Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Balozi aliyejiuzulu, Humphrey Polepole, akizungumza kwa njia ya mtandao, Septemba 18, 2025, amesema amesikia kuhusu kuitwa na Jeshi la Polisi lakini bado kuna tatizo Serikalini kwa sababu walipaswa kuihoji Serikali kwanini haijanirejesha nchini baada ya mimi kuondolewa kazini.
Amesema hata alipoajaribu kuuliza watumishi wenzake kuhusu utaratibu wa kurejea nchini kwa Watumishi wanaofanya kazi nje, aliambiwa Rais Samia ameelekeza afukuzwa kazi na stahiki zake zote asipewe.
Amehoji inakuwaje Serikali iliyomtelekeza Cuba inamtaka afike Polisi wakati haikumrejesha nyumbani ikiwa hiyo ni Haki ya Mtumishi.
Vilevile, ameshauri Jeshi la Polisi kufanyia kazi hoja zake badala ya kumtafuta yeye.
Amesema hata alipoajaribu kuuliza watumishi wenzake kuhusu utaratibu wa kurejea nchini kwa Watumishi wanaofanya kazi nje, aliambiwa Rais Samia ameelekeza afukuzwa kazi na stahiki zake zote asipewe.
Amehoji inakuwaje Serikali iliyomtelekeza Cuba inamtaka afike Polisi wakati haikumrejesha nyumbani ikiwa hiyo ni Haki ya Mtumishi.
Vilevile, ameshauri Jeshi la Polisi kufanyia kazi hoja zake badala ya kumtafuta yeye.