Huu ndio mwisho wa CLOUDS FM

Huu ndio mwisho wa CLOUDS FM

Mimi na familia yangu hatutatizama wala kusikiliza Clouds FM wala TV yao! Hakuna cha PJ wala Bonge tena!!! Jamii imetufumbua macho kumbe ni wanyama hivi!!!!!!!
 
Sanaa isiwe ngazi ya kutengeneza masikini wenye majina makubwa,sanaa iwe kazi

susia skylight pale Thai village
susia matamasha yao na fiesta
susia tv yao ya wafanyakazi majungu
susia radio yao ya maboss wafitini

kaa mbali na majangili wa bongofleva
Hivi kumbe Skylight band ni mali ya Clouds FM?
 
Wana jamvi wenzangu tuige nyendo za Naibu spika J. Ndugai, alisema sintowatoa nje wala kuwaadhibu wapinzani(M4C) tena maana kw akadri ninavyowachukulia hatua ndivyo ninavyowapromoti". Dawa ya mjinga ni kumpuuza tu.
 
Mimi na familia yangu hatutatizama wala kusikiliza Clouds FM wala TV yao! Hakuna cha PJ wala Bonge tena!!! Jamii imetufumbua macho kumbe ni wanyama hivi!!!!!!!

Acha kuwadanganya watu mkeo Mamaa Ponela ni mtuma sms mzuri sana wa kipindi cha Diva cha ala za roho.
 
Harakati zinaendelea kama kawaida mpaka tunahakikisha clouds fm tunaizika. Ingia facebook tafuta page inaitwa mazishi YA clouds FM, huku ndiko harakat zinaendelea na kuwavua nguo clouds fm na maovu yao.

Waswahili hatutakuja kuendelea kamwe hata miaka 200 ijayo, kila mtu anapopiga hatua kuna watu wanakuvuta nyuma, mnaendekeza majungu mnachosahau ni kwamba hawa jamaa wa Clouds wana mchango mkubwa sana ktk Uchumi na maendeleo ya Jamii yetu, watu wengi sana wamepata Ajira ya moja kwa moja na kuweza kuendesha Maisha yao, sasa mnataka mtu afanye nini tena zaidi ya hapo?

Kila siku mnalalamika watu wanamaliza Vyuo hawana ajira, leo hii watu wamejituma wameanzisha kitu ambacho kinatoa ajira bado mnawapiga vita mnataka wafirisike, sasa sijui ili iweje?

Na cha kusikitisha zaidi Wageni ambao wanatuibia kama Wahindi, Wazungu, waarabu,Wachina n.k hamuwaoni, mmekaa kimya, ila Waswahili wenzenu, mnawaleta majungu, arrgghhhhh!

 
Duh mnapoteza muda kweli jamaa ndo wanapaa

Utaona wanapaa ila impact yake ni kubwa sana hasa wanavyozidi kupoteza wasikilizaji. Ila naamini haki siku zote itasimama
 
Wasanii waache kuishambulia Clouds FM kwa maneno.Clouds FM ni wafanyabiashara kama wengine.Ni waajiri kama waajiri wengine. Wanahitaji faida,wanahitaji kulipa kodi,wanahitaji kusaidia jamii.Kitu muhimu ni wasanii kuungana pamoja na ku-'negotiate better deals' na Clouds FM.Bila umoja hakuna la ziada.Kuishambulia Clouds FM bado hamjatenda haki..'They have got families to feed also..'
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom