Hukumu Rufaa ya Godbless Lema yaiva

Hukumu Rufaa ya Godbless Lema yaiva

Hivi Lema akishinda rufaa baadaye CCM wakaipinga kwa kigezo cha jopo la majaji ku- include mtu ambaye si jaji itakuwaje? Technically huyu mzanzibar si jaji.
'Patamu' sana hapo!
 
Yule jaji aliyetoa hukumu nasikia yupo India kapooza na ameshakua kichaa.

Hilo ni somo muhimu sana kwa wakina jaji
Natalia Kimaro, Mbarouk Salim Mbarouk na Salum Massati kuwa Lema yupo pale kwa matakwa ya wananchi kwahiyo laana za wananchi huwa hazichelewi kupatiwa majibu na Mungu
 
Hapo hukumu itatoka kwa Jaji Massati na Kimaro,huyu mwingine jaji voda faster atawasindikiza tu.

Wakiambiwa wanateua majaji vihiyo wanabisha,sasa Werema aje abishe kuwa huyu jaji hasomi chuo kikuuu huria. Sasa kati ya Werema na Lissu nani anatumia kichwa chake kufuga nywele na sio kufikiri.
 
Hapo kwenye red kuna walakini hebu soma hapa chini ushahidi wa Mh. Tundu Lissu (MB) kama ulivyonukuliwa kwenye utetezi wake kwenye kamati haki, maadili na madaraka ya Bunge.

JAJI WA RUFAA MBAROUK SALIM MBAROUK

Mbarouk Salim Mbarouk aliteuliwa kuwa Jaji wa Rufaa wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania mwaka 2008. Kabla ya uteuzi huo Jaji Mbarouk alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar. Sifa za mtu kuteuliwa kuwa Jaji wa Rufaa zimeainishwa katika ibara ya 118(3) ya Katiba:


“Majaji ... wa Rufani watateuliwa na Rais, kwa kushauriana na Jaji Mkuu, kutoka miongoni mwa watu wenye sifa za kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ... zilizoainishwa katika Ibara ya 109 ya Katiba au kutoka miongoni mwa watu wanaoweza kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar kwa mujibu wa sheria zinazotumika Zanzibar na wamekuwa na sifa hizo kwa muda usiopungua miaka kumi na tano.”


Kwa mujibu wa Ibara ya 94(3) ya Katiba ya Zanzibar, 1984,
“Mtu hatoweza kuteuliwa kuwa Jaji au Kaimu Jaji wa Mahkama Kuu mpaka awe na shahada ya Sheria ya Chuo Kikuu kinachotambuliwa au Chuo cha aina hiyo; au awe au amewahi kuwa Jaji wa Mahkama zilizofanana na hii kwa kesi zote za jinai na madai katika Tanzania au sehemu yoyote ya Jumuiya ya Madola au Mahkama ya Rufaa kutoka Mahkama hizo; au awe Mwanasheria wa Zanzibar au Tanzania kwa kipindi kisichopungua miaka saba; au awe na uzoefu wa Jaji au mwanasheria kwa pamoja usiopungua miaka saba.”

Jaji Mbarouk hajatimiza hata moja ya masharti hayo ya Katiba ya Zanzibar. Jaji huyu hana shahada yoyote ya sheria inayotambuliwa na mamlaka ya ithibati ya Tanzania kama inavyotakiwa na Ibara ya 109(7) ya Katiba.

Jaji huyu ana stashahada ya juu ya sheria (Post Graduate Diploma in Law) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Shahada ya Uzamili ya Sanaa ya Chuo Kikuu cha nchini Uingereza.

Uteuzi wa Jaji Mbarouk kuwa Jaji wa Rufaa ulileta minong’ono mingi katika taaluma ya sheria kiasi kwamba marehemu Wakili Leopold Kalunga anasemekana kufungua shauri katika Mahakama Kuu ya Tanzania kutaka uteuzi huo utenguliwe. Hata hivyo, Wakili Kalunga alifariki kabla ya shauri lake kusikilizwa na kwa hiyo liliondolewa mahakamani.

