DOKEZO Huduma za Tiba Ocean Road hadi wagonjwa waandamane?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,826
35,832
Imekuwa ni kawaida iliyozoeleka Ocean Road kwa mgonjwa kufika kwenye miadi ya tiba (kama ilivyopangwa) asubuhi saa moja na kuja kupata huduma saa nne usiku.

Hutokea wakati hata hiyo usiku anaweza bado tiba asipate. Hakuna taarifa zozote zinazotolewa kuhusiana na ucheleweshwaji huu zaidi ya kuwa subirini.

"Mazingira wezeshi kabisa ya rushwa."

Wenye pesa zao, ma V8, wenye utambulisho kutoka Zenji huko nk, hao hutibiwa tiba hizo hizo bIla usumbufu na kwa wakati kama wanavyofika na kujiondokea.

Wagonjwa hawa wengi wao ni wazee waliodhoofu sana. Kukaa hospitali bila kula kutokea asubuhi hadi usiku, ni jambo la kushangaza sana.

Kwa wiki kama tatu zilizopota hali ilionekana kutengamaa baada ya malalamiko makali. Hata hivyo hali imeanza kurejea kule kule tena.

Hali hii hadi lini? Au hadi wagonjwa waandamane kama wale wa TRL Dodoma? Hapo hadi Magogoni si ni umbali wa pua na mdomo?

Acheni kusumbua wagonjwa. Kwa nini miadi isiwekwe kumwezesha mgonjwa mmoja kutokaa zaidi ya saa moja kwenye foleni akisubiri?

Rushwa hadi kwa mgonjwa aliye taabani?

Kwani tunakwenda misikitini au makanisani kufanya nini?

Kila mahali shida zile zile za upigaji. Tutafika tukiwa tumechoka sana.

Mola atufanyie wepesi.
 
Pole mkuu. Ukitaka kuijua hii nchi, we pata shida. Ndugu yangu alifariki nikiwa namuona, nurse wa zamu kila nikimuita aongee na waliojuu yake anasema ndo kakabidhiwa shift nimuache kwanza, baada ya mtu kufariki anajifanya ku sympathize.
Mie wangenilaza polisi maana ningemshushia kipigo cha kufa mtu huyo nesi. Yani ningempiga haswaaa
 
Pole mkuu,
Ukitaka kuijua hii nchi, we pata shida. Ndugu yangu alifariki nikiwa namuona, nurse wa zamu kila nikimuita aongee na waliojuu yake anasema ndo kakabidhiwa shift nimuache kwanza, baada ya mtu kufariki anajifanya ku sympathize,

Ninadhani uwepo wa wingi mkubwa wa medical attendants unakuza tatizo hili.

Hata waliopaswa kuwa wanafanya usafi wanashughulika na wagonjwa kuliko na madili. Wana kauli mbovu na hawana maadili. Hao ndiyo bomba la rushwa, kupenyeza wagonjwa wa connection, kejeli, usumbufu nk.

Kama yalivyokukuta hali ni mbaya sana. Matibabu ya mionzi ni jumatatu hadi ijumaa. Mgonjwa anakuwa yupo hospitali tokea saa moja hadi saa nne usiku kila siku.

Mgonjwa huyu anakula saa ngapi? Vipi kuwapo kwenye mazingira hatarishi ya magonjwa mengine kwa muda mrefu?

Wagonjwa hawa hata kwa afya zao tu wako hatarini mno kwenye mlundikano wa wagonjwa wengine. Ni kukosekana kwa huruma kiasi gani huku?

Hadi wagonjwa waandamane?

Kwa kweli ni Mungu tu.
 
Wao wakipata mafua kidogo tu wanakimbilia nje ya nchi , balaa sana hii, mtafuteni ummy mwalimu labda atasaidia jambo hapo maana nchi yangu bila kuandikana magazetini, mitandaoni na kwenye Ripoti za CAG kichere hakuna kitu kinafanyika.
 
Deep down niliwaza nimpige ata kibao, ila gharama yake ingekua ni kubwa kwangu na kwa familia, ukizingatia ni mwanamke
Hio sheria gani ambayo haitambui kwamba mtu anapofiwa kwa uzembe wa nesi anaweza ghafilika?

Huyo ndugu angekuwa ni mama yako mzazi bado ungewaza hizo gharama?
 
wao wakipata mafua kidogo tu wanakimbilia nje ya nchi , balaa sana hii, mtafuteni ummy mwalimu labda atasaidia jambo hapo maana nchi yangu bila kuandikana magazetini, mitandaoni na kwenye Ripoti za CAG kichere hakuna kitu kinafanyika.

Kila kitu wamefanya siasa wakijua wagonjwa mahututi hawa watapigia wapi kelele?
 
