Huu ni ukweli kuhusu Wanawake

Huu ni ukweli kuhusu Wanawake

Oppo A17k

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2020
Posts
993
Reaction score
3,007
Habari wana jf poleni na majukumu ya ujenzi wa taifa. Leo katika pitapita zangu nimekutana na hivi vitu nikaona bora na nyie niwashirikishe maana vizuri kula na mwenzako

1. Mwanamke anapokasirika, zaidi ya nusu ya mambo anayoongea anakuwa hajamaanisha.

2. Wakati mgumu kabisa kwa mwanamke ni pale anapokuwa mbali na mwanaume anayempenda kwa dhati au anapogundua kuwa mumewe ana mahusiano na mwanamke mwingine.

3: Mwanamke sio kama "tangazo la OMO" usipomfurahisha na kumtunza... wengine wataifanya hiyo kazi badala yako.

4. Inamchukua muda mwanamke kumuamini mwanaume, na akikuamini ni ngumu kumbadilisha, lakini ukijichanganya, sahau kabisa kama atakuamini tena.

5. Mwanamke ni shule ambayo huwezi kuhitimu.

6. Cheti unachopewa unapomuoa mwanamke sio "leseni ya udereva" bali ni kama "kibali cha mwanafunzi".

7. Anaweza kuwa mchungu sasa hivi, lakini baadaye akawa malaika mtamu.. Itategemea namna utakavyoishi naye.

8. Ni ngumu mwanamke kusahau vitu, anakumbuka zaidi yale yanayomuumiza zaidi, hivyo epuka kumuumiza.

9. Mwanamke anaweza kuwa msiri sana... muda mwingi anapokwazwa na jambo anaenda kwa mtu wake wa karibu, analia.

10. Wanawake wote wanapenda kuombwa. Mara nyingi wanaume wanalisahau hili.

11. Wanawake wote wana tabia ya kipekee kama chumvi, unaweza usitambue uwepo wake lakini akikosekana vitu vyote vinakosa ladha.

12. Akikupenda kwa dhati anaweza kufanya chochote unachotaka afanye madamu kinakufurahisha, hivyo usimlazimishe kukupenda.

13. Mkeo anaekupenda kwa dhati, hata kukuomba pesa ataona aibu, na hasa kama anakupenda hawezi kuvumilia matumizi yako mabovu ya pesa... hayo ni miongoni mwa mambo yanayowafanya wanawake kuwa viumbe maalum kabisa..


.
 
Kuna kauli wakuu inassema kwamba kumfahamu mwanamke vizuri itakuchukua thamani ya muda wako wa miaka. Mfano kama una miaka 20 itakuhitaji mingine 20 miaka kumuelewa au kama una 25yrs inakuhitaji mengine 25 kumuelewa. Sasa sijui kuna ukweli ndani yake au ni vipi wakuu. Nawasilisha
 
Ukiona umeanza kumuelewa mwanamke basi jua unakaribia kufa. Siwezi tumia nguvu zangu eti nataka kumuelewa Mwanamke
 
Back
Top Bottom