Hujuma Pantoni za Kigamboni

Hujuma Pantoni za Kigamboni

The Fixer

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2008
Posts
1,365
Reaction score
596
Wadau,
Ipo haja ya Mamlaka husika kuingilia kati swala la kivuko hapa kigamboni, Round trip la hili pantoni kubwa siku hizi dakika 50 badala ya dakika 25.

Pantoni linatembea na injini 2 badala ya 4. Mafuta yanauzwa tu juu kwa juu, Mkuu Mwakyembe najua unapitia hapa na kama utakuwa hujaona lakini najua Vijana wako watakuletea hizi taarifa.

Wizi wa mafuta kwenye hizi pantoni zimezidi
 
Wadau,
Ipo haja ya Mamlaka husika kuingilia kati swala la kivuko hapa kigamboni, Round trip la hili pantoni kubwa siku hizi dakika 50 badala ya dakika 25.

Pantoni linatembea na injini 2 badala ya 4. Mafuta yanauzwa tu juu kwa juu, Mkuu Mwakyembe najua unapitia hapa na kama utakuwa hujaona lakini najua Vijana wako watakuletea hizi taarifa.

Wizi wa mafuta kwenye hizi pantoni zimezidi

Wanaiba mafuta wanapeleka wapi?
 
Panton kubwa limechoka , anzia sakafu ya chini kwenye mlango. Engine zake ndio usiseme.
 
yanatuia engine moja....siku zote

na wizi wa mafuta upo siku zote
 
Kama viongozi wa wa juu wa umma wanaiba shilingi billioni 300, wewe unataka hao walala hoi wa pantoni wale nini?? Ufisadi wa mabillioni ya wananchi umeshahalalisha kila kitu. Hata wanachofanya panya road ni namna ya hao vijana kumwaga hasira zao kwa serikali..... Pengine tu Panya Road wamekosea kidogo, wangejiita Escrow Road, na wangeanzia Masaki, Mikocheni, kudai pesa zao.
 
Hivi usalama mle upoje? life jacket na maboya yanakidhi idadi?

Samahani! ule mpango wa daraja umeishia wapi?
 
Injini Inatumika Moja,inaenda Kama Mdudu Kaa,linazunguka Kama Linaenda Kurasini Linarudi Kama Linawapeleka Zanzibar Kwa Sh,200 Linawarudisha Tena Kurasini Ndo Baadae Linaenda Kuweka Nanga Upande Upande

Hahahaaaa.....yani lile ni jongoo. Nilishindwaga kujua naelekea wapi,kwamaana nilizungushwa mara liende ubavu. Yani ni ovyo ovyo!
 
Bila ya kuchukuliwa kwa hatua stahiki na kali zaidi ipo siku itawapotezea muda watumiaji hata zaidi ya masaa 3 . Tunalikuza tatizo wenyewe
 
Mkuu @ Dr Faustine Ndugulile Mbunge unayetumia njia hii - Hebu lifanyie kazi hili swalaa
 
Hivi hii pantoni mara ya mwisho kufanyiwa service ni lini

Dude linafanya kazi 24hrs no service

Lakini ndio mambo ya tanzania hayo..
 
Wadau,
Ipo haja ya Mamlaka husika kuingilia kati swala la kivuko hapa kigamboni, Round trip la hili pantoni kubwa siku hizi dakika 50 badala ya dakika 25.

Pantoni linatembea na injini 2 badala ya 4. Mafuta yanauzwa tu juu kwa juu, Mkuu Mwakyembe najua unapitia hapa na kama utakuwa hujaona lakini najua Vijana wako watakuletea hizi taarifa.

Wizi wa mafuta kwenye hizi pantoni zimezidi

Muda siyo mrefu watawatoa watu sadaka/Kafara,tena kipindi cha upepeo Mkali wa bahari kama huu wa sasa!

Yaani Nchi hii ni aibu tupu-Mita hata mia mbili haifiki toka Ikulu bado watu wanafanya madudu mchana kweupe!
Hah Kumbe hata Ikulu yenyewe wanapiga madili nilitaka kushau!-Maisha Bora kwa Kila Mtanzania



NB; Kwenye hili kunajambo linanipa shida Mbunge amekuwa mkimya kwenye issue ya Pantoni sijui kuna nini!
 
Suluhisho ni dogo tu!! Ferry ya kuvuka inahitaji kubinafsisha sector hiyo !! Waje wawekezaji kadri ya kukidhi haja ya wasafiri...
yaani wasafiri 1000 kwa pantoni 5 hadi 10 zichuana hapo !! na kila idadi ikiongezeka pantoni ziongezwe !! Ndo tutaendelea, Kwani mteja (msafiri) ni mfalme, Na ni haki yake kusave time yake " time is money "
The Fixer Barasu KATIBUA The Boss
 
Last edited by a moderator:
Mombasa kuna pantoni za ya 5 na abiria ni bure.
Unalipa kama una mizigo mikubwa pamoja na magari tu.
Na pantoni zao ni ajab . Sisi leo tunawatoza raia gharama hii ya kuvuka ambapo hii ni service ya lazima kutoka serikali kuwapa wakaazi kivuko.
Wizi umezidi sana nchii kiasi inatia kichefu chefu.
Leo kuingia airport kwa fedha lakini hatuoni chochote ku improve hali ya airport ukuienda chooni ni aibu.
Mjini parking kila mahali kwa mwezi zinakusanywa billions . Hakika barabara za dar zote zingekuwa za lami bila ya mashimo lakini watu ni mijizi ya kutupwa.
Mabango ya matangazo na billboards yame jaa kila pembe ya Dar . Kuna bank moja inalipa $600,000 kwa mwaka kulipia billboard mija tu ! Hebu fikiria billboard ngapi zipo mjini ? City wanajitajirisha kwa wizi na rushwa.
Hakika jiji hili lingekuwa zaid ya dubai kwa usafi kama sio ufisadi.
Kodi zina ingia matumboni mwa watu.
This country needs someone who could turn it upside down ndio tutaenda
 
Back
Top Bottom