hayataisha hivi karibuni. jamani wadada na wakaka ya JF hili mnalionaje??????
Hii ni story ya kweli na wala si ya kutunga.... Kwanza naomba niwape majina hawa wahusika ili twende pamoja. Kuna mkaka anaitwa Juma na mdada anaitwa Fatu na pia kuna mdada mwingine anaitwa Jamila.
Juma na Fatuma walikuwa wapenzi then wachumba kisha wakafunga ndoa wiki mbili zilizopita. Pamoja na Juma kuwa mchumba wa Fatu lakini alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Jamila.
Ilipokaribia siku ya kufunga ndoa kati ya Juma na Fatu, Juma alimgharamia Jamila kwa kila kitu kilichokuwa kinahusiana na harusi... kama mjuavyo sie akina dada kwenye sherehe tunavotupia iwe viatu, nguo na kila kitu, basi pamoja na hayo Juma alimkatia tiketi ya ndege Jamila ili Jamila ahudhurie katika harusi yake (Juma).
Bila hiyana wala mshipa wa aibu kwa Jamila, Jamila alifunga safari kwenda kwenye harusi ya Juma. Basi kufika huko Jamila ndo kwanza akawa Cameraman wa maharusi tena kimbelembele kweli. Sasa hapo najiuliza huo ni ulimbukeni, unyama au tuuiteje...
Ninamsikitikia sana Fatu make najua mahusiano kati ya jamila na Juma hayataisha hivi karibuni. jamani wadada na wakaka ya JF hili mnalionaje??????