"HUMAN ZOOs" biashara ya fedheha kwa waafrika

nessonlegend

JF-Expert Member
Mar 1, 2013
1,698
1,508
“HUMAN ZOO” - Historia iliyosahaulika
Hakuna mwalimu mzuri kama historia, kwa kadiri unavyozidi kuitafuta ndivyo unavyopata fursa ya kufahamu mambo mengi. Katika shule zetu kwa kiasi kikubwa tumefundishwa historia ya ukoloni barani Afrika, lakini hakuna mahali tulipofundishwa namna ukoloni huu ulivyoendana na biashara ya “MAONYESHO YA BINADAMU
Human zoo” ni biashara iliyoanza katika kipindi cha karne ya 16-20 mwanzoni (kwa mijibu wa vyanzo mbalimbali) ni biashara ambayo binadamu kutoka Afrika, walikuwa wakiwekwa katika majumba, vijiji, au katika maeneo mengine yaliyotengwa kwa lengo la kuonyeshwa kama bidhaa nyingine katika maonyesho ya (saba saba au nane nane). Biashara hii ilianza kukua kwa kasi hususani karne ya 17 yaani miaka ya 1600s ambapo wazungu wengii walikuwa wakituma wafanyabiashara Afrika kuja kununua watu kwa ajili ya maonyesho hayo. Pamoja na kwamba ilikuwa ni ukatiri mkubwa kwa wa afrika ila kwao ilikuwa ni kivutio cha maana sana kwani kwa kadiri muda ulivyokuwa unakwenda ndivyo watazamaji walikuwa wakiongezeka toka sehemu mbalimbali kushuhudia asili ya mtu mweusi.
Katika biashara hii wa afrika walikuwa wakifanyiwa maonyesho ama wakiwa watupu (uchi) au nusu uchi (kwa kufunika sehemu za sili), katika maonyesho haya yaligawanyika katika makundi tofauti tofauti ambapo kuna waliokuwa wakionyeshwa kama familia nzima, au mtu mmoja mmoja ambapo alikuwa akionyeshwa uwezo wake, ukatili wake na mambo mengine kama hayo,watu wafupi (dwarf), pia walionyeshwa watoto wakiume na wakike ambapo walikuwa wakipewa ndizi kama vile tuendavyo kuangalia nyani au sokwe. Ni ukatili mkubwa japo kwao ni furaha iliyoje.
Moja kati ya stori ya kusisimua ni ya Ota Benga huyu alikuwa ni mwafrika aliyenunuliwa na mmishonari na mgunduzi Dr Samuel Philips Verner na kupelekwa USA mnamo mwaka 1904, inasemekana Verner alimleta Benga akiwa na watu wengine saba na kijana mdogo toka Kongo ambao walinunuliwa toka kwa mfanyabiashara wa watumwa ambapo familia ya Benga yani mke na watoto wake waliuliwa katika mauaji ya halaiki (massacre). Historia inasema kwamba, ujio wa Benga na wenzake ulikuwa kivutio kikubwa kwani katika kipindi hiki biashara ya utumwa ilikuwa imefifia sana na hivyo maonyesho yaliyodumu kwa muda wa miaka 400 yalikuwa yamepoteza mvuto kwa kukosa bidhaa (binadamu). Kundi la Benga na wenzake walikuwa wakisafirishwa kimaonyesho kwenda sehemu mbalimbali ikiwemo toka St louis, New orleans, Mardi glas na kisha kufika mpaka Afrika. Katika kuzunguka kote huku inasemekana Benga alionyesha juhudi ya kutaka kujua kusoma na kujifunza mambo ambapo alikuwa akimuomba Verner kumrejesha nyumbani Afrika.
Mnamo mwezi wa nane mwaka 1906 Verner na Benga walifanikiwa kufika New York, ambapo Verner alikuwa akitafuta sehemu ya kumuweka Benga ili aishi huko. Hatimaye akafanikiwa kumpeleka katika Bronxy zoo ambapo mwanzoni alikuwa akitembea tembea na kuwasaidia wafanyakazi wa zoo hiyo. Lakini mwanzoni mwa mwezi wa tisa mwaka huo huo ikaamuliwa Benga apelekwe katika Orang Utan cage ambapo alikuwa akihamasishwa kucheza na jamii hiyo ya Orang utan na kufuma kofia pamoja na kuchezea mshale na upinde. Cage hii ilikuwa ikisimamiwa na Madison Glant huyu alikuwa ni New York Zoologist. (Masimulizi haya yapo katika kitabu cha Ota Benga, The Pygy in the zoo, kilichoandikwa na mjukuu wa Verner, Philips Bradford)
Pamoja na kuwepo kwa ukatili wa binadamu hususani asili ya watu weusi uliokuwa ukifanywa na wamishionari, lakini pia kulikuwa na kundi la watu waliokuwa wakipinga biashara ya maonyesho ya binadamu kama iliyokuwa kwa biashara ya utumwa. Dr Robert Stuart MacArthur of the Calvary Baptist Church in New York was outraged and was quoted in The New York Times on Sept. 10, 1906 as saying, ‘The person responsible for this exhibition degrades himself as much as he does the African. Instead of making a beast of this little fellow, he should be put in school for the development of such powers as God gave to him. It is too bad that there is not some society like the Society for the Prevention of Cruelty to Children. We send our missionaries to Africa to Christianise the people, and then we bring one here to brutalise him.
“Mtu anayejihusisha na maonyesho haya, anajishusha yeye mwenyewe kama vile anavyowafanyia wa afrika, badala ya kumfanyia mambo hayo ilitakiwa tumpeleke shule akajifunze kwa kadili ya uwezo wao waliopewa na Mungu, ni jambo baya sana kwa jamii inayopinga unyanyasaji na ukatili kwa watoto, iliyotuma wamishonari Afrika kwenda kuhubili, kisha kuja na watu haohao na kuwafanyia ukatili” (tafsiri hii ya kimaana ni yangu).
Haya ni maneno yaliyotolewa na kasisi aliyekuwa ana asili ya Afrika-Amerika. ‘Our race, we think, is depressed enough without exhibiting one of us with the apes,’ wrote one such minister, James H. Gordon to the mayor of New York. ‘We think we are worthy of being considered human beings, with souls.’ Gordon was to become Ota Benga’s guardian after the zoo ultimately bowed to public pressure and had Benga removed.
Baada ya Benga kuwa chini ya usimamizi wa Gordon, alihamishiwa katika makazi yaliyojulikana kama Howard Colored Orphan Asaylum yaliyokuwa yamefadhiriwa na kanisa. Mnamo january 1910 Gordon akamfanyia Benga mpago wa kwenda Lynchburg, Virginia. Wakati huu Benga alikuwa akizungumza kiingereza kwa ufasaha huku akiwa anavalia mavazi ya kimarekani, baada ya kufika Virginia na hatimaye akaanza kufanya kazi katika kiwanda cha Tumbaku cha Lynchburgy. Pamoja na kwamba alikuwa na umbo dogo kuliko wafanyakazi wengine, alijidhihirisha kuwa ni wa kipekee hasa katika kupanda juu ya poles kufuata tumbaku bila ya kutumia ngazi, wenzake wakaanza kumwita Bingo. Alijihusisha na kusimulia historia ya maisha yake na alikuwa akipewa bia na watu kama shukrani ya simulizi yake. Katika kipindi hiki alikuwa na plani ya kurudi nyumbani Congo, lakini baada ya kutokea kwa vita ya kwanza ya dunia ndoto yake ikawa imefifia kwa kiasi kikubwa. Mnamo tarehe 20-3-1916 Benga akiwa na umri wa miaka 32 aliamua kukatisha uhai wake kwa kutumia bastola (pisto) aliyokuwa ameiba, kwa kujilipua upande wa moyo wake so sad kwa kweli. Cheti chake cha kifo kimeandikwa OTTO BINGO.

