Housegirl wa Rais Karume alivyoniokoa soko la Sabasaba Morogoro wakati tunatoka Malawi. Dada, barikiwa popote ulipo - uliniokoa

Superbug

JF-Expert Member
Jan 31, 2018
12,417
30,927
Duniani bado kuna watu wema. Nakumbuka Housegirl wa mh Rais Karume tulipanda basi toka Malawi. Miaka ya 2007/8. Nilimpigisha Sana story njiani mpaka akafurahi sana.

Tulipofika Msamvu usiku kabla stend mpya haijajengwa wakaja wahuni wengi including vibaka. Yule dada kwa kutambua hatari iliyokuwa inanikabili akaniambia twende nyumbani hapa siyo salama. Akakodi taxi tukaenda mpaka kwao maeneo ya soko la mitumba la Sabasaba.

Tulipofika hapo ikakonekana Mimi itakuwa ngumu kulala pale kwao na mbaya zaidi ilikuwa saa nane usiku na wahuni walikuwa wengi sana maeneo yale.

Yule dada akampa dreva tax hela na akamuambia anipeleke guest salama na nikipatwa na tatizo yeye dreva tax atawajibika na alichukua namba yake akahakikisha anaipiga inaita.

Nilipewa hela ya guest pia na yule dada. Dreva taxi akanipeleka guest moja nzuri karibu na soko kubwa mjini Morogoro. Kesho yake nikaendelea na safari ya kwenda Mwanza.

Naomba wewe dada kama ni memba humu tuwasiliane, ulinisaidia mnooo.

Tulikaa siti ya nyuma kabisa ya basi na Wamalawi. Na katika maongezi yetu tuliwafunika Mambo mengi kuanzia exposure mpaka lugha ya Kiingereza.

Mungu mbariki dada yule na familia ya mzee Karume.
 
Hili ndo tatizo la watanzania,Kuna MTU mmoja nae alipataga kituko kama chako,sema yeye ni kutoka kwa boss wake,ilikuwa hivi ,huyu jamaa alikuwa anafanya kazi sehemu kama janitor ,sasa kwenye ile nyumba akapatikana mpangaji Wa kizungu ni mdada,yule mzungu akatokea kuiva sana na yule janitor (kijana Wa Usafi) sasa yule kijana maskini akahisi yule mzungu amekolea kwake,akaja akaniomba ushauri kuwa boss wake inavyoonyesha amempenda ila anashindwa tu kumwambia, nikamwambia asubiri kwani wazungu kumpenda MTU kwao si ajabu na kama itakuwa kimapenzi atamwambia tu,jamaa akaniambia Mimi sielewi ndo maana namwambia hivyo akasema hadi soda wanapokezana then Mimi nasema asubiri!akaachana na Mimi akaenda kuomba ushauri kwa fundi mmoja hivi na yule Fundi nae sijui vipi lakini,akamwambia Huyo kakupenda wala haina shaka na wala haiitaji kuuliza,jamaa kutoka pale akaenda dukani akanunua jinzi la kike na card ya mapenzi akampelekea mzungu,mzungu akaipokea huku akishangaa sana , alipomaliza kuisoma akaanza kulia na kukimbia ndani,akampigia mwenye nyumba simu ili aje amuondoe yule kijana pale,alihofia anaweza bakwa,maana jamaa hana akili,utamtongaje anayekulipa mshahara huo ni uchizi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee nimeishi na wazungu kwa mda,kama we wa kukurupuka unaweza ukasema umependwa ,maana jinsi mtakavyoshirikiana na kutoka out kibongobongo utasema zali la mentali
Hili ndo tatizo la watanzania,Kuna MTU mmoja nae alipataga kituko kama chako,sema yeye ni kutoka kwa boss wake,ilikuwa hivi ,huyu jamaa alikuwa anafanya kazi sehemu kama janitor ,sasa kwenye ile nyumba akapatikana mpangaji Wa kizungu ni mdada,yule mzungu akatokea kuiva sana na yule janitor (kijana Wa Usafi) sasa yule kijana maskini akahisi yule mzungu amekolea kwake,akaja akaniomba ushauri kuwa boss wake inavyoonyesha amempenda ila anashindwa tu kumwambia, nikamwambia asubiri kwani wazungu kumpenda MTU kwao si ajabu na kama itakuwa kimapenzi atamwambia tu,jamaa akaniambia Mimi sielewi ndo maana namwambia hivyo akasema hadi soda wanapokezana then Mimi nasema asubiri!akaachana na Mimi akaenda kuomba ushauri kwa fundi mmoja hivi na yule Fundi nae sijui vipi lakini,akamwambia Huyo kakupenda wala haina shaka na wala haiitaji kuuliza,jamaa kutoka pale akaenda dukani akanunua jinzi la kike na card ya mapenzi akampelekea mzungu,mzungu akaipokea huku akishangaa sana , alipomaliza kuisoma akaanza kulia na kukimbia ndani,akampigia mwenye nyumba simu ili aje amuondoe yule kijana pale,alihofia anaweza bakwa,maana jamaa hana akili,utamtongaje anayekulipa mshahara huo ni uchizi

Sent using Jamii Forums mobile app

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Back
Top Bottom