Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,877
- 2,758
Kiukweli kikwete anahitaji changamoto ili aamke alikolala. Jana aliongea sana juu ya TUCTA. Mengine ya ukweli, mengine vitisho, mengine kujitetea, na mengine ushauri, n.k. Lakini ukweli unabaki palepale kuwa tunahitaji kina mgaya wengi wa kumchangamsha rais anayeona kuwa kila kitu ni shwari kumbe sio. Takwimu zake alizotoa si za kimantiki kiivyo. Kuna hela nyingi sana zinavuja nchi hii ambazo zingeweza kuboresha mambo. Rais asingoje kuwaka na kutoa vitisho yanapotokea ya tucta. Ni kweli katishika kwani hajawahi kuona hayo yakitokea. Rais wetu ni muongeaji mzuri ila si mtekelezaji. Kasema kuwa yeye ndie mwajiri mkuu. Hajajua kuwa sisi wananchi ndio tumemwajiri? Kama haamini hilo basi asitekeleze matakwa ya watanzania