Hukumu ya Sabaya imeiumbua CCM

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,603
29,743
Jana dunia imeshuhudia hukumu ya haki iliyotolewa na mahakama dhidi ya kada mwandamizi wa CCM Lengai Ole Sabaya ambaye amehudumu nafasi mbalimbali ndani ya chama (UVCCM), na hata kuteuliwa na JPM kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai.

Hukumu ya Mahakama imeenda kuhitimisha kesi iliyomkabili Sabaya ambapo alitiwa hatiani kwa makosa ya ujambazi wa kutumia silaha.

Sitaki kuingia undani wa kesi kwa sababu wachambuzi mbalimbali wameshaweka mabandiko humu wakielezea kwa kina na kwa vipengele vya kisheria na hata wengine waliweka bettings za kumtoa au kumtia Sabaya hatiani.

Hapa najikita kwenye eneo la Siasa.

Sabaya ametenda makosa yake akiwa mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya. Hakuwahi kuonywa wala kupewa angalizo dhidi ya mwenendo wake huo. Ikumbukwe katika moja ya matukio aliyoyafanya aliwahi kusifiwa na mteuzi wake, waziri wa fedha (sasa Makamo wa Rais), Gavana wa Benki Kuu na hata TRA waliwahi kutia neno la kumuunga mkono.

Hitimisho la.kesi hii, hata kama Sabaya atakata rufaa na kushinda limeiweka CCM kwenye kona mbaya sana ya kukosa uaminifu wa kisiasa. Sabaya kama Mkuu wa Wilaya, anashika nafasi ya 4 kwenye Kamati ya Siasa ya Wilaya. Anaingia vikao vyote vya maamuzi ya CHAMA ngazi ya Wilaya. Pia ikumbukwe yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Mahakimu wikayani. Hivi vyeo vyote vilipaswa kumfanya awe makini na tahadhari kuwa kwenye wajibu wake.

Ushiriki wake kwenye siasa kama kamisaa wa Chama Wilayani umeleta tafsiri mpya sasa, tafsiri yake ni kwamba hawa viongozi wanaoteuliwa na Rais wamekuwa wanajiona wana kinga ya kutoshtakiwa wakati Katiba ya JMT inatoa kinga kwa rais pekee. Wanaweza wakafanya lolote kwa yeyote na wasifanywe chochote.

Sabaya alifanikisha mradi wa CCM kuwaminya Wapinzani Wilaya ya Hai. Ikumbukwe namna alivyofanikisha ushindi wa kibabe kwenye uchaguzi Mkuu Oktoba 2020 ambapo Mbowe alikosa ushindi kwa kuporwa kura zake huku mshindani kutoka CCM akishinda isivyo halali.

Kufungwa miaka 30 jela kwa kosa la ujambazi, na kosa lenyewe lilifanyika akiwa Mteule wa Rais ambapo anaongoza vyombo vya Ulinzi na Usalama Wilaya ni DOA kubwa sana kwa medani za kisiasa. Doa hili halimuachi salama mteuzi. Doa hili haliiachi salama CCM.

Kutumia madaraka yako kufanya ujambazi tena wa silaha dhidi ya watu ambao umeapa kuwalinda na kuwahakikishia ustawi wao kijamiii na kiuchumi ni jambo linaloleta ukakasi mkubwa kwa wadadisi wa kisiasa.

Inawezekana Sabaya ameangukiwa na jani la vunjagenge lakini wapo wengine ambao hawajaguswa na kiujambazi ni wabaya kuliko Sabaya.

Wapinzani wakiacha siasa zao za OyaOya na kujikita kimkakati, huu ndiyo wakati wa kuielezea CCM kwa Umma namna ambavyo inakumbatia na kulinda wahalifu kwa kigezo cha HUYU NI MWENZETU. Hukumu ya Sabaya iwafungue macho kuifahamu CCM halisi na siyo hii ambayo inajitabainisha kuwa ina viongozi safi na wenye falsafa.

Wananchi wameshaanza kuichoka CCM tangu kale, na kinachoisaidia ni ndoa yake ya mitala na vyombo vya Ulinzi na Usalama ambapo vimeapa kufanya lolote hata ikibidi kuua nusu ya Watanzania ili CCM iendelee kutawala.