Aidha, monong’ono hiyo ilimfanya Jaji wa Rufaa Mbarouk kujiunga na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ambako bado ni mwanafunzi hadi ninapoandika Addendum hii.

Kama huu ushahidi wa Mh Tundu Lissu ni wa kweli basi sijui hii nchi tuiiteje? Mtu anapanda vyeo hadi kuwa jaji wa mahakama ya rufaa huku akiwa hajawahi kusoma japo shahada ya kwanza ya sheria? Ajabu mno! Tusishangae kuambiwa ana sifa zaidi ya mwenye LLB, maana tumeshasikia sana hadithi zinazosema advanced diploma ni sawa na degree ya kwanza, lakini hatuambiwi kwa nini universities zinaendelea kutoa degrees badala ya advanced diploma, au kwa nini hiyo diploma isiitwe degree kama ziko sawa. Nashangaa mno!
 
Huyu kwenye red si ndiyo Mwanafunzi wa LLB Open university aliyetajwa na Tundu Lisu kuwa Kiwango Duni! Sina imani Naye atakomoa CDM.
RUFAA ya kupinga kuvuliwa ubunge ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), imepangwa kusikilizwa Septemba 20, mwaka huu, mbele ya majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa; Natalia Kimaro, Mbarouk Salim Mbarouk na Salum Massati.

Source: Tanzania Daima
 
Kama kuna mtu ana access na profile ya Lema pls ningependa kuona CV yake hapa JF! Asije akawa naye ni kihiyo tu asiye deserve kuwakilisha wananchi Bungeni!
 
Masati anaweza kuwa smart, what about Mbarouk Salim? Si ndiye jaji tuliyeambiwa na Lissu kuwa ndio kwanza anasomea shahada ya kwanza ya sheria chuo kikuu huria? Nina wasiwasi hata yule wakili Kalunga aliyefungua shauri kupinga uteuzi wa jaji huyu alipigwa kipande. Usiweke matumaini ya kupata haki kwenye mahakama za majaji wa aina hii.
Tundu Lissu kafanya 'timing' nzuri sana kwa sababu Mbarouk kashatajwa mapungufu yake kwenye utetezi wa Lissu, atafanya makosa ili Lissu apate sema 'si mnaona.

I told you! Naamini Mbarouk atakuwa makini kulinda integrity yake, by the way jamaa anamalizia LLB pale OUT soon.
 
RUFAA ya kupinga kuvuliwa ubunge ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), imepangwa kusikilizwa Septemba 20, mwaka huu, mbele ya majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa; Natalia Kimaro, Mbarouk Salim Mbarouk na Salum Massati.

Kwa mujibu taarifa za kikao cha Mahakama ya Rufaa cha Arusha, rufaa hiyo iliyofunguliwa na Lema akipinga uamuzi uliotengua ubunge wake kufuatia shauri lililofunguliwa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, inatarajiwa kusikilizwa kwa siku moja ambapo baada ya hapo itapangwa tarehe kwa ajili ya kutoa uamuzi.

Awali, Lema kupitia wakili wake, Method Kimomogoro, aliwasilisha kwenye mahakama hiyo hoja 18 za madai akipinga kutenguliwa kwa ubunge wake na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Aprili 5, mwaka huu.

Kwenye baadhi ya madai hayo, Lema aliiomba Mahakama ya Rufaa kutengua uamuzi wa Mahakama Kuu, uliotengua ubunge wake, huku akiitaka imtangaze kuwa mbunge halali wa Jimbo la Arusha Mjini.

Aidha, aliitaka mahakama hiyo ya juu, iwaamuru walalamikiwa katika shauri hilo walipe gharama za rufaa hiyo pamoja na zile za kesi iliyomalizika kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Arusha.

