Human Rights' Press release on Dr Ulimboka

NIMEAMINI WANAHARAKATI WANATUMWA
this press release is rubbishhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh! hawana akili hawa wanaharakati. wakiambiwa teteeni ndoa ya jinsia moja wanatetea! naichana hii ripoti.. shaa shaa shaaaaaaaaa

Kwani ni nani Tanzania hatumiwi? Kama serikali inategemea zaidi ya nusu ya bajeti yake kutoka kwa wafadhili maana yake nini? sio kwamba Tanzania nzima tunatumiwa (kuanzia serikali mpaka wananchi wenyewe wanaotegemea bajeti hiyo). Ivi kweli serikali inaweza kunyanyua mdomo mbele ya mfadhili anayewapa zaidi ya nusu ya mahitaji yao ili waishi? Umeona wapi mtu anakuja nyumbani kwako anakupa fedha zaidi ya nusu yaku-kuhudumia wewe na familia yako bila demand zozote? Nafikiri inabidi tujiangalie sana kwenye hizi kebehi tunazotoa; ukitazama sana tunaji-kebehi wenyewe bila kujua. Hao hao wafadhili mnaowadhihaki wakikatisha hilo fungu la bajeti utaona pressure zitakavyopanda.
 
Tumia akili..walienda kwenye mkutano na mtu wa ikulu.ndipo yalipotokea hayo..it shouldn't even have been 'allegedly'..it should have been 'kidnapped and tortured by Tanzania Government secret service agents..'

Hii tactic waliitumia pia "puppets wa Moi" Walikuwa na torture chamber na-kulikuwa na mass killings kabla upinzani kushinda. Kuna mzee mmoja alimpinga Moi (name withheld); yeye alikimbilia nchi za magharibi na familia yake. Yeye alinielezea kwamba baada ya upinzani kushinda maadui wa Moi (akiwepo yeye) walishinikiza Moi & co wafanyiwe the same thing. Yakafanyika mazungumzo kati ya pande mbili Mzee Moi & Co waka-confess; wakawaonyesha the otherside ilipokuwapo torture chamber yaani kulikuwa kumebaki mafuvu. Ilichukua months and months of peace talks na kuwekana sawa.. It is real real sad kwakweli. Viongozi wengi waki-Africa wanapenda wawe watawala na sio viongozi. Mungu alishapanga Dr. Ulimboka akutwe hai ili watu waelewe hasa tunakokwenda..
 
Hivi mzinga wanauza SMG ? KAMA SIO...Kwa kuwa imesemwa SMG ilitumika katika utekahji,kitendo cha silaha zinazomilikiwa na serikali kutumika kwenye utekaji,moja kwa moja pasipo kumung'unya maneno'Serikali inahusika' moja kwa moja au kupitia watumishi wake...Usilete habari ya oooh hata majambazi wanazo,majambazi wa aina hiyo sio hao,majambazi wenye SMG wanatafuta fedha na si kujeruhi madaktari kwa kuongoza mgomo

H1N1,

Unaijua SMG au unaisikia tu kijana?

Huyo aliyekwambia kama wahusika walikuwa na SMG ni nani? kama ungefahamu matumizi ya SMG wala usingesema hayo unayosema. Kama kuna mtu anasema hao jamaa walikuwa na SMG basi yeye nae anatakiwa atiwe hatiani maana inaonesha wakati Ulimboka anachukuliwa yeye alikuwa busy kukodolea silaha. Na kama ni ulimboka mwenyewe ameripoti SMG basi atakuwa amepata maumivu makali ya kichwa pengine na fahamu zake zinachanga habari , ukizingatia yeye ni daktari hana ujuzi wa mambo ya silaha hiyo habari ya SMG itakuwa kama ile ya waziri Malima aliyekutwa na Shot gun ya kuwindia.
 
Mijitu mingine bwana!

Hivi wewe kwa akili yako unategemea hawa waliomteka Dr.Ulimboka ni watu waliotumwa na ndugu zake wanaogombea shamba kweli???Mimi siyo mwanasheria lakini hata Mahakamani kuna kitu wanaita,''circumstancial evidences'' au ushahidi wa kimazingira. Huo tu unatosha kumtia mtu hatiani. Sasa hebu tuangalia mazingira ya kutekwa kwa Dr. Ulimboka: Kwamba alipigiwa simu na mtu wa serikali(siyo ndugu yake,jamaa au rafiki) kwamba wakutane Leaders Club.Wakti wakiongea wakaja wale jamaa(agents) wakiwa na silaha(not majambazi) yumkini ni plain cloth policemen au Usalama wa Taifa na wakadai wanamtaka Dr. ULIMBOKA TU. Kilichofuatia hapo tunakielewa mpaka kuja kuokotwa kwa Dr. Ulimboka toka msitu wa Mabwepande.

