Leejay49
JF-Expert Member
- Feb 10, 2023
- 19,295
- 60,919
Wakuu habari ya weekend,,.
Vipi mmeshatoka jumuiya??,,Na bahasha za pasaka vipi mlisharudisha wote au kunaa wengine bado mnazo ndani?😃,.
Leo buana mama aliniomba tusaidizane kupanga vitu chumbani kwake,. Nimeshangaa kuona eti bado anatunza madaftari yangu ya chekechea😃😆😆,. Kwanza nlivyoona mwandiko ikabidi kwanza nianze kucheka,.
Ni hivi,. Ule mwaka naanza shule kwa kumbukumbu zangu mama alikuwaga kusoma,. Alirudi alinikuta niko chekechea mwaka wa pili ule,. Ile siku amerudi akaanza kuniuliza habari za shule akataka niandike ,. Amenipa daftari na penseli ananitajia maneno ya kuandika nikaanza kuandika pale ananisifia kwelikweli kumbe alikua na jambo lake bwana,. Akasubiri baba amerudi akaanza kumhoji eti " kwanini umeruhusu mtoto anatumia mkono wa kushoto kula na kuandika???"...
Hakuna aliyewaza kama alikua serious akaanza kuniambia hataki anione natumia mkono wa kushoto si nikajua utani labda mwe🥲,. Ilikua akinituma kitu nimpe au kupokea kitu kwa mkono wa kushoto nachapwa,. Akaniambia hadi shuleni hakuna kuandikia mkono wa kushoto,. Basi nkirudi nyumbani anaanza kunifundisha kuandika upya kwa mkono wa kulia na nikisema tu hata nimechoka nachapwa,. Madaftari nikirudi nyumbani anakagua anauliza ulitumia mkono gani kuandika nikisema wa kulia basi ananipa karatasi andika tena kama hivi kwa kutumia mkono wa kulia Asa ole nikosee anajua nimeandika kwa mkono wa kushoto nachapwaa,.basi nitahangaika mpaka nitaweza,. Hadi shule sasa badae nikawa naogopa kuandika, basi nitajikakamua wee niandike tu kwa mkono wa kulia ilimradi tu nikirudi nyumbani nisichapwe,.
Hadi walimu shuleni walikua wanashangaa, mama akiitwa kuambiwa anachokifanya sio sawa alikua anawajibu tu huyu ni mwanangu na atakua vile mimi nataka awe,. Walikua wanagombana na baba karibu kila siku kwamba anakazania kitu ambacho Mungu ameniumba nacho,. mpaka tu mzee alishazoea akiona nimeitwa na mama kusoma au kuandika ye huyo anaondoka zake maana alikua hapendi makelele asa vile navyochapwa na mama akikazania jambo lake,.
Kweli niliteseka ile chekechea mpaka nakuja kumaliza nilishaanza kuzoea sasa kuandikia mkono wa kulia,. La kwanza napo kwa shida shida hivyohivyo mpaka mikono ikawa na nguvu kiasi kwamba hata nikiwa naandika kwa mkono wa kushoto najistukia nahisi mama ananiona😃😅😅,..
But guess what.........,,. Kuanzia darasa la pili na kuendelea hadi leo mkono wangu wa kulia ndio unafanya shughuli zote,. Wa kushoto eti ndio naona umelegea sikuizi 😂😂😂😂
Ni hivyo tu,. Mnavyosoma hii namalizia kupanga vitu hapa nawahadithieni kisa kingine cha mdogo wangu aliyenifatia ana kigugumizi alivyokua anateseka na yeye ,. Ila mama🙌🙌
Endelea link hiyo hapo chini
Huu msemo "Samaki mkunje angali mbichi" uko Real sana
Vipi mmeshatoka jumuiya??,,Na bahasha za pasaka vipi mlisharudisha wote au kunaa wengine bado mnazo ndani?😃,.
Leo buana mama aliniomba tusaidizane kupanga vitu chumbani kwake,. Nimeshangaa kuona eti bado anatunza madaftari yangu ya chekechea😃😆😆,. Kwanza nlivyoona mwandiko ikabidi kwanza nianze kucheka,.
Ni hivi,. Ule mwaka naanza shule kwa kumbukumbu zangu mama alikuwaga kusoma,. Alirudi alinikuta niko chekechea mwaka wa pili ule,. Ile siku amerudi akaanza kuniuliza habari za shule akataka niandike ,. Amenipa daftari na penseli ananitajia maneno ya kuandika nikaanza kuandika pale ananisifia kwelikweli kumbe alikua na jambo lake bwana,. Akasubiri baba amerudi akaanza kumhoji eti " kwanini umeruhusu mtoto anatumia mkono wa kushoto kula na kuandika???"...
Hakuna aliyewaza kama alikua serious akaanza kuniambia hataki anione natumia mkono wa kushoto si nikajua utani labda mwe🥲,. Ilikua akinituma kitu nimpe au kupokea kitu kwa mkono wa kushoto nachapwa,. Akaniambia hadi shuleni hakuna kuandikia mkono wa kushoto,. Basi nkirudi nyumbani anaanza kunifundisha kuandika upya kwa mkono wa kulia na nikisema tu hata nimechoka nachapwa,. Madaftari nikirudi nyumbani anakagua anauliza ulitumia mkono gani kuandika nikisema wa kulia basi ananipa karatasi andika tena kama hivi kwa kutumia mkono wa kulia Asa ole nikosee anajua nimeandika kwa mkono wa kushoto nachapwaa,.basi nitahangaika mpaka nitaweza,. Hadi shule sasa badae nikawa naogopa kuandika, basi nitajikakamua wee niandike tu kwa mkono wa kulia ilimradi tu nikirudi nyumbani nisichapwe,.
Hadi walimu shuleni walikua wanashangaa, mama akiitwa kuambiwa anachokifanya sio sawa alikua anawajibu tu huyu ni mwanangu na atakua vile mimi nataka awe,. Walikua wanagombana na baba karibu kila siku kwamba anakazania kitu ambacho Mungu ameniumba nacho,. mpaka tu mzee alishazoea akiona nimeitwa na mama kusoma au kuandika ye huyo anaondoka zake maana alikua hapendi makelele asa vile navyochapwa na mama akikazania jambo lake,.
Kweli niliteseka ile chekechea mpaka nakuja kumaliza nilishaanza kuzoea sasa kuandikia mkono wa kulia,. La kwanza napo kwa shida shida hivyohivyo mpaka mikono ikawa na nguvu kiasi kwamba hata nikiwa naandika kwa mkono wa kushoto najistukia nahisi mama ananiona😃😅😅,..
But guess what.........,,. Kuanzia darasa la pili na kuendelea hadi leo mkono wangu wa kulia ndio unafanya shughuli zote,. Wa kushoto eti ndio naona umelegea sikuizi 😂😂😂😂
Ni hivyo tu,. Mnavyosoma hii namalizia kupanga vitu hapa nawahadithieni kisa kingine cha mdogo wangu aliyenifatia ana kigugumizi alivyokua anateseka na yeye ,. Ila mama🙌🙌
Endelea link hiyo hapo chini
Huu msemo "Samaki mkunje angali mbichi" uko Real sana