Huu ni ugonjwa gani?

KingPower

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2015
Posts
1,144
Reaction score
1,888
Habari wana JF mwanangu yamemtoka mapele ya ajabu,
Wife amempeleka hospital Jmosi na anatumia dawa Ila bado vinamtoka

Naombeni msaada wenu Kwa anaeujua huu ugonjwa vizuri.

Wengine wanasema ni Tetekuwanga Ila navoujua huu ugonjwa unatoka mwili mzima Ila yeye umemtoka kifuani, mgongoni na shingoni Tu .

Nimeplan ikibidi kesho twende tena hospital.

Karibu Kwa ushauri.


 
Vimemuanza lini ?

Je anavyo usoni hivyo vipele ?

Asante.
 
Mtoto amepata chanjo zote za awali?

Je mtoto anapata homa, kujikuna, kukosa hamu ya kula n.k?

Kwa kutazama haraka inaonekana kama ni chicken pox (tetekuwanga), ni byema umfikishe mtoto hospitali kwa uchunguzi zaidi
 
Tuwasiliane kwa namba hii 0678211747 Hata mimi mdogo wangu aliugua kwa muda mrefu lakini saiv amepona kabisa
 
Ikiwa sio tetekuwanga basi ni ugonjwa mmoja hivi wapare wanauita kiguma.

Ongea na wapare wa milimani, wiki tu mtoto amepona.

Atapewa dawa fulani ya asili apake na kumeza.

Hospitali utanunulishwa dawa hadi basi na huenda sizifae chochote.

Pole sana mkuu.
 
Nimepanga nimpeleke tena

Yes chanjo zote amepata bado ya mwaka mmoja na nusu

Yeah kuna Muda vinamuwasha (anajikuna) pia vipele vilimjia na kikohozi Ila sasa kikohozi ni kama amepona.
Mtoto amepata chanjo zote za awali?

Je mtoto anapata homa, kujikuna, kukosa hamu ya kula n.k?

Kwa kutazama haraka inaonekana kama ni chicken pox (tetekuwanga), ni byema umfikishe mtoto hospitali kwa uchunguzi zaidi
 
Asante Mkuu Kwa ushauri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…