Huenda waliokuwa wakivujisha siri za Serikali walikuwa ni wasaidizi wa Rais, hawakupendezwa naye

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Binadamu wana tabia ya kinafiki sana, wanacheka na wewe na kukushauri Kisha wanautoa ushauri wao nje kwenda kukuangamiza. Tangu aingie mama Samia suluhu uvujaji wa Taarifa umepungua Jambo linaloonyesha Kwamba waliokuwa wanavujisha siri ni watu wale wale waliokuwa wanapaswa kuzihifadhi.

Naamini Mama Samia hana timu mpya sana na wala waliomzunguka siyo ndugu Wala rafiki yake Bali ni Watumishi wale wale waliomzunguka JPM. Watumishi hawa wanasali na wana imani lakini kikubwa wanautambuzi wa mema na mabaya. Wengi wa watendaji kwenye ofisi hii nyeti wameapa kuiilinda nchi ndipo wamlinde kiongozi wa nchi. Ikitokea kiongozi mwenye nchi akaisaliti nchi watu hao lazima watatafuta namna ya kuvujisha taarifa kudhibiti damage.

Kwa muktadha huo naanza kuamini wbado Wapo Wazalendo ikulu ambao pamoja na kukabidhiwa nafasi nyeti wanaweza kutoa taarifa wanazodhani zinaliumiza Taifa ili wananchi wajue na mwenye nchi ajue wananchi wanamjua kuliko anavyojijua.

Kosa lililofanywa na mfumo ni kupambana kuzuia taarifa zisitoke badala yakudhibiti uharibifu wa Taifa letu. Uwekezaji uliofanywa kudhibiti Siri ulikuwa mkubwa na wanufaika wanaweza kuwa ni walewale waliovujisha Siri ndio walipewa jukumu lakujitafuta bila kujua ni vigumi kujipata.

Nimshukuru Mama Samia kuua mradi huu wakupambana na watoa Siri badala yake akaamua kutenda yaupendezayo mfumo Hadi ukaona hakuna damage. Asipotoke akaendelea kudhibiti maana anaowatumia kudhibiti ndio hao hao wanaovujisha Siri ili waendelee kupewa kazi ya kudhibiti.

Nasema ni system kwa sababu hata wizi wa mabilioni uliofanywa kupitia EPA na Escrow haukujulikana kwa serikali kudhamiria ujulikane ila watu wachache Wazalendo walivujisha Siri na nyaraka watu wakanyanyuka nazo Bungeni nakumfanya Mzee wa Msoga asafiri nje akatulie Kwanza kutafakari anapangua vipi siri zilizovuja.

Wabarikiwe watoa siri wanaotufanya tujue mianya ya wizi na kuwafanya Wazalendo kuiziba. Leo hii hata taarifa za uteuzi hazivuji japo sasa nazo zinakosa vetting ya kutosha hadi makapi nayo yanapitishwa na kuwapa agenda Wasaga sumu kupata agenda mitandaoni.
 
Nchi kama US suala la uteuzi siyo siri. Tena wasaidizi wa President wanasema wazi kabisa na POTUS anaweza hata kumsema mtu even before appointment. Sisi shida yetu kubwa ni "focus". Kama taifa hatujawahi kuwa na " focus" hata kidogo.

Hii imeanza na Mzee Nyerere mwenyewe. Wazungu wanafahamu nini wanataka. Sisi tuna shida. Hatuna "focus". US wamewekeza kwenye intelligence community.

Sisi Intel community yetu ni ya hovyo sana. Imejaa nepotism ya hali ya huu. Iko weak sana. Ukiwa na strong and brilliant Intel community, utapata " focus" na kuisimamia. Nchi itasonga mbele sana.
 
Ni kweli kabisa kama Ikulu pailigeuzwa kuwa Blood shedding scene ingekuwa ni kosa wasingevujisha.
 
Nchi kama US suala la uteuzi siyo siri. Tena wasaidizi wa President wanasema wazi kabisa na POTUS anaweza hata kumsema mtu even before appointment. Sisi shida yetu kubwa ni "focus". Kama taifa hatujawahi kuwa na " focus" hata kidogo...
Tatizo wanaoteuliwa wanateuliwaje? US hata CIA wanajiliwa kwa platform za wazi kabisa.
 
Ukiwapa uhuru watu wa kuongea huwa vya kuongea vinaisha, wanakosa vya kuongea wanaanza umbea na majungu. Ukiwanyima wanaanza kutafuta vya kuongea kwa nguvu. Mama aliwaambia waacheni waongee jamani na yeye anasikiliza sana.
Magenge yaliyokuwa yanapanga njama za uhalifu, wizi, mauaji nautekaji yamepungua nguvu kwa sasa. We are watching
 
Nchi kama US suala la uteuzi siyo siri. Tena wasaidizi wa President wanasema wazi kabisa na POTUS anaweza hata kumsema mtu even before appointment. Sisi shida yetu kubwa ni "focus". Kama taifa hatujawahi kuwa na " focus" hata kidogo.

Hii imeanza na Mzee Nyerere mwenyewe. Wazungu wanafahamu nini wanataka. Sisi tuna shida. Hatuna "focus". US wamewekeza kwenye intelligence community.

Sisi Intel community yetu ni ya hovyo sana. Imejaa nepotism ya hali ya huu. Iko weak sana. Ukiwa na strong and brilliant Intel community, utapata " focus" na kuisimamia. Nchi itasonga mbele sana.
Kweli mkuu sisi tunajua adui yetu ni CHADEMA na siyo umaskini na magonjwa
 
Tuna kwenda safari ambayo tunabadili dereva lakini shinda kubwa ni kwamba kila dereva hajui tunako kwenda na ndani ya bus abiria wamelala
 
Back
Top Bottom