Human_Zoos_or_Ethnic_Show.jpg
Maonyesho yaliyofanywa na Jesuits huko hispania barcelona 1929

Human_Zoos_or_Ethnic_Shows guinean woman first colonial porguese exbition 1934.jpg
Picha ya Roshina, mwanamke toka Guinea “malkia wa kwanza” wa maonyesho ya kireno huko Oporto mwaka 1934

Human_Zoos_or_Ethnic_Shows.jpg
Maonyesho ya kikoloni huko paris 1906

issue2_brown human zoo mchoro wa saartje baartman british museum.jpg
Mchoro wa saartije baartman huko makumbusho ya uingereza

1.jpg
Watot waliokuwa wakihifadhiwa kwa maonyesho hapo akipewa ndizi na watazamaji

2.jpg
Namna ambavyo walikuwa wakifanyiwa waafrika wenzetu.
Historia ni ndefu sana waweza kujiongeza kwa kutafuta maarifa zaidi kwa ku-google HUMAN ZOO
 
M
Unazidi kunifungua na kunidhihirishia kuwa mzungu ni mbaya kuliko mwarabu. Ila amemzidi mwarabu ujanja wa kuficha ubaya wake na kuonesha ubaya wa mwenzake kwa waafrika mpaka leo tumekariri waarabu ni wabaya.
Mzungu hana maana hata kidogo, jaribu kujiuliza hao watumwa walikuwa wanaenda kufanya kazi wapi? Km sio ulaya wazungu wao walikuwa hawanunui watumwa Moja Kwa Moja maana walijua baadae mambo yakija kubumburuka Dunia itawalaumu, na ndio wakaamua kuwasakizia waarabu ambao mpaka Leo tunasoma ubaya wao, wazungu wakiwa wametulia tulii,
 
M

Mzungu hana maana hata kidogo, jaribu kujiuliza hao watumwa walikuwa wanaenda kufanya kazi wapi? Km sio ulaya wazungu wao walikuwa hawanunui watumwa Moja Kwa Moja maana walijua baadae mambo yakija kubumburuka Dunia itawalaumu, na ndio wakaamua kuwasakizia waarabu ambao mpaka Leo tunasoma ubaya wao, wazungu wakiwa wametulia tulii,
Mpaka kesho,mzungu ni mbaya kwetu kuliko hata mwarabu. Ukiangalia matendo ya ubaguzi wa rangi,kufananishwa waafrika na sokwe bado yapo na yameshamiri ulaya. Hakuna ubaguzi mkubwa kama ule wa kumtupia mwafrika ndizi. Lakini matukio haya hatuyaoni yakitokea kwa waarabu.
 
Unazidi kunifungua na kunidhihirishia kuwa mzungu ni mbaya kuliko mwarabu. Ila amemzidi mwarabu ujanja wa kuficha ubaya wake na kuonesha ubaya wa mwenzake kwa waafrika mpaka leo tumekariri waarabu ni wabaya.
na kuna waAfrika ambao wanadhani mzungu atawakomboa
 
