Huna kazi unang'ang'ania nini kukaa Dar?

Huna kazi unang'ang'ania nini kukaa Dar?

Unaaamka asubuhi huna na hujui cha kufanya,hujui utalala, kula wapi na nini, mvua ikinyesha, jua liliwaka we upo mjini tu unashinda na kulala njaa huna pa kuanzia! Na bado umekariri eti ni afadhali kuishi maisha hayo. Huwezi kuwa sawa kichwani. Unakariri kwamba maisha yapo Dar! Matokeo yake udhalilishwe mwili na wenye pesa ili uweze kuishi
Kwa matatizo hayo ndipo tutakapopata uwezo halisi wa mwanadamu kufikiri. Kumbuka kuwa sisi tunaishi kusurvive na sio kuzifurahisha nafsi zetu. Huyu ambaye yupo dar hana kazi leo, miaka mitano ndiye atakayekuja kijijini kwenu kuangusha mjengo wa maana ambao mtakua mkipita hapo mnaushangaa.
Kama hujui ni kwamba akili ni bora kuliko mali. Tafakar hii kauli yangu
 
Alichosema mleta ndio ukweli ingawa ni mchungu, na wengi wetu hatupo tayari kusema ukweli huo. Ardhi lukuki Bonde la Mto Ruvu, Mto Rufiki, kuna skimu za Umwagiliaji nyingi sana katika Mabonde ya Pangani, Rufiji, Mbalali, Ziwa Tanganyika, ziwa Victoria, Ziwa Rukwa nk nk maji yapo kwa kipindi chote cha Mwaka. Mazao ya Mbogamboga, Nafaka, Maua nk yanastawi vizuri kabisa. Badala yake tumebaki watu wa kulalamika tu
 
Usitake kudanganya wenzako, King of All Social Networks alivyorudi kwanini hakwenda Dodoma kulima zabibu au Tukuyu kulima ndizi ingawa alikuwa na $500 mfukoni sasa hivi ni King of All Social Networks pia Director and CEO wa Swahili TV. Mjini kuna fursa bwana.

And billionaire
 
Mtu kama huyo anasubiri gari la mwisho kwenda dodoma litakalokua limebeba vitu vya serikali pindi wanahamia dodoma
Najua wengi mtakasirika lakini potelea mbali.

Unakuta jitu zima halina shughuli yoyote ya kujiingizia kipato, nguvu linazo lakini linang'ang'ania kukaa kwenye mji wa pesa kama Dar bila kuona aibu matokeo yake ni kujiingiza katika vitendo vya kiuhalifu.

Kazi kuamka asubuhi na kutunisha makalio na makende wakati fursa za kilimo na mapori tele nje ya Dar.

Mijitu kula shida, kulala shida na bado mnajilundika mijini kwa kutegemea ujambazi, uporaji, umalaya na uuzaji wa gongo.

We kazi huna alafu unapenda maisha ya starehe ndio maana wengi wenu mnatumbukia kwenye uhalifu kwa sababu hamuwezi fikiria.
Mnaishi maisha ya dhiki, maisha chini ya robo dola lakini hamjitambui maana mmefunga akili zenu katika mitungi ya ulumbukeni.

Kwa kuendekeza uzinzi, ulevi, uvivu, starehe na anasa na kutopenda kufunguka kiakili, sishangai kama mtu na kizazi chake wote wakawa vibaka/malaya tangu mtoto mpaka babu/bibi.

Yaani jitu linaishi mjini kwa kutunisha makende/makalio? Huu ni upumbavu wa hali ya juu.

Nawashauri tokeni Dar mrudi mikoani mkalime na kuzalisha mazao muondokane na umasikini na laana mnazopata mkiwa Dar bila sababu. Kwani maisha ni Dar tu? Nani kawarioga nyie?

RC Makonda nadhani ile ahadi yako ya kuwakamata na kuwaswaga majitu ya namna hii umewadia.
 
Usitake kudanganya wenzako, King of All Social Networks alivyorudi kwanini hakwenda Dodoma kulima zabibu au Tukuyu kulima ndizi ingawa alikuwa na $500 mfukoni sasa hivi ni King of All Social Networks pia Director and CEO wa Swahili TV. Mjini kuna fursa bwana.
Samahan mkuu huyo mtu unaemtaja ni na Kwa jina??? Mie simjui labda naweza kua namjua Kwa namna nyingine.
 
Kwa matatizo hayo ndipo tutakapopata uwezo halisi wa mwanadamu kufikiri. Kumbuka kuwa sisi tunaishi kusurvive na sio kuzifurahisha nafsi zetu. Huyu ambaye yupo dar hana kazi leo, miaka mitano ndiye atakayekuja kijijini kwenu kuangusha mjengo wa maana ambao mtakua mkipita hapo mnaushangaa.
Kama hujui ni kwamba akili ni bora kuliko mali. Tafakar hii kauli yangu
Nyie ndio mnategemea social evils mpate mali. Hizo sio akili ndugu. Upate mali kwa kumwaga damu zawatanzania wasio na hatia.
Tatizo kubwa ni akili mgando na uvivu wa kufikiri. Tamaa za kupata utajiri wa ghafla bila kutoa jasho.
Mnapenda kula,utajiri hampendi kazi. Wavivu!
 