Lakini pia wakti wa harakati za kumfikisha Dr. Ulimboka pale MOI baadaye walimbaini askari mmoja akiwa CHOONI AKIWASILIANA NA WENZAKE SOMEWHERE KWA RADIO CALL AKIWAELEZA KUWA JAMAA(DR.ULIMBOKA) HAJAFA BADO ANAPUMUA!!!Hapa haihitaji hata akili ya kwenda kusomea sheria kila kitu kiko wazi. Kama ni askari Polisi uko kwenye kutimiza wajibu wako KWANINI UKAONGELEE CHOONI??Ni dhahiri hawa walikuwa Government AGENTS WALIOKUWA WAMEPEWA MAELEKEZO MAALUMU YA KWENDA KUMKAMATA NA KUMWUA HUYU DOC ILI KUMNYAMAZISHA KWA KIFO!!!Huo ni ukweli ambao kila mtu mwenye akili timamu atakubaliana nao.

Mimi kwa mawazo yangu ni kwamba tunataka haya 3 yafuatayo yafanyiwe kazi kwa haraka sana:
  1. Huyu kigogo wa Serikali aliyemwita Dr. Ulimboka wakutane Leaders Club ni nani na awe wa kwanza kukamatwa ili aisadie polisi.Huyu atakuwa anajua mchongo wote.
  2. Yule askari alyekuwa anawasiliana na wenzake kuwajulisha kuwa Dr. Ulimboka hajafa naye akamatwa kama yule kigogo.
  3. Kuundwe tume huru itakayohusisha pande zote mbili MADAKTARI,SERIKALI(POLISI)na KAMATI YA BUNGE YA HAKI ZA JAMII ili kufanya uchunguzi wa kina kabisa kuhusu sakata hili. Kama POLISI wataachwa peke yao washughulikie hili tatizo basi tusitarajie matokeo mazuri! Maana kama kweli kuna mkono wa serikali LAZIMA WATACHAKACHUA TU!We really know them.

Wasalaam.

Makoye2009,

Naomba nikuulize swali dogo , wewe leo ukipigiwa simu na mtu usiyemfahamu akakwambia kwamba yeye ni mtu wa serikali anataka kuonana na wewe utaenda?

Hilo la kusema "hajafa bado anapumua" ni upuuzi mtupu. Hata mimi ningekuwa eneo la tukio namfahamisha mwenzangu aliyembali ningejificha kwa mbali ikiwezekana chooni nikaongea kama alivyoongea askari. Kwa sababu alichosema askari ni kweli Dr alikuwa bado anapumua na yeye ana wajibu wa kufahamisha vyombo vinavyohusika ili vijue vinaanzia wapi kufanya kazi yao.

Tume huru naunga mkono lakini isihusishe wanaharakati ambao tayari wameshasema "govt agents wamehusika" haina maana ya wao kuwepo kwenye tume ambayo inatafuta "FACTS" wakati wao tayari wapo kwenye conclusion.

Ukweli utajulikana na huyu Daktari Ulimboka kama hatasema ukweli wa yaliyomsibu atakuja kuumbuka mbele ya safari.
 
Kama umeshindwa kuitisha hayo maandamano sasa hivi hata ungekuwa kwenye chama gani cha wanaharakati usingeitisha maandamano. Mtu uliyejificha nyuma ya monitor hauwezi ukatoa uchafu kama huo kwa huyu mama jasiri...!

Mwambie mkuu naona anasema sana wakati yuko nyuma ya pazia.
 
Ujinga mtupu, sasa hapa kaongea nini? I thought she is calling for a mass movement against this barbaric deeds by the government! Yeye anatoa kauli ya kulaani? Tena anailaani serikali ya viziwi hii isiyo na hata tone la aibu? Huyu Bisimba naye anazeeka vibaya. Amenichefua tu hapa, sijaona la maana!

Hivi unaweza kusimama mbele za watu na kuanza kulaani matendo ya kichaa? Si utaonekana na wewe ni kichaa tu? Kama kichaa analeta kero mtaani kwenu chukueni hatua za ama kuchangishana hela mmpeleke milembe au mmhamishe mtaani kwenu.

Sasa Bisimba anapolaani vitendo vya serikali ya vichaa hii si anaonekana yeye ndiyo kichaa? Imeshalaaniwa na wangapi na kwa mangapi na hakuna chochote ilichorekebisha zaidi ya ubabaishaji usiokoma? To hell with vyama vya wanaharakati visivyo na meno hivi!