Kwa wale wanaofikiria waarabu ni wakatiri kuliko wazungu wajiulize swali hili. Je wazungu wameua watu wangapi ukilinganisha na waarabu katika historia ?
Halafu tujiulize, mbona unyama mkubwa ambao binadamu hasa mwafrika amekwisha mfanyia binadamu mwenzake umefanywa na wazungu wa kristo pamoja na waarabu waislamu na si watu wanaofuata dini sa asili kama za kwetu?
Kama dini zetu kweli zilikuwa za kishenzi mbona hatukuwafanyia wanadamu wengine ubaya kama waliotufanyia wa kristu na waislamu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
“HUMAN ZOO” - Historia iliyosahaulika
Hakuna mwalimu mzuri kama historia, kwa kadiri unavyozidi kuitafuta ndivyo unavyopata fursa ya kufahamu mambo mengi. Katika shule zetu kwa kiasi kikubwa tumefundishwa historia ya ukoloni barani Afrika, lakini hakuna mahali tulipofundishwa namna ukoloni huu ulivyoendana na biashara ya “MAONYESHO YA BINADAMU
Human zoo” ni biashara iliyoanza katika kipindi cha karne ya 16-20 mwanzoni (kwa mijibu wa vyanzo mbalimbali) ni biashara ambayo binadamu kutoka Afrika, walikuwa wakiwekwa katika majumba, vijiji, au katika maeneo mengine yaliyotengwa kwa lengo la kuonyeshwa kama bidhaa nyingine katika maonyesho ya (saba saba au nane nane). Biashara hii ilianza kukua kwa kasi hususani karne ya 17 yaani miaka ya 1600s ambapo wazungu wengii walikuwa wakituma wafanyabiashara Afrika kuja kununua watu kwa ajili ya maonyesho hayo. Pamoja na kwamba ilikuwa ni ukatiri mkubwa kwa wa afrika ila kwao ilikuwa ni kivutio cha maana sana kwani kwa kadiri muda ulivyokuwa unakwenda ndivyo watazamaji walikuwa wakiongezeka toka sehemu mbalimbali kushuhudia asili ya mtu mweusi.
Katika biashara hii wa afrika walikuwa wakifanyiwa maonyesho ama wakiwa watupu (uchi) au nusu uchi (kwa kufunika sehemu za sili), katika maonyesho haya yaligawanyika katika makundi tofauti tofauti ambapo kuna waliokuwa wakionyeshwa kama familia nzima, au mtu mmoja mmoja ambapo alikuwa akionyeshwa uwezo wake, ukatili wake na mambo mengine kama hayo,watu wafupi (dwarf), pia walionyeshwa watoto wakiume na wakike ambapo walikuwa wakipewa ndizi kama vile tuendavyo kuangalia nyani au sokwe. Ni ukatili mkubwa japo kwao ni furaha iliyoje.
Moja kati ya stori ya kusisimua ni ya Ota Benga huyu alikuwa ni mwafrika aliyenunuliwa na mmishonari na mgunduzi Dr Samuel Philips Verner na kupelekwa USA mnamo mwaka 1904, inasemekana Verner alimleta Benga akiwa na watu wengine saba na kijana mdogo toka Kongo ambao walinunuliwa toka kwa mfanyabiashara wa watumwa ambapo familia ya Benga yani mke na watoto wake waliuliwa katika mauaji ya halaiki (massacre). Historia inasema kwamba, ujio wa Benga na wenzake ulikuwa kivutio kikubwa kwani katika kipindi hiki biashara ya utumwa ilikuwa imefifia sana na hivyo maonyesho yaliyodumu kwa muda wa miaka 400 yalikuwa yamepoteza mvuto kwa kukosa bidhaa (binadamu). Kundi la Benga na wenzake walikuwa wakisafirishwa kimaonyesho kwenda sehemu mbalimbali ikiwemo toka St louis, New orleans, Mardi glas na kisha kufika mpaka Afrika. Katika kuzunguka kote huku inasemekana Benga alionyesha juhudi ya kutaka kujua kusoma na kujifunza mambo ambapo alikuwa akimuomba Verner kumrejesha nyumbani Afrika.