***
Ndg Otorong'ong'o ebu tupe sababu za kuchukia kwako.../ maana yaonekana kama ndg mwandishi amekugusa kwelikweli.../
Ndugu! Maisha hayana formula au kanuni kwamba nikifuata Formula fulani ndio nitafanikiwa...Ingekuwa ni hivyo hakika ningenunua formula aliyotumia Mzee Mengi kuwa tajiri...

Vijana wadogo wa Kichagga wanakimbia huko Moshi na kuja mijini Arusha na Dar na wanafanikiwa. Leo Kariako ni vijana wadogo wamemkimbiza Muhindi Kkoo na kushika hatamu..Hao wote wamekimbia mashamba huko Moshi na kuja mjini...

Kila mtu ana malengo yake ya kufanikiwa iwe kwa hila au kwa haki....

Ndio maana nikamuita mnafiki...Halafu umeshagundua kitu, hawa watu wanao shauri watu wajiajiri wasitegee ajira za kuajiriwa wao wenye wako kwenye pay roll ya ajira ila ni mabingwa wa kushauri watu wajiajiri...huu ni unafiki wa kiwango cha juu sana....
 
Ndugu! Maisha hayana formula au kanuni kwamba nikifuata Formula fulani ndio nitafanikiwa...Ingekuwa ni hivyo hakika ningenunua formula aliyotumia Mzee Mengi kuwa tajiri...

Vijana wadogo wa Kichagga wanakimbia huko Moshi na kuja mijini Arusha na Dar na wanafanikiwa. Leo Kariako ni vijana wadogo wamemkimbiza Muhindi Kkoo na kushika hatamu..Hao wote wamekimbia mashamba huko Moshi na kuja mjini...

Kila mtu ana malengo yake ya kufanikiwa iwe kwa hila au kwa haki....

Ndio maana nikamuita mnafiki...Halafu umeshagundua kitu, hawa watu wanao shauri watu wajiajiri wasitegee ajira za kuajiriwa wao wenye wako kwenye pay roll ya ajira ila ni mabingwa wa kushauri watu wajiajiri...huu ni unafiki wa kiwango cha juu sana....
Ndugu naona unapindisha ukweli. Labda na wewe ni miongoni mwao, mnaokariri kwamba kupata maisha lazima uishi dar hata kwa kudhalilika ubinadamu wako au kutoa uhai wa wengine ili upate wewe. Mzizi wake ni uvivu na mgando wa kufikiri. Hao wachaga na wakinga wa kariakoo achana nao hao wakitoka vijijini kwao kuja dar huja kwa malengo ya kutimiza tofauti na vijana wengi mnasubiri kukaba watu n kuuza miili na umri unakwenda.
Ndo maana utakuta mtu mzima haaminiki yaani hata wazee wa huko ni ujanjanujanja tu.
 
Ndugu naona unapindisha ukweli. Labda na wewe ni miongoni mwao, mnaokariri kwamba kupata maisha lazima uishi dar
Aliyekuambia maisha yana Formula ni nani..?

hata kwa kudhalilika ubinadamu wako au kutoa uhai wa wengine ili upate wewe
Kwanini unafikiri kufanikiwa ni lazima udhalilishe ubinadamu wako na kutoa uhai wa wengine..?? Vipi ulikuwa subjected kwenye such environment..?

Mzizi wake ni uvivu na umgando wa akili.
Una uhakika na hiki ulichoandika...?

Hao wachaga na wakinga wa kariakoo achana nao hao wakitoka vijijini kwao kuja dar huja kwa malengo ya kutimiza tofauti na vijana wengi mnasubiri kukaba watu n kuuza miili na umri unakwenda.
Samahani labda sijajua, hii mada yako imelenga watu au vijana wa kundi gani hasa.....???

Ndo maana utakuta mtu mzima haaminiki yaani hata wazee wa huko ni ujanjanujanja tu.
Una exposure ndogo sana...Pole lakini...
 
Alichosema mleta ndio ukweli ingawa ni mchungu, na wengi wetu hatupo tayari kusema ukweli huo. Ardhi lukuki Bonde la Mto Ruvu, Mto Rufiki, kuna skimu za Umwagiliaji nyingi sana katika Mabonde ya Pangani, Rufiji, Mbalali, Ziwa Tanganyika, ziwa Victoria, Ziwa Rukwa nk nk maji yapo kwa kipindi chote cha Mwaka. Mazao ya Mbogamboga, Nafaka, Maua nk yanastawi vizuri kabisa. Badala yake tumebaki watu wa kulalamika tu
Najua unasema tu ila kumbuka Leo unacho kesho huna,na pia si kila anae kuja Dar anakuja ila azunguke mtaani
 
Nyie ndio mnategemea social evils mpate mali. Hizo sio akili ndugu. Upate mali kwa kumwaga damu zawatanzania wasio na hatia.
Tatizo kubwa ni akili mgando na uvivu wa kufikiri. Tamaa za kupata utajiri wa ghafla bila kutoa jasho.
Mnapenda kula,utajiri hampendi kazi. Wavivu!
Sasa anayefikiri utajir kati yangu mm na huyo anayetaka watu wakalime chakula ni nani?
Think twice kabla hujavamia quote zangu
 
Back
Top Bottom