Huna kazi unang'ang'ania nini kukaa Dar?

Huna kazi unang'ang'ania nini kukaa Dar?

mathabane

JF-Expert Member
Joined
Jan 27, 2013
Posts
2,405
Reaction score
1,900
Najua wengi mtakasirika lakini potelea mbali.

Unakuta jitu zima halina shughuli yoyote ya kujiingizia kipato, nguvu linazo lakini linang'ang'ania kukaa kwenye mji wa pesa kama Dar bila kuona aibu matokeo yake ni kujiingiza katika vitendo vya kiuhalifu.

Kazi kuamka asubuhi na kutunisha makalio na makende wakati fursa za kilimo na mapori tele nje ya Dar.

Mijitu kula shida, kulala shida na bado mnajilundika mijini kwa kutegemea ujambazi, uporaji, umalaya na uuzaji wa gongo.

We kazi huna alafu unapenda maisha ya starehe ndio maana wengi wenu mnatumbukia kwenye uhalifu kwa sababu hamuwezi fikiria.
Mnaishi maisha ya dhiki, maisha chini ya robo dola lakini hamjitambui maana mmefunga akili zenu katika mitungi ya ulumbukeni.

Kwa kuendekeza uzinzi, ulevi, uvivu, starehe na anasa na kutopenda kufunguka kiakili, sishangai kama mtu na kizazi chake wote wakawa vibaka/malaya tangu mtoto mpaka babu/bibi.

Yaani jitu linaishi mjini kwa kutunisha makende/makalio? Huu ni upumbavu wa hali ya juu.

Nawashauri tokeni Dar mrudi mikoani mkalime na kuzalisha mazao muondokane na umasikini na laana mnazopata mkiwa Dar bila sababu. Kwani maisha ni Dar tu? Nani kawarioga nyie?

RC Makonda nadhani ile ahadi yako ya kuwakamata na kuwaswaga majitu ya namna hii umewadia.
 
Usitake kudanganya wenzako, King of All Social Networks alivyorudi kwanini hakwenda Dodoma kulima zabibu au Tukuyu kulima ndizi ingawa alikuwa na $500 mfukoni sasa hivi ni King of All Social Networks pia Director and CEO wa Swahili TV. Mjini kuna fursa bwana.
 
Mjini dar kuzuri hasikudanganye mtu,
Ukitaka kujua mjini pazuri muulize Maja.li.wa kwa nini muda mwingi yupo dar
Watu wameondoka chato, wamehamia dar
Dar sio mji wa ki sport sport.
 
Mleta mada ulikuwa na wazo zuri tu lakini umetumia maneno yasiyo ya kiuungwana ...kiukweli umewatusi hao uliowakusudia.

Kwa hali hiyo ujumbe wako unaweza ukawa opposite na lengo lako kivitendo.

'Kazi ya limao haiwezi kufanywa na chungwa'
 
Usitake kudanganya wenzako, King of All Social Networks alivyorudi kwanini hakwenda Dodoma kulima zabibu au Tukuyu kulima ndizi ingawa alikuwa na $500 mfukoni sasa hivi ni King of All Social Networks pia Director and CEO wa Swahili TV. Mjini kuna fursa bwana.
Tatizo umemsoma mleta mada upande mmoja tu, yeye amewalenga wasiokua na kazi maalum na kila siku wao wapo wapo tu mjini,

Unakuta mtu analala na njaa ili mradi tu na yeye yupo Dar wakati huko kijijini kwao kaacha mashamba na wazazi wazee wenye kuhitaji msaada wake.
 
Kazi maalumu unamaanisha zile za kuvaa tai na kulipwa kila mwezi au hata hizi za vibarua? Hivi watu wa Dar wakiwa na kazi nani atasaidia kuzoa taka? Nani atasaidia vishughuli vinavyoibuka vya hapa na pale ambavyo havitokezi kila siku? Nani atachimba mashimo ya choo? Kumbuka wajenzi nao ni watu wasio na kazi wanasubiri wewe mwajira unaolipwa mshahara ujenge na wao wapate ajira sasa wasipokuwepo nani atajenga? Ulisoma kitabu cha economic thinkers form 3 kilizungumzia Specialization jaribu kusoma tena elimu ya form three hiyo.
 
kila mtu ananafasi yake katika jamii .. wasipokuwepo hao watunisha makalio wahalifu kuna sekta zitadhurika .. huwa tunategemeana na ndiyo maana ya jamii
 
Mbona vijana wa hiyo mikoa mingine kila siku wanatafuta nauli za kwenda Dar, washauri lingine sio hilo, serikari yenyewe imeshindwa kuhamia mkoani eti mpaka 2020.
 
Mbona vijana wa hiyo mikoa mingine kila siku wanatafuta nauli za kwenda Dar, washauri lingine sio hilo, serikari yenyewe imeshindwa kuhamia mkoani eti mpaka 2020.

Thubutu hata hio 2020 hakuna atakayehama dar,
Magu akipata tena kuongoza ataimaliza awamu yake ya pili ndani ya jiji la makondakta.
 
Kuna haka kamsemo eti rudi kijijini ukalime acheni kukalili zama zimebadirika unaweza ukakuta huyo unaemwambia arudi kijiji hana hata sehemu ya kulima na yawezekana hata huko kijijini ardhi haina rutuba wala mvua hainyeshi kwa wakati sasa huwa naangalia mawazo ya watu juu ya kufikiri kwa ufupi naona wamekaririshwa kwamba kama huna kazi nenda kijijini kalime,
Huwa nacheka sana kisha naanza ku image jinsi atavyofika na kuanza kulima.

Bila shaka mtoa mada utakuwa la nne B hujakomaa kiakili, na ninahisi huna Elimu ya kutosha na kama unayo una elimu ya kwenye daftari sio ya kuelimisha na kujitambua,
Akili yako kama ya makonda inabidi wamikoani waje dar kwa sababu maalumu.
 
Kuna haka kamsemo eti rudi kijijini ukalime acheni kukalili zama zimebadirika unaweza ukakuta huyo unaemwambia arudi kijiji hana hata sehemu ya kulima na yawezekana hata huko kijijini ardhi haina rutuba wala mvua hainyeshi kwa wakati sasa huwa naangalia mawazo ya watu juu ya kufikiri kwa ufupi naona wamekaririshwa kwamba kama huna kazi nenda kijijini kalime,
Huwa nacheka sana kisha naanza ku image jinsi atavyofika na kuanza kulima.

Bila shaka mtoa mada utakuwa la nne B hujakomaa kiakili, na ninahisi huna Elimu ya kutosha na kama unayo una elimu ya kwenye daftari sio ya kuelimisha na kujitambua,
Akili yako kama ya makonda inabidi wamikoani waje dar kwa sababu maalumu.
Unaaamka asubuhi huna na hujui cha kufanya,hujui utalala, kula wapi na nini, mvua ikinyesha, jua liliwaka we upo mjini tu unashinda na kulala njaa huna pa kuanzia! Na bado umekariri eti ni afadhali kuishi maisha hayo. Huwezi kuwa sawa kichwani. Unakariri kwamba maisha yapo Dar! Matokeo yake udhalilishwe mwili na wenye pesa ili uweze kuishi
 
Ni mkoa gani wanatakiwa kuishi watu wasio na kazi?
 
Back
Top Bottom