How are you examplifying yourself to the younger generation?

How are you examplifying yourself to the younger generation?

Gorgeousmimi

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
9,296
Reaction score
7,688
Habari za asubuhi wapendwa wangu.

Utandawazi unatubadilisha mno fikra zetu,mienendo yetu,ule ukuta au usiri/aibu ulokuwepo awali kati ya wakubwa kuficha mambo yao na vijana wadogo kuyajua wakiwa na umri mdogo hayapo tena.Tukianza hapa Jamii Forums kuna mchanganyiko wa watu wengi
.

Je wewe kama mtu mzima ulopevuka unajiainisha vipi mbele ya hadhira hii?


  • Unajitambulisha vipi kwa vijana wadogo ambao wanakuangalia na unatakiwa uwe mfano bora kwao,mfano wa kuiga?
  • Michango yako inawafunza nini kuhusu maisha?

Nasikia sana watu wakisema hiki ni kizazi cha nyoka na naamini ni kweli.Siku hizi watu wamenyimwa haya,mtu mzima unamkuta anapayuka tu na kuongea mambo ya ajabu,mbele ya vijana wadogo.

  • Mipaka imeenda wapi?
  • Hekima na busara zimeenda wapi?
  • Heshima imeenda wapi?

Kitu kingine ni kwamba je kuna kitu kinachotupa ujasiri wa kujiona kila tunalofanya tuko sahihi?Malezi tulokulia yanaathiri mno maisha kwa namna moja au nyingine.Wale watu ambao hawana mipaka wamekosa good mentors and examples to look up to in their upbringing?Au ndo utandawazi unazitawala fikra zetu mpaka tunasahau maadili na mienedo mema?(Are we brainwashed)?

Ni muhimu kuwa na diversity kwamba ukiwa upo na watu kama ww uwe uhuru na sehem ambayo hujui kuna mchanganyiko wa watu wa aina gani unakuwa makini.Jamani utandawazi umefungua mambo mengi lakini sisi kama watu wazima tunatakiwa tuwe ngangali na kuweka mipaka ili kuwajenga younger generation katika misingi bora.

Kuna availability ya kila kitu siku hizi lakini isiwe ndio sababu ya kujilemaza na haimaanishi ndo tujiachie tu na kusahau majukumu yetu kama grown ups.Tunajidhalilisha sisi mbele ya vijana wadogo na tunajidharaulisha.Majukumu yako kama mtu mzima hayaishii kwenye familia yako tu,yanaextend hata ukiwa nje na watu baki.

Jinsi unavyojiwakilisha ndivyo jinsi watu wanavyokuchukulia.Ukiwa kigeugeu leo unajiwakilisha kama mtu mzima na kesho unaongea maneno ya kipuuzi.Younger generation hawatokuchukulia serious.Kwanini waone wewe ni mfano bora wakati huoneshi upevu wa fikra na huna msimamo?Be an example,A change starts when you are ready to make it.

Karibuni tuchangie
 
Accept change

kwanza kabisa sisi grown ups tunabidi tukubali kwamba change is an unavoidable and vital part of life. Accepting change and adjusting to it, inasaidia kujua namna gani ya kuweza kudeal with the young generation na kuweza kuwa mfano bora.

Make Time for them


Unapoweza kutenga muda na kuwasikiliza hawa madogo inasaidia sana kutengeneza uhusiano mzuri na kuondoa ile nidhamu ya uwoga ambayo most of the times sisi grown ups tunatengeneza. Unapotenga muda kwa ajili yao inawasaidia wao kuwa huru, wao kucommunicate, kujifunza na pia kupata the ability to seek and accept help from us.

Teaching them


Inabidi sisi grown ups tuelewe kwamba mambo yamebadilika, personally huwa najitahidi kuwafundisha na kuwahimiza umuhimu wa kuset goals, kuwa na expectations nzuri za maisha yao na umuhimu pia wa making the right choices and decisions
 
Watu wengi kipindi hiki hawataki kujikubali kuwa wao ni wanamna gani hasa, hilo la kutokujitambua ndio tatizo kubwa sana katika kizazi chetu.
tunapenda maisha ya kuigiza zaidi kuliko vinginevyo.
 