Ukishatishia maslahi ya CCM, fahamu kuwa umetishia maslahi ya Nchi. Ifike mahala tuyaone haya mambo kwa jicho la udadisi na utafiti.

Nyerere aliwahi kusema Tanzania na Watanzania Kwanza kisha mengine yanafuatia. Pia aliwahi kusema kuwa CCM siyo baba wala mama yake.

Ni wakati sasa wa walio wasafi ndani ya CCM kujiepusha na chama hiki ili kuleta mwanzo mpya wa siasa na uongozi wa nchi yetu.

Kesi hii ya Sabaya imezua mijadala mitaani kuhusu hatima ya CCM kwenye chaguzi zijazo.

Mungu isaidie na kuibariki Tanzania
IMG-20211015-WA0029.jpg
IMG-20211015-WA0025.jpg
2ojspt.jpg
 
Daima tukumbuke cheo ni dhamana. Hakuna aliyekuja nacho duniani. Kuwa mtu wa haki siku zote, haki itakufuata daima.
 
Jana dunia imeshuhudia hukumu ya haki iliyotolewa na mahakama dhidi ya kada mwandamizi wa CCM Lengai Ole Sabaya ambaye amehudumu nafasi mbalimbali ndani ya chama (UVCCM), na hata kuteuliwa na JPM kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai.

Hukumu ya Mahakama imeenda kuhitimisha kesi iliyomkabili Sabaya ambapo alitiwa hatiani kwa makosa ya ujambazi wa kutumia silaha.

Sitaki kuingia undani wa kesi kwa sababu wachambuzi mbalimbali wameshaweka mabandiko humu wakielezea kwa kina na kwa vipengele vya kisheria na hata wengine waliweka bettings za kumtoa au kumtia Sabaya hatiani.

Hapa najikita kwenye eneo la Siasa.

Sabaya ametenda makosa yake akiwa mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya. Hakuwahi kuonywa wala kupewa angalizo dhidi ya mwenendo wake huo. Ikumbukwe katika moja ya matukio aliyoyafanya aliwahi kusifiwa na mteuzi wake, waziri wa fedha (sasa Makamo wa Rais), Gavana wa Benki Kuu na hata TRA waliwahi kutia neno la kumuunga mkono.

Hitimisho la.kesi hii, hata kama Sabaya atakata rufaa na kushinda limeiweka CCM kwenye kona mbaya sana ya kukosa uaminifu wa kisiasa. Sabaya kama Mkuu wa Wilaya, anashika nafasi ya 4 kwenye Kamati ya Siasa ya Wilaya. Anaingia vikao vyote vya maamuzi ya CHAMA ngazi ya Wilaya. Pia ikumbukwe yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Mahakimu wikayani. Hivi vyeo vyote vilipaswa kumfanya awe makini na tahadhari kuwa kwenye wajibu wake.

Ushiriki wake kwenye siasa kama kamisaa wa Chama Wilayani umeleta tafsiri mpya sasa, tafsiri yake ni kwamba hawa viongozi wanaoteuliwa na Rais wamekuwa wanajiona wana kinga ya kutoshtakiwa wakati Katiba ya JMT inatoa kinga kwa rais pekee. Wanaweza wakafanya lolote kwa yeyote na wasifanywe chochote.

Sabaya alifanikisha mradi wa CCM kuwaminya Wapinzani Wilaya ya Hai. Ikumbukwe namna alivyofanikisha ushindi wa kibabe kwenye uchaguzi Mkuu Oktoba 2020 ambapo Mbowe alikosa ushindi kwa kuporwa kura zake huku mshindani kutoka CCM akishinda isivyo halali.

Kufungwa miaka 30 jela kwa kosa la ujambazi, na kosa lenyewe lilifanyika akiwa Mteule wa Rais ambapo anaongoza vyombo vya Ulinzi na Usalama Wilaya ni DOA kubwa sana kwa medani za kisiasa. Doa hili halimuachi salama mteuzi. Doa hili haliiachi salama CCM.

