Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,201
- 254
Tumekuwa tunalalamika sana kuhusu watangazaji wa baadhi ya vituo vya redio na televisheni kutumia lugha chafu ambazo haziendani na maadili ya utangazaji bila vituo hivi wala tangangazaji hawa na wahariri wao kuchukuliwa hatua zozote zile za kinidhamu na waajiri au vyombo vinavyosimamia taaluma hizi .
Wiki iliyopita katika kuto cha Clouds mmoja watangazaji maarufu wa kutuo hicho Bwana Gerald Hando aliamua kuendelea kuvunja maadili haya kwa mara nyingi kwa kujiamini na kwa kurudiarudia kauli zake kama vile wanaosikiliza ni wa upande wake peke yake au hata haieleweki alikuwa ujumbe huo anawapelekea wakina nani haswa .
Kulikuwa na msikilizaji mmoja aliuliza , hivi chuo cha mafisadi kiko wapi ? nataka kusomea na mimi niwe fisadi , jamaa Gerald akaibuka akasema kiko kule ukivuka bahari kama unaenda Zanzibar alimaanisha kigamboni , mwenye kujua kule kule kigamboni kuna chuo gani atakuwa anajua kimeongelewa nini hapo .
Ajue kwamba radio ile inasikilizwa na watu wengi sana watu wenye umri mbali mbali na vyama mbali mbali vya siasa , kijamii na vya kidogo anavyotoa kauli kama zile ni uchokozi na ukosefu wa nidhamu ya utangazaji na kudhalilisha wanaokimiliki chuo hicho , hata hao wanaotajwa mafisadi hakuna hata mmoja aliyefikishwa mahakamani mpaka sasa hivi kwa tuhuma hizo kwahiyo yeye sio hakimu aanze kuhukumu watu .
Pili akaja na kituko kingine msikilizaji aliuliza swali kuhusu hadhi ya zanziber kama ni nchi , akasema yeye haitambui Zanzibar hata kidogo yeye anaitambua Tanganyika , na pale alipo yuko Tanganyika sio Tanzania msimamo wake ni huo huo wenzake wakaanza kucheka na kumshangilia kama vile alivyofanya ni sahihi kabisa .
Baada ya hili kuna kutuo kimoja cha radio kwa jina la radio kheri nacho kimekuwa kikiruhusu wachambuzi wa dini na wanazuoni wake kutumia lugha chafu na uchochezi dhidi ya dini nyingine bila hatua zozote zile kuchukuliwa na wasimamizi wa vituo hivi au taasisi ya mawasiliano .
Kama uhuru wenyewe wa habari ndio huu basi , njia tunayoelekea sio hii hata kidogo , tunataka kujenga jamii zinazoheshimika na kuheshimu jamii za wenzao na kuvumiliana tunataka kuona watangazaji wasiokuwa na upande wowote wa chama au dini wakati wa kuwasilisha mada na makala zao zingine kama wao ni wanachama wa chama Fulani au dini Fulani basi waweke wazi tujue misimamo yao ndio hiyo na hiyo ni misimamo vya vituo vyao na wahariri wa vyombo hivyo wamekubali hivyo
Wiki iliyopita katika kuto cha Clouds mmoja watangazaji maarufu wa kutuo hicho Bwana Gerald Hando aliamua kuendelea kuvunja maadili haya kwa mara nyingi kwa kujiamini na kwa kurudiarudia kauli zake kama vile wanaosikiliza ni wa upande wake peke yake au hata haieleweki alikuwa ujumbe huo anawapelekea wakina nani haswa .
Kulikuwa na msikilizaji mmoja aliuliza , hivi chuo cha mafisadi kiko wapi ? nataka kusomea na mimi niwe fisadi , jamaa Gerald akaibuka akasema kiko kule ukivuka bahari kama unaenda Zanzibar alimaanisha kigamboni , mwenye kujua kule kule kigamboni kuna chuo gani atakuwa anajua kimeongelewa nini hapo .
Ajue kwamba radio ile inasikilizwa na watu wengi sana watu wenye umri mbali mbali na vyama mbali mbali vya siasa , kijamii na vya kidogo anavyotoa kauli kama zile ni uchokozi na ukosefu wa nidhamu ya utangazaji na kudhalilisha wanaokimiliki chuo hicho , hata hao wanaotajwa mafisadi hakuna hata mmoja aliyefikishwa mahakamani mpaka sasa hivi kwa tuhuma hizo kwahiyo yeye sio hakimu aanze kuhukumu watu .
Pili akaja na kituko kingine msikilizaji aliuliza swali kuhusu hadhi ya zanziber kama ni nchi , akasema yeye haitambui Zanzibar hata kidogo yeye anaitambua Tanganyika , na pale alipo yuko Tanganyika sio Tanzania msimamo wake ni huo huo wenzake wakaanza kucheka na kumshangilia kama vile alivyofanya ni sahihi kabisa .
Baada ya hili kuna kutuo kimoja cha radio kwa jina la radio kheri nacho kimekuwa kikiruhusu wachambuzi wa dini na wanazuoni wake kutumia lugha chafu na uchochezi dhidi ya dini nyingine bila hatua zozote zile kuchukuliwa na wasimamizi wa vituo hivi au taasisi ya mawasiliano .
Kama uhuru wenyewe wa habari ndio huu basi , njia tunayoelekea sio hii hata kidogo , tunataka kujenga jamii zinazoheshimika na kuheshimu jamii za wenzao na kuvumiliana tunataka kuona watangazaji wasiokuwa na upande wowote wa chama au dini wakati wa kuwasilisha mada na makala zao zingine kama wao ni wanachama wa chama Fulani au dini Fulani basi waweke wazi tujue misimamo yao ndio hiyo na hiyo ni misimamo vya vituo vyao na wahariri wa vyombo hivyo wamekubali hivyo