Huawei yajidhatiti

Ku support apk sio issue pia sababu kuna os tayari zinasupport apka kama vile tizen ya samsung, sailfish os ya Jolla na BB10 os ya blackberry na zote hazikufanikiwa. Kuna mambo mbalimbali kama vile
-kuto support google service, hapa haimaanishi tu app za google ndio zitakuwa hazipatikani bali app zote ambazo zinahitaji hii service mfano hio app niliyoitaja hapo juu yaani snapchat, hata uki sideload apk haitafanya kazi.
-runtime, kama utakumbuka android za zamani kama vile jelly bean kushuka zilikuwa zinatumia dalvik runtime ilikuwa slow sana na android ilikuwa nzito baadae google akahama kwenda art tukaona mabadiliko makubwa kuanzia kitkat, os zote zinazosideload apk zinakuwa na tatizo hili inachukua muda sana toka uclick app ya android mpaka kuja kufunguka. Ngoja tuone kama wana maajabu ila nategemea hapa pia kuwa na tatizo.
 
Akifanikiwa kuwa convice makampuni yote ya kichina kutumia OS yake atakuwa amemaliza.
Maana simu zote % kubwa ni Chinnes
 
Alishindwa blackberry hii vita tena wakati ule ndo alikuwa smartphone super brand huku android ndo kwanza ilikuwa inachipukia lakini ikaibuka kidedea hadi wakaruhusu android platform kwenye balackberry os lakini wapi na leo hii wameamua kuungana tu na android mana hakuna namna.
Kampuni za kimarekani sio nzuri kwenye mashindano ya kibiashara hata kidogo. China wameendelea sana ila bado wanasafari ndefu sana kuifikia Marekani, wasipokuwa makini wanapotea kama walivyopotea wengine.
 
Mi mwenyewe nimeliona hilo tangazo, wanasema itaitwa Ark OS sasa swali langu ni vipi wanapima hiyo speed difference na kwa tekinolojia gani wanatumia kutambua hilo?
Wanaonekana kujiandaa kweli maana wamesha sambaza copy 1.million za simu zao zinazotumia hiyo OS kufanya test.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…