MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,006
- 2,166
"When you cut out the tongue of a man, you’re not convincing the world he’s a liar. You’re only telling the world you fear of what he might say".POLEPOLE KUWA BALOZI NI PROMOTION LAKINI........
Na Elius Ndabila
0768239284
Leo Mhe Rais amemteua Mhe Humphrey Polepole kwenda kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi. Ikumbukwe kuwa Mhe Polepole Kwa siku za hivi karibuni alikuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya awamu ya sita Kwa alichokiita shule ya uongozi.
Baada ya uteuzi wake kuna mijada inakuja kuwa je Mhe Polepole amepata Demotion au Promotion? Jibu ni Promotion.
Hadhi ya Ubalozi ni kubwa kuliko Ubunge. Ubalozi ni nchi ndani ya nchi nyingine. Hivyo unapokuwa Balozi ni sawa na kuwa wewe ni Mkuu wa nchi kwenye nchi nyingine. Kuwa Balozi kunakupa immunity/ Kinga nyingi kuliko Ubunge. Balozi hata begi lake tu haliruhusiwi kuguswa na mtu yeyote. Kwa tafsiri isiyo rasmi Polepole anaenda kuwa Rais wa Tanzania ndani ya Malawi. Maswala yote yanayohusiana na Diplomasia nchini Malawi yeye ndiye atakuwa kilanja mkuu.
Lakini.......Mhe Polepole amezoea kuongea. Kama atafika Malawi atajisahau akaanza kuongea aliyokuwa anaongea huku basi nafasi yake inaweza kuwa DEMOTION. Inaweza kuwa demotion Kwa kuwa anaweza kuondolewa. Lakini kama atakuwa mtiifu basi hii ni Promotion.
Tafakari