Mnamo mwezi wa nane mwaka 1906 Verner na Benga walifanikiwa kufika New York, ambapo Verner alikuwa akitafuta sehemu ya kumuweka Benga ili aishi huko. Hatimaye akafanikiwa kumpeleka katika Bronxy zoo ambapo mwanzoni alikuwa akitembea tembea na kuwasaidia wafanyakazi wa zoo hiyo. Lakini mwanzoni mwa mwezi wa tisa mwaka huo huo ikaamuliwa Benga apelekwe katika Orang Utan cage ambapo alikuwa akihamasishwa kucheza na jamii hiyo ya Orang utan na kufuma kofia pamoja na kuchezea mshale na upinde. Cage hii ilikuwa ikisimamiwa na Madison Glant huyu alikuwa ni New York Zoologist. (Masimulizi haya yapo katika kitabu cha Ota Benga, The Pygy in the zoo, kilichoandikwa na mjukuu wa Verner, Philips Bradford)
Pamoja na kuwepo kwa ukatili wa binadamu hususani asili ya watu weusi uliokuwa ukifanywa na wamishionari, lakini pia kulikuwa na kundi la watu waliokuwa wakipinga biashara ya maonyesho ya binadamu kama iliyokuwa kwa biashara ya utumwa. Dr Robert Stuart MacArthur of the Calvary Baptist Church in New York was outraged and was quoted in The New York Times on Sept. 10, 1906 as saying, ‘The person responsible for this exhibition degrades himself as much as he does the African. Instead of making a beast of this little fellow, he should be put in school for the development of such powers as God gave to him. It is too bad that there is not some society like the Society for the Prevention of Cruelty to Children. We send our missionaries to Africa to Christianise the people, and then we bring one here to brutalise him.
“Mtu anayejihusisha na maonyesho haya, anajishusha yeye mwenyewe kama vile anavyowafanyia wa afrika, badala ya kumfanyia mambo hayo ilitakiwa tumpeleke shule akajifunze kwa kadili ya uwezo wao waliopewa na Mungu, ni jambo baya sana kwa jamii inayopinga unyanyasaji na ukatili kwa watoto, iliyotuma wamishonari Afrika kwenda kuhubili, kisha kuja na watu haohao na kuwafanyia ukatili” (tafsiri hii ya kimaana ni yangu).
Haya ni maneno yaliyotolewa na kasisi aliyekuwa ana asili ya Afrika-Amerika. ‘Our race, we think, is depressed enough without exhibiting one of us with the apes,’ wrote one such minister, James H. Gordon to the mayor of New York. ‘We think we are worthy of being considered human beings, with souls.’ Gordon was to become Ota Benga’s guardian after the zoo ultimately bowed to public pressure and had Benga removed.
Baada ya Benga kuwa chini ya usimamizi wa Gordon, alihamishiwa katika makazi yaliyojulikana kama Howard Colored Orphan Asaylum yaliyokuwa yamefadhiriwa na kanisa. Mnamo january 1910 Gordon akamfanyia Benga mpago wa kwenda Lynchburg, Virginia. Wakati huu Benga alikuwa akizungumza kiingereza kwa ufasaha huku akiwa anavalia mavazi ya kimarekani, baada ya kufika Virginia na hatimaye akaanza kufanya kazi katika kiwanda cha Tumbaku cha Lynchburgy. Pamoja na kwamba alikuwa na umbo dogo kuliko wafanyakazi wengine, alijidhihirisha kuwa ni wa kipekee hasa katika kupanda juu ya poles kufuata tumbaku bila ya kutumia ngazi, wenzake wakaanza kumwita Bingo. Alijihusisha na kusimulia historia ya maisha yake na alikuwa akipewa bia na watu kama shukrani ya simulizi yake. Katika kipindi hiki alikuwa na plani ya kurudi nyumbani Congo, lakini baada ya kutokea kwa vita ya kwanza ya dunia ndoto yake ikawa imefifia kwa kiasi kikubwa. Mnamo tarehe 20-3-1916 Benga akiwa na umri wa miaka 32 aliamua kukatisha uhai wake kwa kutumia bastola (pisto) aliyokuwa ameiba, kwa kujilipua upande wa moyo wake so sad kwa kweli. Cheti chake cha kifo kimeandikwa OTTO BINGO.