Katika madai mengine, Lema anamlalamikia, Jaji Gabriel Rwakibarila, aliyesikiliza kesi hiyo kuwa, alitoa uamuzi wake kwa kuzingatia maneno ya uvumi, huku akipuuza ushahidi uliotolewa mahakamani hapo.

Lema anadai kuwa, Jaji alikosea wakati alipoamua kuwa mpiga kura yeyote anaruhusiwa kupinga matokeo ya uchaguzi hata kama haki zake za msingi hazijaguswa.

Kesi hiyo iliyotengua ubunge wa Lema, ilifunguliwa na wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); Mussa Mkanga, Agness Mollel na Happy Kivuyo, wakidai kuwa wakati wa kampeni mbunge huyo alimdhalilisha mgombea mwezake, Dk. Batilda Burian kwa kutumia lugha za matusi.


Source: Tanzania Daima

Mhhhh sidhani kama Lema atashinda kesi hii maana Naliona jina la Jaji Mbarouk Salim Mbarouk ambaye ametajwa kwenye Ripoti maalum ya TUNDU LISSU aliyoitoa kwenye kamati ya Haki, Kinga na maadili ya Bunge. Hofu yangu ni kuwa Watataka kuionesha Chadema kuwa wao ni Majaji makini!!! Hebu Tusubiri tuone, ila dalili nayoiona ni GIZA kwa Lema
 
hapa hamna kitu lema atulie tu aendeleee na kazi yake ya ujangiri kama zamani na kukwiba magari ya watu arusha kama alivyotuhumiwa na zombeee kwakuwa wanajuana vizuri..ubunge asahau kwa sasa

kumbe bado una ule ugonjwa wa kichwa! samahan sikufahamu mapema
 
Angalizo:

Huyo jaji mbarouk salum mbarouk,ni jaji kwa magamba na jk lakini kikatiba si jaji wa jmt na lolote atakalo fanya ama maamuzi atakayotoa hayatambuliki
(kwa sasa ndio mwanafunzi wa sheria chuo kikuu huria)

akataliwe ili awekwe jaji anaestahili kwa mujibu wa katiba ya jmt

nawakilisha
 
Angalizo:

Huyo jaji mbarouk salum mbarouk,ni jaji kwa magamba na jk lakini kikatiba si jaji wa jmt na lolote atakalo fanya ama maamuzi atakayotoa hayatambuliki
(kwa sasa ndio mwanafunzi wa sheria chuo kikuu huria)

akataliwe ili awekwe jaji anaestahili kwa mujibu wa katiba ya jmt

nawakilisha

kweli.. Kwa mujibu wa Katiba hajakidhi vigezo vya kuwa Jaji huyu jamaa.. Ni vyema akakataliwa mapema (Japokuwa sijui taratibu za kumkataa jaji wa mahakama ya Rufani)
 
Imekaa vizuri Lema atarudi bungeni namuamini sana jaji Salum Massati 99.9% pia na Natalia Kimaro 80% lakini huyu walakini Mbarouk Salim Mbarouk 50%

Mkuu naunga mkono hoja ila Mbarouk 30% namwamini. Huyu yuko kwenye orodha ya Tundu Lissu.
 
Kuna tetesi zilishaletwa hapa kuwa huyu Jaji Gabriel Rwakibarila alipooza miguu. Hebu mtu athibitishe pls
 
Uzuri katika case hii ni kwamba tuna majibu ikiwa itaamuliwa tumeshindwa. Itakuwa ni yale yalee. Kesi ya nyani kapewa ngedere wakati nyani ni boss wake ngedere. Ki-ukweli kwenye jamii ya kimasai mwanamke hawezi kuwa kiongozi na hizo ni mila zao hazihusiani na watu wengine na lema alikuwa anawaambia wamasai japo wagogo, wazaramo etc.. walisikia pia
 
Back
Top Bottom