Huu msamiati mpya humu Shuleni na Vyuoni umeingia lini?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
60,443
120,800
Nimeshangaa sana hadi sasa hivi najiuliza na sipati majibu kwani muda si mrefu matokeo yetu ya Mtihani wa Kozi moja hivi ninayoifanya yametoka online na kuna njemba fulani zinaijua namba yangu ya Mtihani wamenipigia Simu huku wakiwa wanacheka huku wakiniambia kuwa Mimi na Wao tume Bashite hivyo eti tunatakiwa kufanya Kimeo chetu cha Sup siku ya Jumanne.

Kama hiyo haitoshi juzi Ijumaa wakati napita pembezoni mwa Shule moja ya Sekondari nikamsikia kwa masikio yangu Mwalimu Mkuu wao akisema naomba nimnukuu " Nyie Wanangu Shule nzima tunawaamini hivyo mwaka huu katika Mtihani wenu wa kumaliza Kidato cha nne hatutaki mtuletee Mabashite mengi hapa kwani mtakuwa mmetuaibisha sana na sijui tutaficha wapi hizi sura zetu " mwisho wa kumnukuu.

Naomba nipatiwe maana na dhana nzima ya huu Msamiati mpya na ambao naona unaanza kushika kasi wa neno Bashite kwani binafsi mpaka sasa sijajua una maana gani ila nikaona kwakuwa humu JF kuna Great Thinkers wa kutukuka kabisa basi sitakosa majibu yake.

Nitawashukuruni na nawasilisha.
 
Ha ha ha ha ha ha ha ha ...... Mkuu nimecheka tu hapo ili kukuonyesha ushirikiano ila sijakuelewa hapo na Wewe uliponiambia Mimi ni Bashite mkubwa. Je umemaanisha nini Mkuu? Kama vipi basi na Wewe ni Bashite vile vile!
tafadhali niombe msamaha mkuu..!!mimi unajua nahasira sana unaniitaje hilo jina!!bashite maanake ukoko ulio ungua
 
tafadhali niombe msamaha mkuu..!!mimi unajua nahasira sana unaniitaje hilo jina!!bashite maanake ukoko ulio ungua

Nakuomba sana radhi Mkuu Bashite kwa kuku Bashite hivyo. Nataka kulala sasa na namwomba Mwenyezi Mungu usingizi wangu nao usipatwe na Mabashite mengi hapo katikati.
 
Haya maneno bhana sijui ni misemo au misimu yazuka kwa kasi tuu

√√utajiju
√√mwendo kasi
√√Mungu anakuona

*Bashit*

hili neno sidhani kama litaweza kuchuja kama hayo mengine
 
Nimeshangaa sana hadi sasa hivi najiuliza na sipati majibu kwani muda si mrefu matokeo yetu ya Mtihani wa Kozi moja hivi ninayoifanya yametoka online na kuna njemba fulani zinaijua namba yangu ya Mtihani wamenipigia Simu huku wakiwa wanacheka huku wakiniambia kuwa Mimi na Wao tume Bashite hivyo eti tunatakiwa kufanya Kimeo chetu cha Sup siku ya Jumanne.

Kama hiyo haitoshi juzi Ijumaa wakati napita pembezoni mwa Shule moja ya Sekondari nikamsikia kwa masikio yangu Mwalimu Mkuu wao akisema naomba nimnukuu " Nyie Wanangu Shule nzima tunawaamini hivyo mwaka huu katika Mtihani wenu wa kumaliza Kidato cha nne hatutaki mtuletee Mabashite mengi hapa kwani mtakuwa mmetuaibisha sana na sijui tutaficha wapi hizi sura zetu " mwisho wa kumnukuu.

Naomba nipatiwe maana na dhana nzima ya huu Msamiati mpya na ambao naona unaanza kushika kasi wa neno Bashite kwani binafsi mpaka sasa sijajua una maana gani ila nikaona kwakuwa humu JF kuna Great Thinkers wa kutukuka kabisa basi sitakosa majibu yake.

Nitawashukuruni na nawasilisha.
Pole bhana so umebashite sap ngap
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom