Unakula ugali! Chakula ambacho mwilini mwako hakiongezi chochote kile. Tunadanganyana kuutetea ugali kwamba unaongeza nguvu! Nguvu gani ugali umewahi kuongeza? Ugali unaongeza nini mwilini mwako? Unajaza tumbo ila baadaye ukipimwa unaonekana mwili wako haukuwa na chakula.
Majuzi wakati nakula chipsi banda la mpira, jamaa akaniambia nile ugali. Nikamwambia kwa nini nile ugali? Akasema ili niwe na nguvu. Nikamwambia tukimchukua mla ugali, mchezaji wa Kitanzania na tukamuweka na Halaand mla chipsi mayai nani atakuwa na nguvu?
Tunautetea sana ugali, chakula ambacho hakiliwi kwa wenzetu kwa kuwa wanajua hakiongezi chochote mwilini. Chakula ambacho hata kwa Kiingereza kinabaki hivyohivyo, ugali.
Bro! Tafuta pesa, ugali ni chakula cha kula kwa hamu tu na si kuwa kwenye ratiba. Ule ugali ukiwa na hamu na si kiwe kwenye ratiba. Utafiti wa chuo kimoja Kenya nadhani kiligundua matatizo mengi ya Kiafrika akilini yanatokana na ulaji mkubwa wa ugali, akili haipati nguvu.