Hurray! Tumegundua mafuta darajani! 😂

Hurray! Tumegundua mafuta darajani! 😂

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
370,974
Reaction score
858,957
Wakati wa kazi zinazoendelea sasa za kupanua barabara ya eneo la Darajani, Zanzibar, wakandarasi wamechimba ardhini na kuligundua daraja la zamani lililokuwa limefukiwa kwa miaka mingi.

Chini ya beams za daraja hilo wamekutwa maji meusi yaliyochanganyika na mafuta machafu.

Lakini kabla hatujaanza kugawana vitalu vya mafuta, tukumbuke historia.

Eneo la Darajani zamani lilikuwa mkondo wa bahari uliotenganisha Mji Mkongwe na Ngambo. Ukitaka kwenda Kikwajuni, ilibidi uvuke kwenye daraja hilo ndiyo maana eneo hilo likaitwa Darajani na upande wa pili uliitwa Ngambo .

Wakati wa Serikali ya Sultan Seyyid Khalifa, ilifanyika reclamation ya eneo hilo. Kwa mujibu wa wazee, daraja halikuvunjwa. Lilifukiwa pamoja na mkondo wa bahari kwa kutumia mawe, mchanga na hata takataka za aina mbalimbali.

Leo, wakati barabara inapanuliwa, daraja hilo la zamani limegunduliwa tena.

Chini yake kuna maji machafu yaliyochanganyika na mafuta. Huenda huo ni uchafu unaotokana na takataka zilizotumika kuufukia mkondo huo wa bahari miaka mingi iliyopita.

Lakini kichekesho kikubwa zaidi si daraja wala hayo “mafuta.”

Maafisa wa Manispaa, Ofisi ya Meya na taasisi nyingine walipofika eneo hilo, wakasema kwa mshangao:

“Hatuna kumbukumbu zozote kuhusu daraja hili!”

Kweli?

Eneo linaitwa Darajani, lakini taasisi zetu hazina kumbukumbu ya daraja! Hii ni sawa na kwenda Uwanja wa Ndege halafu kuuliza: “Ndege zilianza lini kufika hapa?”

Badala ya kuwaita wanahistoria, wataalamu wa mambo ya kale na wahandisi kuchunguza ugunduzi huu, hatua ya haraka ikawa

kuweka ulinzi watu wasiibe yale “mafuta”! 😂

Hongereni Zanzibar!

Tumepoteza kumbukumbu za daraja, lakini tumelinda mafuta yake.

Sasa tunasubiri taarifa rasmi:

“Zanzibar yagundua mafuta Darajani; uzalishaji waanza chini ya daraja la Sultan!”

Hili si jambo la kuchekesha pekee. Ni aibu kwa taasisi za umma kutokuwa na kumbukumbu za historia ya eneo maarufu kiasi hiki. Daraja hilo linaweza kuwa sehemu muhimu ya urithi wetu na ushahidi wa namna Stone Town ilivyokuwa imetenganishwa na Ngambo kabla ya kufanyika reclamation.

Tusije tukaliharakia kulifukia tena kabla halijachunguzwa na kuhifadhiwa kihistoria halafu vizazi vijavyo vikaja kuligundua kwa mara ya tatu na kutangaza kuwa vimepata gesi! 😂

Credit: Abuu Shani Ally Saleh Farid Himid Omar Said Shaaban
1787018306615.jpg
1787018310672.jpg
1787018314601.jpg
 
Wakati wa kazi zinazoendelea sasa za kupanua barabara ya eneo la Darajani, Zanzibar, wakandarasi wamechimba ardhini na kuligundua daraja la zamani lililokuwa limefukiwa kwa miaka mingi.

Chini ya beams za daraja hilo wamekutwa maji meusi yaliyochanganyika na mafuta machafu.

Lakini kabla hatujaanza kugawana vitalu vya mafuta, tukumbuke historia.

Eneo la Darajani zamani lilikuwa mkondo wa bahari uliotenganisha Mji Mkongwe na Ngambo. Ukitaka kwenda Kikwajuni, ilibidi uvuke kwenye daraja hilo ndiyo maana eneo hilo likaitwa Darajani na upande wa pili uliitwa Ngambo .