Kutumia madaraka yako kufanya ujambazi tena wa silaha dhidi ya watu ambao umeapa kuwalinda na kuwahakikishia ustawi wao kijamiii na kiuchumi ni jambo linaloleta ukakasi mkubwa kwa wadadisi wa kisiasa.

Inawezekana Sabaya ameangukiwa na jani la vunjagenge lakini wapo wengine ambao hawajaguswa na kiujambazi ni wabaya kuliko Sabaya.

Wapinzani wakiacha siasa zao za OyaOya na kujikita kimkakati, huu ndiyo wakati wa kuielezea CCM kwa Umma namna ambavyo inakumbatia na kulinda wahalifu kwa kigezo cha HUYU NI MWENZETU. Hukumu ya Sabaya iwafungue macho kuifahamu CCM halisi na siyo hii ambayo inajitabainisha kuwa ina viongozi safi na wenye falsafa.

Wananchi wameshaanza kuichoka CCM tangu kale, na kinachoisaidia ni ndoa yake ya mitala na vyombo vya Ulinzi na Usalama ambapo vimeapa kufanya lolote hata ikibidi kuua nusu ya Watanzania ili CCM iendelee kutawala.

Ukishatishia maslahi ya CCM, fahamu kuwa umetishia maslahi ya Nchi. Ifike mahala tuyaone haya mambo kwa jicho la udadisi na utafiti.

Nyerere aliwahi kusema Tanzania na Watanzania Kwanza kisha mengine yanafuatia. Pia aliwahi kusema kuwa CCM siyo baba wala mama yake.

Ni wakati sasa wa walio wasafi ndani ya CCM kujiepusha na chama hiki ili kuleta mwanzo mpya wa siasa na uongozi wa nchi yetu.

Kesi hii ya Sabaya imezua mijadala mitaani kuhusu hatima ya CCM kwenye chaguzi zijazo.

Mungu isaidie na kuibariki TanzaniaView attachment 1976068View attachment 1976070View attachment 1976075

D1D1851F-C051-472B-928B-08ACDB7515EA.jpeg
 
Kuna mtifuano mkubwa ndani ya CCM sasa hasa baada ya hii Hukumu tutaona na kusikia mengi.

Grim Reaper atapata tenda za hapa na pale au siyo Mshana Jr?
 
Kila kitu ni mtazamo...

Mwingine anaweza sema kimeisafisha ccm na matendo maovu ya wachache..
Kashtakiwa Hadi kuhukumiwa chini ya serikali ya CCM..
 
Mkuu wa wilaya ni mwenyekiti wa kamati ya maadili ya mahakimu wilayani?!
Jana dunia imeshuhudia hukumu ya haki iliyotolewa na mahakama dhidi ya kada mwandamizi wa CCM Lengai Ole Sabaya ambaye amehudumu nafasi mbalimbali ndani ya chama (UVCCM), na hata kuteuliwa na JPM kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai.

Hukumu ya Mahakama imeenda kuhitimisha kesi iliyomkabili Sabaya ambapo alitiwa hatiani kwa makosa ya ujambazi wa kutumia silaha.

Sitaki kuingia undani wa kesi kwa sababu wachambuzi mbalimbali wameshaweka mabandiko humu wakielezea kwa kina na kwa vipengele vya kisheria na hata wengine waliweka bettings za kumtoa au kumtia Sabaya hatiani.

Hapa najikita kwenye eneo la Siasa.

Sabaya ametenda makosa yake akiwa mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya. Hakuwahi kuonywa wala kupewa angalizo dhidi ya mwenendo wake huo. Ikumbukwe katika moja ya matukio aliyoyafanya aliwahi kusifiwa na mteuzi wake, waziri wa fedha (sasa Makamo wa Rais), Gavana wa Benki Kuu na hata TRA waliwahi kutia neno la kumuunga mkono.

Hitimisho la.kesi hii, hata kama Sabaya atakata rufaa na kushinda limeiweka CCM kwenye kona mbaya sana ya kukosa uaminifu wa kisiasa. Sabaya kama Mkuu wa Wilaya, anashika nafasi ya 4 kwenye Kamati ya Siasa ya Wilaya. Anaingia vikao vyote vya maamuzi ya CHAMA ngazi ya Wilaya. Pia ikumbukwe yeye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Mahakimu wikayani. Hivi vyeo vyote vilipaswa kumfanya awe makini na tahadhari kuwa kwenye wajibu wake.