Kuna actions zinakuaga kama involuntary unajikuta tayari upo rumande. Umefikaje hujui
Aisee acha tu, mimi wangenilaza ndani kwa kweli ila maaskari wenyewe wangenitoa mapema maana kesi inaeleweka kipigo ni haki yake.
 
Mie wangenilaza polisi maana ningemshushia kipigo cha kufa mtu huyo nesi. Yani ningempiga haswaaa
Asalaam mkuu, napenda mno kusoma comments kama hii ya kwako ,push back ukiona haki yako inapuuzwa why uje kulalama humu?na mbaya zaidi uzi huu sio kama ni whistle blower ,hauna facts zozote kama, tarehe yaliyotokea haya, majina ya watumishi (angalia name tag zao),video za wagonjwa wakisubiria huduma etc
 
Unaweza kuta mashine ya mionzi ipo moja tu na yenyewe imeishiwa mionzi, hii ndo bongolala bhana.....
 
Asalaam mkuu, napenda mno kusoma comments kama hii ya kwako ,push back ukiona haki yako inapuuzwa why uje kulalama humu?na mbaya zaidi uzi huu sio kama ni whistle blower ,hauna facts zozote kama, tarehe yaliyotokea haya, majina ya watumishi (angalia name tag zao),video za wagonjwa wakisubiria huduma etc

Hauna facts zozote wala tarehe?

Nimekwambia hali ilikuwa Imekuwa bora yapata wiki 3 zilizopita (baada ya kulalamika lalamika sana) lakini hali imeanza kuzorota tena.

Huwezi kuona kuwa siku za karibuni zinazotajwa hapo hata jana tu itakuwa inahusika?

Kimsingi kuweka wazi, hata jana tu hali ilikuwa mbaya zaidi. Wagonjwa kadhaa hata kufikia usiku huo bado hawakuweza kutibiwa pamoja na kuwa walikuwa hapo kuanzia 0700.

Angalia post #2 kwenye Uzi huu:

Rais tusaidie MRI ya Muhimbili MOI itengenezwe

Angalia post #61 kwenye uzi huu:

Ukaguzi wa CAG usiozingatiwa ni wa nini?

Kwani wewe ni mmoja wa wanufaika kwenye huku kutuchulia vifo prematurely? Au ungependa tukaandikie malalamiko kama haya tukiwa makaburini ndugu?

Kwamba unakomaa vipi, physically? Wakati unaambiwa subiri, japo longo longo unaziona?

Nenda ocean road kaone. Labda wawe wamejirekebisha tena leo.

Ni hayo tu ndugu mjumbe.
 
Unaweza kuta mashine ya mionzi ipo moja tu na yenyewe imeishiwa mionzi, hii ndo bongolala bhana.....

Akiwapo JPM hizi longo longo zilikwisha. Angalia post #2 kwenye uzi huu:

Rais tusaidie MRI ya Muhimbili MOI itengenezwe

Ocean road ukisikia leo matibabu ya mionzi hamna machine ya radiation mbovu, wewe tupia rupia tu.

Chap chap machine inasikia na unapata tiba yako na machine hiyo hiyo.

Siyo siri kuwa kwenye zama za jiwe upuuzi huu ulitoweka.
 
Hauna facts zozote wala tarehe?

Nimekwambia hali ilikuwa Imekuwa bora yapata wiki 3 zilizopita lakini hali imeanza kuzorota tena. Huwezi kuona kuwa siku za karibuni zinazotajwa hapo hata jana tu ni wazi kuwa itakuwamo?

Kimsingi kuweka Kila kitu wazi, hata jana tu hali ilikuwa mbaya zaidi na wagonjwa kadhaa hata kufikia usiku huo bado hawakutibiwa pamoja na kuwa walikuwa hapo kuanzia 0700.

Angalia post #2 kwenye Uzi huu:

Rais tusaidie MRI ya Muhimbili MOI itengenezwe

Angalia post #61 kwenye uzi huu:

Ukaguzi wa CAG usiozingatiwa ni wa nini?

Kwani wewe ni mmoja wa wanufaika kwenye huku kutuchulia vifo prematurely?

Unakomaa vipi, physically? Wakati unaambiwa subiri, japo longo longo unaziona?

Nenda ocean road kaone. Labda wawe wamejirekebisha tena leo. Kumbuka around wiki tatu zilizopita baada ya kukomaa nao sana walibadilika.

Ni hayo tu ndugu mjumbe.
Hii ya Muhimbili ndio keroo zaid, i was there, watu wa emergency wanakuja hapo mliokuwa kwenye foleni mtangojea, kuna mgonjwa wa mionzi akiingia ni 2/3 hours kungojea mind you bado wa kufanya vipimo wako msululu mrefu. Na machine ni 1
 
Back
Top Bottom