Oppo A17k
JF-Expert Member
- Apr 1, 2020
- 993
- 3,007
Habari wana jf poleni na majukumu ya ujenzi wa taifa. Leo katika pitapita zangu nimekutana na hivi vitu nikaona bora na nyie niwashirikishe maana vizuri kula na mwenzako
1. Mwanamke anapokasirika, zaidi ya nusu ya mambo anayoongea anakuwa hajamaanisha.
2. Wakati mgumu kabisa kwa mwanamke ni pale anapokuwa mbali na mwanaume anayempenda kwa dhati au anapogundua kuwa mumewe ana mahusiano na mwanamke mwingine.
3: Mwanamke sio kama "tangazo la OMO" usipomfurahisha na kumtunza... wengine wataifanya hiyo kazi badala yako.
4. Inamchukua muda mwanamke kumuamini mwanaume, na akikuamini ni ngumu kumbadilisha, lakini ukijichanganya, sahau kabisa kama atakuamini tena.
5. Mwanamke ni shule ambayo huwezi kuhitimu.
6. Cheti unachopewa unapomuoa mwanamke sio "leseni ya udereva" bali ni kama "kibali cha mwanafunzi".
7. Anaweza kuwa mchungu sasa hivi, lakini baadaye akawa malaika mtamu.. Itategemea namna utakavyoishi naye.
8. Ni ngumu mwanamke kusahau vitu, anakumbuka zaidi yale yanayomuumiza zaidi, hivyo epuka kumuumiza.
9. Mwanamke anaweza kuwa msiri sana... muda mwingi anapokwazwa na jambo anaenda kwa mtu wake wa karibu, analia.
10. Wanawake wote wanapenda kuombwa. Mara nyingi wanaume wanalisahau hili.
11. Wanawake wote wana tabia ya kipekee kama chumvi, unaweza usitambue uwepo wake lakini akikosekana vitu vyote vinakosa ladha.
12. Akikupenda kwa dhati anaweza kufanya chochote unachotaka afanye madamu kinakufurahisha, hivyo usimlazimishe kukupenda.
13. Mkeo anaekupenda kwa dhati, hata kukuomba pesa ataona aibu, na hasa kama anakupenda hawezi kuvumilia matumizi yako mabovu ya pesa... hayo ni miongoni mwa mambo yanayowafanya wanawake kuwa viumbe maalum kabisa..

.
1. Mwanamke anapokasirika, zaidi ya nusu ya mambo anayoongea anakuwa hajamaanisha.
2. Wakati mgumu kabisa kwa mwanamke ni pale anapokuwa mbali na mwanaume anayempenda kwa dhati au anapogundua kuwa mumewe ana mahusiano na mwanamke mwingine.
3: Mwanamke sio kama "tangazo la OMO" usipomfurahisha na kumtunza... wengine wataifanya hiyo kazi badala yako.
4. Inamchukua muda mwanamke kumuamini mwanaume, na akikuamini ni ngumu kumbadilisha, lakini ukijichanganya, sahau kabisa kama atakuamini tena.
5. Mwanamke ni shule ambayo huwezi kuhitimu.
6. Cheti unachopewa unapomuoa mwanamke sio "leseni ya udereva" bali ni kama "kibali cha mwanafunzi".
7. Anaweza kuwa mchungu sasa hivi, lakini baadaye akawa malaika mtamu.. Itategemea namna utakavyoishi naye.
8. Ni ngumu mwanamke kusahau vitu, anakumbuka zaidi yale yanayomuumiza zaidi, hivyo epuka kumuumiza.
9. Mwanamke anaweza kuwa msiri sana... muda mwingi anapokwazwa na jambo anaenda kwa mtu wake wa karibu, analia.
10. Wanawake wote wanapenda kuombwa. Mara nyingi wanaume wanalisahau hili.
11. Wanawake wote wana tabia ya kipekee kama chumvi, unaweza usitambue uwepo wake lakini akikosekana vitu vyote vinakosa ladha.
12. Akikupenda kwa dhati anaweza kufanya chochote unachotaka afanye madamu kinakufurahisha, hivyo usimlazimishe kukupenda.
13. Mkeo anaekupenda kwa dhati, hata kukuomba pesa ataona aibu, na hasa kama anakupenda hawezi kuvumilia matumizi yako mabovu ya pesa... hayo ni miongoni mwa mambo yanayowafanya wanawake kuwa viumbe maalum kabisa..

.