View attachment 1011512
Maonyesho yaliyofanywa na Jesuits huko hispania barcelona 1929

View attachment 1011513
Picha ya Roshina, mwanamke toka Guinea “malkia wa kwanza” wa maonyesho ya kireno huko Oporto mwaka 1934

View attachment 1011514
Maonyesho ya kikoloni huko paris 1906

View attachment 1011517
Mchoro wa saartije baartman huko makumbusho ya uingereza

View attachment 1011510
Watot waliokuwa wakihifadhiwa kwa maonyesho hapo akipewa ndizi na watazamaji

View attachment 1011511
Namna ambavyo walikuwa wakifanyiwa waafrika wenzetu.
Historia ni ndefu sana waweza kujiongeza kwa kutafuta maarifa zaidi kwa ku-google HUMAN ZOO
Mababu zetu walikuwa viazi sana, ndio walioweka msingi wa ngozi nyeusi kuwa na inferiority issues!
 
Mababu zetu walikuwa viazi sana, ndio walioweka msingi wa ngozi nyeusi kuwa na inferiority issues!
Ujima ndo uliwaponza. Waliwekeza sana kwenye nidhamu. Nidhamu ikizidi unakuwa lofa,huna utofauti na msukule. Ujue ukifuatilia baadhi ya makabila katika mambo yao ya jadi,utakuja ujiulize hawa watu walikuwa malofa kiasi gani. Kuna kabila fulani kusini walikuwa kiongozi wao anapofaliki. Anazikwa pamoja na mtu mwingine akiwa hai anaenda kumpakata yule maiti ambaye ni kiongozi wao. Huu wenyewe waliita ni ushujaa. Sasa aina hii ya nidhamu ndio ubwege na ndio hata unaweza ukaona jinsi haikuwa kazi ngumu kuwapata watumwa
 
Ujima ndo uliwaponza. Waliwekeza sana kwenye nidhamu. Nidhamu ikizidi unakuwa lofa,huna utofauti na msukule. Ujue ukifuatilia baadhi ya makabila katika mambo yao ya jadi,utakuja ujiulize hawa watu walikuwa malofa kiasi gani. Kuna kabila fulani kusini walikuwa kiongozi wao anapofaliki. Anazikwa pamoja na mtu mwingine akiwa hai anaenda kumpakata yule maiti ambaye ni kiongozi wao. Huu wenyewe waliita ni ushujaa. Sasa aina hii ya nidhamu ndio ubwege na ndio hata unaweza ukaona jinsi haikuwa kazi ngumu kuwapata watumwa
Hakika mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom