naamini pole pole ni mmoja wa vijana wanaojielewa sana. ni mmoja wa watu wanaoamini matatizo hayakimbiwi bali ni kushindana nayo kuyashinda.
kuhama chama sio suluhisho, kama nyumba chafu na ni yako pambana kuisafisha na fanya kila juhudi ili iwe safi. mtu mpambanaji husifiwa kwa kutengeneza na sio kuhamia kwenye nyumba zilizojengwa na wengine.
sizani kama yy anataka nafasi yyte ila anasimamia misingi ya chama ambacho kiukweli ccm ukilinganisha na vyama vilivyopo ndio chama pekee kilicho na muundo mzuri na uwazi.
ccm kimejengwa kiwe chama cha wote. ila ttz kuna watu wanaharibu chama, wamekipora na nnafananisha na watu waliotupa taka kwenye jengo takatifu. sasa kwa wenye kulipenda hawalikimbii ila watapambana na wachafuzi ama kuwashawish waache vitendo vyao na kulisafisha jengo kwa pamoja au kuwafukuza na kuwatupa nje au wawafukuze walio wasafi. kwa hio pole pole labda afukuzwe kinyume chake atapambana kuleta usafi ndani ya chama