Jamani, kwani radio ziko ngapi hapa TZ?
Kwa nini usiridhike na mziki wako kupigwa na vituo vingine vya radio, mpaka iwe Clouds?
Acheni chuki, ile ni radio binafsi na ikiona muziki wako hauna standards za kupigwa kwenye radio yao kaa kimya, mbona kuna nyimbo kibao tu zinakaushiwa lakini inabidi kuziachia kwa sababu watu wanaziomba sana?
Mara ngapi Jay Dee nyimbo zake zimepigwa kwenye Jahazi kipindi yupo mumewe? Kipindi cha masaa 2.5 nyimbo zaidi ya nne za mtu mmoja? Mbona hakumwambia mumewe kupunguza ili wasanii wengine wapate nafasi?
Leo amechuniwa analalama, walikupandisha, watakushusha!
Clouds ni taasisi, Jay Dee ni mtu mdogo sana kuishusha, kashajua Clouds wamemchunia, Tuzo hatapata, analalamika!