Namkubali na kumuunga mkono sana mh raisi wetu. Lkn kwa suala la Makonda na vyeti kama ni kweli alinunua cha mtu na anamtetea napinga kwa nguvu zote kama ifuatavyo
1. Kuna wtz inasemekana wamekufa kwa pressure sbb ya vyeti.
2. Kuna wtz wamepoteza kazi sbb ya vyeti.
3. kuna wtz wamesimamishiwa mishahara sbb ya utata wa vyeti.
4. Kuna wtz wametumia resources zao (pesa) kwenda Dar necta kutatua changamoto za vyeti.
5. kuna wtz wameshindwa kuajiriwa ssb ya utumishi na vyeti hewa.
6. Wtz hawajapata legal increment kwenye mishahara yao na kutopanda madaraja sbb inasemwa uhakiki.
7. kuna wtz wameitwa vilaza sbb ya vyeti vyao kuwa na performance isiyoridhisha ilihari necta imesema wamefaulu.
8. kuna wtz wanafukuzwa vyuoni kwsbb tunaambiwa hawana sifa.
9. kuna wtz wamekwama kwenda elimu ya juu sbb GPA zao hazifiki 3.0.
10. Serikali imetumia mamilioni ya fedha sabb ya kuhakiki watumishi na vyeti vyao.
Nb. pamoja nayo mh. alisema watu waajiliwe kwa elimu yao, wewe kama ni la saba uwe kuli na hakuna atakaye kusumbua. Pia sijaelewa nguvu kubwa inayotumika kumtetea rc, badala ya nguvu hiyo kusema wazi anasingiziwa au kweli alicheza mchezo mchafu.
Mwisho zoezi la uhakiki litakuwa halina maana yoyote kama hatutakuwa na similar treatment kwa wote. Haiingii akilini mwaka mzima mkulu na serikali imesimamia uhakiki wa watumishi na vyeti pia elimu kwa ujumla halafu leo zoezi liharibike kirahisi tu. Tutakuwa tumepata hasara kubwa sana ya resources na time factor.
Mh mkulu kama rc yuko vizuri kivyeti ithibitishwe mjadala ufungwe, na hata rc atakuwa huru kutekeleza majukumu yake vyema.
Ushauri kwa rc, tafadhali mpunguzie raisi wetu mzigo huu wa kukutetea kwa kuprove wrong wanaokuamdama kwa kuweka hadharani vyeti.
Nakukubali Makonda ktk utendaji na raisi anakukubali hata ukiwa la saba bado mkulu ndiye mteuaji, utabaki rc tena Dar hapa hapa.