Wakati wa Serikali ya Sultan Seyyid Khalifa, ilifanyika reclamation ya eneo hilo. Kwa mujibu wa wazee, daraja halikuvunjwa. Lilifukiwa pamoja na mkondo wa bahari kwa kutumia mawe, mchanga na hata takataka za aina mbalimbali.

Leo, wakati barabara inapanuliwa, daraja hilo la zamani limegunduliwa tena.

Chini yake kuna maji machafu yaliyochanganyika na mafuta. Huenda huo ni uchafu unaotokana na takataka zilizotumika kuufukia mkondo huo wa bahari miaka mingi iliyopita.

Lakini kichekesho kikubwa zaidi si daraja wala hayo “mafuta.”

Maafisa wa Manispaa, Ofisi ya Meya na taasisi nyingine walipofika eneo hilo, wakasema kwa mshangao:

“Hatuna kumbukumbu zozote kuhusu daraja hili!”

Kweli?

Eneo linaitwa Darajani, lakini taasisi zetu hazina kumbukumbu ya daraja! Hii ni sawa na kwenda Uwanja wa Ndege halafu kuuliza: “Ndege zilianza lini kufika hapa?”

Badala ya kuwaita wanahistoria, wataalamu wa mambo ya kale na wahandisi kuchunguza ugunduzi huu, hatua ya haraka ikawa

kuweka ulinzi watu wasiibe yale “mafuta”! 😂

Hongereni Zanzibar!

Tumepoteza kumbukumbu za daraja, lakini tumelinda mafuta yake.

Sasa tunasubiri taarifa rasmi:

“Zanzibar yagundua mafuta Darajani; uzalishaji waanza chini ya daraja la Sultan!”

Hili si jambo la kuchekesha pekee. Ni aibu kwa taasisi za umma kutokuwa na kumbukumbu za historia ya eneo maarufu kiasi hiki. Daraja hilo linaweza kuwa sehemu muhimu ya urithi wetu na ushahidi wa namna Stone Town ilivyokuwa imetenganishwa na Ngambo kabla ya kufanyika reclamation.

Tusije tukaliharakia kulifukia tena kabla halijachunguzwa na kuhifadhiwa kihistoria halafu vizazi vijavyo vikaja kuligundua kwa mara ya tatu na kutangaza kuwa vimepata gesi! 😂

Credit: Abuu Shani Ally Saleh Farid Himid Omar Said ShaabanView attachment 3652322View attachment 3652323View attachment 3652324
Mashalaah mashalaaah
Mie sasa nitakuwa muungujah!!
 
#MAKINIKIA: HEKAYA FUPI YA ENEO MAARUFU LA DARAJANI, ZANZIBAR

Kwa uliefika Zanzibar lazima utakuwa umepita eneo maarufu la Darajani, upande wa pili wa Marikiti. Na bila ya shaka umejiuliza li wapi hilo daraja?

Darajani Bridge, au “Daraja la Darajani,” lililokuwepo kati ya Stone Town na Ng'ambo huko Zanzibar, halipo tena kwa sababu ya mabadiliko makubwa ya mazingira yaliyofanywa na utawala wa kikoloni wa Kiingereza katika nusu ya kwanza ya karne ya 20.

Wakati huo, kulikuwa na mkondo mkubwa wa maji ya bahari (tidal creek) uliopita eneo hilo. Mkondo huo ulikuwa chanzo kikubwa cha mbu waliokuwa wakisababisha milipuko ya malaria.

Hivyo basi, kati ya mwaka 1913 hadi 1957, serikali ya mkoloni ilianzisha mradi mkubwa wa kuivua ardhi hiyo (land reclamation) kwa kuujaza mkondo huo wa maji ili kupunguza mazalia ya mbu.
Matokeo yake, sehemu hiyo ya mkondo ikajazwa kabisa kwa udongo, na hivyo daraja la Darajani likawa halihitajiki tena—hatimaye likatoweka kabisa.

Eneo ambalo lilikuwa la daraja sasa limebadilika na kuwa sehemu ya mji wa kisasa, hususan maeneo ya karibu na Soko la mtaa wa Darajani ambalo kwa sasa ni kitovu cha shughuli za biashara mjini Zanzibar.