Ushiriki wake kwenye siasa kama kamisaa wa Chama Wilayani umeleta tafsiri mpya sasa, tafsiri yake ni kwamba hawa viongozi wanaoteuliwa na Rais wamekuwa wanajiona wana kinga ya kutoshtakiwa wakati Katiba ya JMT inatoa kinga kwa rais pekee. Wanaweza wakafanya lolote kwa yeyote na wasifanywe chochote.

Sabaya alifanikisha mradi wa CCM kuwaminya Wapinzani Wilaya ya Hai. Ikumbukwe namna alivyofanikisha ushindi wa kibabe kwenye uchaguzi Mkuu Oktoba 2020 ambapo Mbowe alikosa ushindi kwa kuporwa kura zake huku mshindani kutoka CCM akishinda isivyo halali.

Kufungwa miaka 30 jela kwa kosa la ujambazi, na kosa lenyewe lilifanyika akiwa Mteule wa Rais ambapo anaongoza vyombo vya Ulinzi na Usalama Wilaya ni DOA kubwa sana kwa medani za kisiasa. Doa hili halimuachi salama mteuzi. Doa hili haliiachi salama CCM.

Kutumia madaraka yako kufanya ujambazi tena wa silaha dhidi ya watu ambao umeapa kuwalinda na kuwahakikishia ustawi wao kijamiii na kiuchumi ni jambo linaloleta ukakasi mkubwa kwa wadadisi wa kisiasa.

Inawezekana Sabaya ameangukiwa na jani la vunjagenge lakini wapo wengine ambao hawajaguswa na kiujambazi ni wabaya kuliko Sabaya.

Wapinzani wakiacha siasa zao za OyaOya na kujikita kimkakati, huu ndiyo wakati wa kuielezea CCM kwa Umma namna ambavyo inakumbatia na kulinda wahalifu kwa kigezo cha HUYU NI MWENZETU. Hukumu ya Sabaya iwafungue macho kuifahamu CCM halisi na siyo hii ambayo inajitabainisha kuwa ina viongozi safi na wenye falsafa.

Wananchi wameshaanza kuichoka CCM tangu kale, na kinachoisaidia ni ndoa yake ya mitala na vyombo vya Ulinzi na Usalama ambapo vimeapa kufanya lolote hata ikibidi kuua nusu ya Watanzania ili CCM iendelee kutawala.

Ukishatishia maslahi ya CCM, fahamu kuwa umetishia maslahi ya Nchi. Ifike mahala tuyaone haya mambo kwa jicho la udadisi na utafiti.

Nyerere aliwahi kusema Tanzania na Watanzania Kwanza kisha mengine yanafuatia. Pia aliwahi kusema kuwa CCM siyo baba wala mama yake.

Ni wakati sasa wa walio wasafi ndani ya CCM kujiepusha na chama hiki ili kuleta mwanzo mpya wa siasa na uongozi wa nchi yetu.

Kesi hii ya Sabaya imezua mijadala mitaani kuhusu hatima ya CCM kwenye chaguzi zijazo.

Mungu isaidie na kuibariki TanzaniaView attachment 1976068View attachment 1976070View attachment 1976075
 
Mkuu wa wilaya ni mwenyekiti wa kamati ya maadili ya mahakimu wilayani?!
 
Ila Gaidi mbowe akihukumiwa kwenda jera utakuwa uonevu na siyo haki si ndiyo?
Mkuu unaonekana upo mweupe sana kwenye masuala ya kisheria.Mbowe hawezi kuitwa gaidi hadi mahakama pekee ikimtia hatiani ndo unaweza kumuita gaidi.

Sabaya kwasasa kumuita jambazi ni sahihi kwasababu mahakama imethibitisha kuwa ni jambazi.Tujifunze sheria kuliko kuongozwa na mihemko ya kisiasa.
 
Back
Top Bottom