Malezi tuliyolelewa na ndio siku zote yanaleta utofauti.Hao waropokaji na wasiojiheshimu ni kutokana na malezi au mazingira yanayomzunguka.Kuna mama mmoja jirani nilikuwa namuona mstaarabu sana siku hiyo nimeenda kwake aiseee nilijuta yani alikuwa anawatukana wanae hadi nikaona aibu na kwa jinsi nilivyoona mazingira ya pale na matusi mazito kwa watoto nikasema piga ua watoto lazima na wao waje kuwa watukanaji wazuri
 
watu wengi kipindi hiki hawataki kujikubali kuwa wao ni wanamna gani hasa, hilo la kutokujitambua ndio tatizo kubwa sana katika kizazi chetu.
tunapenda maisha ya kuigiza zaidi kuliko vinginevyo....
Kuna wengine wanajiona wanajitambua lakini ukitazama matendo yao sasa utashangaa yanaenda kinyume kabisa na maneno yao.Hata sijui tatizo ni nini kwa kweli!!
 
watu kibao wanajidai hawajielewi na kujiona vijana ilhali wao ni watu wazima kukopi na kupaste life style za watu imetuathiri
Unajua hiko ni kitu kingine najiuliza sana je kuna watu ambao they never grow up?Au ndo hawakufanya wanayoyafanya utotoni wanafanya ukubwani??
 
Unajua hiko ni kitu kingine najiuliza sana je kuna watu ambao they never grow up?

My dear hakuna ambae hakui ndo mana nkakuambia ni kujitoa ufaham tu na kujifanya hawajielewi ila ukweli uko pale pale hakuna asiekua na umri haustuck hua unasonga mbele wala haurud nyuma.
 
Malezi tuliyolelewa na ndio siku zote yanaleta utofauti.Hao waropokaji na wasiojiheshimu ni kutokana na malezi au mazingira yanayomzunguka.Kuna mama mmoja jirani nilikuwa namuona mstaarabu sana siku hiyo nimeenda kwake aiseee nilijuta yani alikuwa anawatukana wanae hadi nikaona aibu na kwa jinsi nilivyoona mazingira ya pale na matusi mazito kwa watoto nikasema piga ua watoto lazima na wao waje kuwa watukanaji wazuri
Ni sawa kabisa watoto wanaiga kwa wakubwa hasa wakiwa na umri mdogo hawana upeo mzuri wa kutofautisha zuri na baya....Na isitoshe anaona mama anafanya kwann na mm nisifanye?Makuzi yanaathiri wengi sana...
 
Kuna wengine wanajiona wanajitambua lakini ukitazama matendo yao sasa utashangaa yanaenda kinyume kabisa na maneno yao.Hata sijui tatizo ni nini kwa kweli!!

Hao unaowaona hivyo wengi ni wale wenye kuiga maisha na mafanikio ya wengine,wajua kuna watu haishi wapasavyo kuwa.
 
Accept change

kwanza kabisa sisi grown ups tunabidi tukubali kwamba change is an unavoidable and vital part of life. Accepting change and adjusting to it, inasaidia kujua namna gani ya kuweza kudeal with the young generation na kuweza kuwa mfano bora.

Make Time for them


Unapoweza kutenga muda na kuwasikiliza hawa madogo inasaidia sana kutengeneza uhusiano mzuri na kuondoa ile nidhamu ya uwoga ambayo most of the times sisi grown ups tunatengeneza. Unapotenga muda kwa ajili yao inawasaidia wao kuwa huru, wao kucommunicate, kujifunza na pia kupata the ability to seek and accept help from us.

Teaching them

Inabidi sisi grown ups tuelewe kwamba mambo yamebadilika, personally huwa najitahidi kuwafundisha na kuwahimiza umuhimu wa kuset goals, kuwa na expectations nzuri za maisha yao na umuhimu pia wa making the right choices and decisions
You are a good example rafiki hata hapa JF nakukubali sana!!🙂
 
Hivi humu mnajuana fulani ana umri gani ? Au ndio mnaangalia comments za mtu ndio unasema fulani babu inabidi awe mfano? Usije kujikuta unataka kuwa mfano kwa baba/mama yako.....even fools grow old!
 
Hivi humu mnajuana fulani ana umri gani ? Au ndio mnaangalia comments za mtu ndio unasema fulani babu inabidi awe mfano? Usije kujikuta unataka kuwa mfano kwa baba/mama yako.....even fools grow old!

Kuna watu wapumbavu kabisa humu. Kwa kuangalia tu mabandiko ya watu kwao inatosha kujifanya wanaujua umri wa mtu.

Na kudhihirisha zaidi upumbavu wao, mtu unaweza hata ukatunga stori tuseme ya mwaka 1983 ukiwa Canada ukisoma shahada yako yako ya uzamili na hao wapumbavu wakaingia mkenge na kujifanya wanaujua umri wako kwa kuona tu umeandika hivyo.

Na hapo hata hawakujui, hawajawahi hata kukuona, hata ulichokiandika hawana uhakika nacho, lakini wanafikia hitimisho la kujifanya wanaujua umri wako.

Kibaya zaidi unakuta wanajiaminisha kabisa kuwa wanachokisadiki ndicho sahihi. Huo ni zaidi ya ujuha na ujinga. Ni upumbavu maradufu.
 
Back
Top Bottom