Ningekuwa mimi saa hizi ningekuwa naitisha countrywide demonstration against this brutal act bila kujali ni nani amefanya hilo. Ni kazi ya serikali kulinda usalama wa watu wake na kama imeshindwa iachie ngazi. Period! Sasa analeta longolongo, ashakuwa mwanasiasa?

Lukolo....Unasema ungekuwa wewe kwani hapo ulipo sio wewe?? Acha maneno matupu ya kwenye mitandao ya kijamii huyo mama pamoja na umri wake kuwa mkubwa ameshaonyesha ujasiri mkubwa mpaka kupelekea kuwekwa kizuizini.
Fikiria kabla ya kuandika kashfa za namna hii pia na wewe fanya sehemu yako usikae tu ukategemea kila kitu aanzishe Mama Kijo Bisimba.
Tunisia kijana Mohammed Bouazizi alijichoma moto hadharani akasababisha mabadiliko ya kihistoria,tujiulize mimi na wewe tutafanya nini? Sio kusema 'kama ningekuwa yule au ningekuwa mimi' unataka uwe wewe mara ngapi?
Tunaweza tujiamini na tujaribu.
 
Last edited by a moderator:
H1N1,

Unaijua SMG au unaisikia tu kijana?

Huyo aliyekwambia kama wahusika walikuwa na SMG ni nani? kama ungefahamu matumizi ya SMG wala usingesema hayo unayosema. Kama kuna mtu anasema hao jamaa walikuwa na SMG basi yeye nae anatakiwa atiwe hatiani maana inaonesha wakati Ulimboka anachukuliwa yeye alikuwa busy kukodolea silaha. Na kama ni ulimboka mwenyewe ameripoti SMG basi atakuwa amepata maumivu makali ya kichwa pengine na fahamu zake zinachanga habari , ukizingatia yeye ni daktari hana ujuzi wa mambo ya silaha hiyo habari ya SMG itakuwa kama ile ya waziri Malima aliyekutwa na Shot gun ya kuwindia.

SMG naijua,nimepita JKT nimeitumia...
Watu wengi wasio askari wanaijua SMG si kwa kuwa ilitumika mahali lah,bali ni silaha ya kijeshi ambayo ikitumiwa kwenye ujambazi huwa inaonyeshwa,mtu anayeijua SMG hawezi ifananisha na shortgun,SMG zimetapakaa mitaani zikiwa mikononi mwa mapolisi wetu kwenye doria au kwa wale walindao Benki,kama ulifikiri kwa kutumia SMG kumteka watu hawataitambua umebugu step,wakati mnamteka mlitumia silaha gani kama sio SMG ? Funguka bro.
 
hawa kina kijo bi simba ni wachochezi wakubwa,naona wanataka fedha za wafadhili kwa nguvu.

wanaposema MOST LIKELY TO STATE AGENTS INA MAANA WAO WAMESHAMALIZA UCHUNGUZI NA HAYO NDIO MAJIBU YAKE.HUU NI UCHOCHEZI UNAOLENGA KUPANDIKIZA CHUKI KWA WANANCHI DHIDI YA SERIKALI.
 
Wamekosea hapo kusema "Most likely alleged to be state agents" wangeacha blank kama hapo mwanzo waliposema "Unknown group of individuals" , kwa kutumia maneno haya inaonesha wao wanakuwa driven na emotions zaidi kuliko weledi! Pathetic!

Je ikibainika huko mbele kwamba wana ugomvi wa kugombea shamba la urithi Dr Ulimboka na ndugu zake?

Huna utu usijidai kukosoa hapa we walewale akina Mchemba tu ambao badala ya kuangalia theme wanapambana na context na typing error
 
ulimboka.jpg

mtanisamehe wakuu kwa kudgrug hii kitu ndefu.

Yangu ni haya.

1.je haya ndio matokeo ya utafiti/uchunguzi wa kisayansi waliofanya??

2.watuthibitishie kuwa ni kweli serikali imehisika maana kusema most likely to be state agents umejiridhisha vya kutosha.

3.ikija kubainika kuwa sio serikali hawa kina bisimba watajificha wapi?


4.bisimba anazungumziaje watanzania maskini wanaokufa kwa kukosa matibabu kutokana na mgomo wa madaktari

5.tunaomba academic qualifications zao ili tujue elimu yao kwani tamko hili halina hadhi ya watu waliosoma

6.watupe utaratibu waliotumia kuajiriwa kwani kwa shirika makini hasa haya ya haki za binadam wasingeweza kuajiri watu wanaokurupuka kwenye mambo kama walivofanya hawa kina bisimba

7.pole dr ulimboka
 
Wamekosea hapo kusema "Most likely alleged to be state agents" wangeacha blank kama hapo mwanzo waliposema "Unknown group of individuals" , kwa kutumia maneno haya inaonesha wao wanakuwa driven na emotions zaidi kuliko weledi! Pathetic!

