babalao 2
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 5,425
- 3,300
HUMPHREY POLEPOLE:Salamu zangu
za Mwisho wa Wiki kwenu:
1. Nilipata fursa ya kuwapitisha wanachama 180 wa Jukwaa la Katiba katika Rasimu ya Katiba Toleo la Pili. Nikazungumza nao pia juu ya wajibu wa Asasi za Kiraia kudai mchakato huu ukamilike kwa mafanikio kama ilivyokusudiwa na waliopewa dhamana wakati huu kuheshimu maoni ya wananchi. Nchi hii ni zaidi sana ya maslahi yetu binafsi na makundi
2. Nimemaliza kuandika Makala yangu itakayotoka Gazeti la Mwananchi Jumapili Agosti 17. Jumapili hii nimezungumzia juu ya Uraia Pacha, nimeeleza changamoto zake na nimeweka suluhisho linalopendekezwa na Rasimu ya Katiba.
3. Nimepokea Mualiko kutoka Gazeti la Rai linalotoka kila Alhamisi kwamba niwe natoa Maarifa huko uandishi wa Makala. Nimekubali. Na sasa mtaanza kunisoma katika gazeti la Rai kuanzia wiki ijayo Alhamisi Agosti 21.
4. Nitawajulisha hivi punde vipindi vya Televisheni nitakavyokuwa nikitoa elimu kwa umma wiki ijayo ili twende pamoja. Niwatakie Mapumziko mema ya Wikendi. Usisahau kusoma magazeti, kusikiliza redio na kuangalia Televisheni ili uendelee kupata ufahamu wa nini kinaendelea katika Mchakato wa Katiba Mpya. Hatma ya kupatikana kwa Katiba Mpya iko Mikononi Mwako.
Asante na Tafakari