Kwa kifupi, daraja hilo lilitoweka si kwa kubomolewa tu, bali kwa sababu ya mabadiliko ya ardhi yaliyolenga kuimarisha afya ya jamii kwa kupunguza malaria, sambamba na kuunganisha maeneo ya zamani ya Stone Town na Ng’ambo kuwa mji mmoja ulioungana vizuri.

Ukisimama pale Darajani leo, huwezi hata kudhani kuwa palikuwa na daraja linalopita juu ya maji. Maendeleo yamefanya eneo hilo kusahaulika kihistoria—lakini kwa wakongwe wa Zanzibar, watakwambia "kulikuwa na daraja hapo zamani!"

#makinikiyayahabari
#zanzibar
#darajani
#stonetown
1787019469797.jpg
1787019465485.jpg
 
Yaa siyo darajani asilimia kubwa unguja kuna mafuta ikitokea muungano ukavunjika bas watutawapita kimaendelea wale jamaa watatuacha mbali sana ambacho kiwapendi ni ile ubifasi sana tofauti na wapemba
 
Wakati wa kazi zinazoendelea sasa za kupanua barabara ya eneo la Darajani, Zanzibar, wakandarasi wamechimba ardhini na kuligundua daraja la zamani lililokuwa limefukiwa kwa miaka mingi.

Chini ya beams za daraja hilo wamekutwa maji meusi yaliyochanganyika na mafuta machafu.

Lakini kabla hatujaanza kugawana vitalu vya mafuta, tukumbuke historia.

Eneo la Darajani zamani lilikuwa mkondo wa bahari uliotenganisha Mji Mkongwe na Ngambo. Ukitaka kwenda Kikwajuni, ilibidi uvuke kwenye daraja hilo ndiyo maana eneo hilo likaitwa Darajani na upande wa pili uliitwa Ngambo .

Wakati wa Serikali ya Sultan Seyyid Khalifa, ilifanyika reclamation ya eneo hilo. Kwa mujibu wa wazee, daraja halikuvunjwa. Lilifukiwa pamoja na mkondo wa bahari kwa kutumia mawe, mchanga na hata takataka za aina mbalimbali.

Leo, wakati barabara inapanuliwa, daraja hilo la zamani limegunduliwa tena.

Chini yake kuna maji machafu yaliyochanganyika na mafuta. Huenda huo ni uchafu unaotokana na takataka zilizotumika kuufukia mkondo huo wa bahari miaka mingi iliyopita.

Lakini kichekesho kikubwa zaidi si daraja wala hayo “mafuta.”

Maafisa wa Manispaa, Ofisi ya Meya na taasisi nyingine walipofika eneo hilo, wakasema kwa mshangao:

“Hatuna kumbukumbu zozote kuhusu daraja hili!”

Kweli?

Eneo linaitwa Darajani, lakini taasisi zetu hazina kumbukumbu ya daraja! Hii ni sawa na kwenda Uwanja wa Ndege halafu kuuliza: “Ndege zilianza lini kufika hapa?”

Badala ya kuwaita wanahistoria, wataalamu wa mambo ya kale na wahandisi kuchunguza ugunduzi huu, hatua ya haraka ikawa

kuweka ulinzi watu wasiibe yale “mafuta”! 😂

Hongereni Zanzibar!

Tumepoteza kumbukumbu za daraja, lakini tumelinda mafuta yake.

Sasa tunasubiri taarifa rasmi:

“Zanzibar yagundua mafuta Darajani; uzalishaji waanza chini ya daraja la Sultan!”

Hili si jambo la kuchekesha pekee. Ni aibu kwa taasisi za umma kutokuwa na kumbukumbu za historia ya eneo maarufu kiasi hiki. Daraja hilo linaweza kuwa sehemu muhimu ya urithi wetu na ushahidi wa namna Stone Town ilivyokuwa imetenganishwa na Ngambo kabla ya kufanyika reclamation.

Tusije tukaliharakia kulifukia tena kabla halijachunguzwa na kuhifadhiwa kihistoria halafu vizazi vijavyo vikaja kuligundua kwa mara ya tatu na kutangaza kuwa vimepata gesi! 😂

Credit: Abuu Shani Ally Saleh Farid Himid Omar Said ShaabanView attachment 3652322View attachment 3652323View attachment 3652324
Hureeeeeeeeey. Basi sasa wauvunje tu huo muungano wao haramu
 
Back
Top Bottom