Kakke
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 1,883
- 1,482
Sifieni kama kuna mambo ya kusifia na onyeni kama kuna mambo ya kuonya lakini hekima busara kwa sababu kauli hiyo ni kauli ya moto inaweza ikatujenga inaweza ikatubomoa.Kuna namna nyingi za kurekebisha, tusije tukageuza na kujadiliana na Maaskofu, Askofu anasema tunamjibu, tutakuwa tunamkosea Mungu.
Mimi sitaki kusema Maaskofu wamekosea au hawajakosea lakini nataka kusema haya majadiliano ukiyaangalia yanatokea wapi? Tusije tukaingia kwenye mtego wa Ibilisi tukajikuta tukimtizama askofu fulani tunaona chama fulani. Askofu unaonekana kama chama fulani, mfano mimi ni mwanaccm nina dhambi zangu nataka kuja kuungama kwako, ntaungamaje kwako wakati wewe una itikadi tofauti na mimi?
Chama chetu kinaamini binadamu wote ni sawa, kinaamini katika utu, kinaamini katika kujitegemea, kinaamini katika heshima ya watu, kinaamini katika kusema kweli, kinaamini katika vita dhidi ya rushwa, kinaamini katika umoja kinaamini katika kujitoa, kinaamini katika kazi ni kipimo cha utu.
Sasa nikikutizama wewe unaamini katika ubwanyenye, unamini katika kuhodhi mali, unaamini katika umangimeza, unaamini katika mimi ni mwenyekiti peke yangu na hakuna mwingine. Sasa utaanza kunipoteza.
Mimi sitaki kusema Maaskofu wamekosea au hawajakosea lakini nataka kusema haya majadiliano ukiyaangalia yanatokea wapi? Tusije tukaingia kwenye mtego wa Ibilisi tukajikuta tukimtizama askofu fulani tunaona chama fulani. Askofu unaonekana kama chama fulani, mfano mimi ni mwanaccm nina dhambi zangu nataka kuja kuungama kwako, ntaungamaje kwako wakati wewe una itikadi tofauti na mimi?
Chama chetu kinaamini binadamu wote ni sawa, kinaamini katika utu, kinaamini katika kujitegemea, kinaamini katika heshima ya watu, kinaamini katika kusema kweli, kinaamini katika vita dhidi ya rushwa, kinaamini katika umoja kinaamini katika kujitoa, kinaamini katika kazi ni kipimo cha utu.
Sasa nikikutizama wewe unaamini katika ubwanyenye, unamini katika kuhodhi mali, unaamini katika umangimeza, unaamini katika mimi ni mwenyekiti peke yangu na hakuna mwingine. Sasa utaanza kunipoteza.