Je ikibainika huko mbele kwamba wana ugomvi wa kugombea shamba la urithi Dr Ulimboka na ndugu zake?
Hakuna mtu binafsi anayeweza kuorganize tukio kama hili..ww ndio pathetic. Matukio ya ugomvi wa familia na individuals ktk mazingira ya TZ yana picha tofauti na hii.
Unapofanyiwa jambo lolote baya the first step is find the prime suspect kutokana na historia ya maisha yako. Kwa historia ya maisha ya Dr. Ulimboka kwa muda huu mfupi tuliomfaham alikuwa na ugomvi na serikali. Sasa kama kuna maadui wengine wa Ulimboka unawajua waseme, sio unakuja na assumption za kizushi.
 
Watanzania maskini wanakufa kwa kukosa huduma wakati madaktari wanapokea mishahara inayotokana na kodi zao.huu nao ni ufisadi mwingine
 
mtanisamehe wakuu kwa kudgrug hii kitu ndefu.

Yangu ni haya.

1.je haya ndio matokeo ya utafiti/uchunguzi wa kisayansi waliofanya??

2.watuthibitishie kuwa ni kweli serikali imehisika maana kusema most likely to be state agents umejiridhisha vya kutosha.

3.ikija kubainika kuwa sio serikali hawa kina bisimba watajificha wapi?


4.bisimba anazungumziaje watanzania maskini wanaokufa kwa kukosa matibabu kutokana na mgomo wa madaktari

5.tunaomba academic qualifications zao ili tujue elimu yao kwani tamko hili halina hadhi ya watu waliosoma

6.watupe utaratibu waliotumia kuajiriwa kwani kwa shirika makini hasa haya ya haki za binadam wasingeweza kuajiri watu wanaokurupuka kwenye mambo kama walivofanya hawa kina bisimba

7.pole dr ulimboka
Ndio mana wametumia maneno most likely na alleged..kwa maana nyingine ni prime suspect. Ww ungeambiwa sasa hivi kuchunguza tukio la Ulimboka ungeanzia wapi?
 
Madai ya msingi yapi yaliyotekelezwa na serikali? Si uwapeleke hao ndugu zako kwenye private Hospitals sasa wasife, unamlalamikia nani?

nyie madaktari ni mafisadi,kwanza mnapokea mishahara inayotokana na kodi zetu
halafu mnagoma kuhudumia wananchi,
pili mnaiba madawa mnaenda kuuza kwenye hospitali zenu,wehu sana nyie,mungu atawaadhibu
 
Ndio mana wametumia maneno most likely na alleged..kwa maana nyingine ni prime suspect. Ww ungeambiwa sasa hivi kuchunguza tukio la Ulimboka ungeanzia wapi?

popote pa kuanzia lakini sio kumtaja mtu mana ukishaanza kumtuhum mtu huku unachunguza unaharibu kila kitu.

naamini tunahitaji uchunguzi huru sio majibu ya kihisia
 
popote pa kuanzia lakini sio kumtaja mtu mana ukishaanza kumtuhum mtu huku unachunguza unaharibu kila kitu.

naamini tunahitaji uchunguzi huru sio majibu ya kihisia
Hakuna kitu kama hicho 'popote pale'..there should be a starting point which is determined by a series of events. Lakini sababu wengine mmetumwa hapa JF kuja kupiga propaganda na kujaribu kuleta theories za kizushi, you will write any **** kujustify ujinga wenu.
Unfortunately, in a corrupt country like TZ hata huo uchunguzi ukikamilika unaweza ukaja na majibu ya uongo utakaofanywa ukweli. That is why we rely and believe on the series of events and circumstances rather than what the police reveals, court rules or any government official says. Because many of them are the beneficiaries of this system.
 
Nina amini ni haki ya LHRC kulaani. Watu hawa wametekeleza wajibu wao wa uandikishwaji wao. Kuna bwana mmoja naona yeye anawaponda kwa kusema afadhali wangeitisha manadamao nchi nzima. Mimi ninafikirihilo angeliweka kama wazo lake kwa wanaharakati hawa na si kuwalalamikia. In other good words -- one needs to know what heart is saying first before he/she can act. Labda yaweza ikawa ni busara sasa kuzungumzia maandamano baada ya tamko kama LRHC kutoka.

Maandamano basi yatokana na Tamko kwa kuliunga mkono na si lazima maandamano hayo yaanzishwe na LHRC. Sisi tuandamane kwa kuunga mkono Tamko la LRHC.
 
Back
Top Bottom